YALIYOMO
Fonetiki
– Taaluma
inayochunguza
sauti
zote
ambazo
zinaweza
kutumika
katika
lugha
yoyote
ile
na
kutoa
sifa
za
sauti
hizo
bila
kujali
zinatumika
katika
lugha
gani
na
kwa
njia
gani.
(i)
Fonolojia
– Taaluma
inayofafanua
mfumo
wa
sauti
zitumikazo
katika
lugha
mahsusi
na
jinsi
sauti
hizo
zinavyotumika.
Katika
Fonolojia
kinachoshughulikiwa
ni
mifumo
sauti
ya
lugha
maalum.
Wanafonolojia
wameunda
vipashio
maalum
vya
kujadilia
mfumo
sauti
kv.
Fonimu
na
alofoni. Mfumo
sauti
wa
lugha
unajumuisha
vitamkwa
vya
lugha
pamoja
na
mfuatano
wa
vitamkwa
unaunda
silabi
na
muundo
wake,
kanuni
za
kifonolojia,
toni,
kiimbo,
nk.
(ii)
Mofolojia
– Taaluma
inayochunguza
maumbo
ya
maneno
katika
lugha.
Taaluma
inayochambua
na
kuweka
kanuni
za
jinsi
maumbo
tofauti
ya
maneno
yanavyohusiana
katika
sarufi
ya
lugha
husika.
Vipashio
vidogo
kabisa
vya
lugha
vinavyounda
maneno
ya
lugha
vinaitwa
mofimu
mfano
m-tu wa-tu.
Mofimu
ni
vipashio
vinavyoonyesha
uhusiano
uliopo
kati
ya
sauti
msingi
za
lugha
(yaani
fonimu)
na
maana
katika
sarufi
ya
lugha.
Maumbo
toauti
ya
mofimu
moja
yanajulikana
kama
alofoni
za
mofimu
hiyo,
mfano
mtoto
– watoto
– hapa
m
na
wa
ni
alomofu.
(iii) Sintaksia
– Taaluma
inayojihusisha
na
uchambuzi
na
ufafanuzi
wa
muundo
wa
sentensi
za
lugha.
Inaendelea
pale
ilipoishia
mofolojia.
Uchambuzi
wa
kisintaksia
unaonyesha
uhusiano
wa
maneno
na
vipashio
vingine
vinavyojenga
sentensi
za
lugha.
(iv) Semantiki
– Taaluma
inayojihusisha
na
ufafanuzi
wa
maana
katika
lugha
(yaani
maana
ya
maneno
na
sentensi).
(v)
Pragmatiki
– Taaluma
inayojihusisha
na
ufafanuzi
wa
maana
katika
lugha
kwa
muktadha
mahususi
(yaani
muktadha
wa
matumizi).
2 Isimu Tumizi
Ni
uwanja wa
Isimu
unaohusika
na
utumiaji
wa
matokeo
ya
tafiti
za
kiisimu
katika
nyanja
mbalimbali
kwa
lengo
la
kutatua
matatizo
yahusuyo
lugha.
Taaluma
hii
ilianza
baada
ya
Vita
Vikuu
vya
Pili
vya
Dunia
wakati
huo
ilihusika
na
ufundishaji
wa
lugha
kwa
wageni,
mfano
Kiarabu,
Kichina,
Kirusi,
nk.
Baadaye
katika
miaka
ya
1950
– 1960
ulizuka
uwanja
mpya
wa
utafiti
wa
lugha
kwa
kutumia
mashine.
Kwa
hali
hiyo
isimu
tumizi
ilipanuka
na
kujumuisha
nyanja
zifuatazo:
(a)
Ufundishaji
wa
lugha
kwa
wageni.
(b)
Tafsiri
kwa
kutumia
mashine
(c)
Eneo
la
sera
ya
lugha
na
upangaji
wa
lugha.
(d)
Lugha
na
elimu.
(e)
Lugha
na
siasa
(Propaganda
katika
siasa).
3
Isimu
Nafsia
(Saikolojia)
Ni
taaluma inayohusika
na
mambo
yanayowezesha
watu
kujifunza
lugha
mama.
Inamwezesha
kutumia
na
kuelewa
lugha.
Isimu
nafsia
mamboleo
hutumia
matokeo
ya
taaaluma
mbalimbali,
mfano
elimu
viumbe,
sayansi
ubongo,
sayansi
utambuzi,
isimu
ubongo,
nk.
Isimu
nafsia
hutumia
matokeo
ya
isimu
ubongo,
isimu
utambuzi,
elimu
viumbe
ili
kutambua
jinsi
ubongo
unavyochakata
lugha
(language
processing).
Isimu
nafsia
ya
ujifunzaji
lugha
huhusika
na
uwezo
wa
watoto
kujifunza
lugha.
4 Isimu Ubongo
Sayansi
inayochunguza
utendaji
wa
ubongo
na
utendaji
unaohusiana
na
mambo
ya
uelewa,
uzalishaji
na
ujuzi
dhahania
wa
lugha.
Utendaji
huu
unachunguzwa
katika
hali
mbalimbali
za
lugha,
mfano
uneni,
maandishi,
alama
au
ishara.
Isimu
ubongo
inashirikisha
nyanja
zifuatazo
za
taaluma:
a)
Biolojia
b)
Sayansi
ya
kompyuta
Afasiolojia
(aphasiology)
– Taaluma
inayochunguza
matatizo
ya
lugha
wayapatayo
watu
wenye
matatizo
ya
ubongo.
5 Isimu Ujifunzaji Lugha
Taaluma
inayochunguza
jinsi
mtoto
anavyojifunza
lugha
ya
mama
kwa
kuzingatia:
a)
Mazingira
anayopitia
mtoto.
b)
Hatua
anazopitia
katika
kujifunza
lugha.
Mazingira
– Lazima
mtoto
awe
katika
jamii
ya
wanalugha
na
atagusane
nao.
Hatua
– Huangalia
hatua
za
mtoto
katika
kujifunza
lugha.
6 Isimu Historia
Taaluma
inayotalii
jinsi
lugha
zinavyobadilika
kwa
kuchunguza
lugha
zinazoingiliana
kimsamiati,
kisintaksia
na
kimofolojia.
Uchunguzi
huo
hufanywa
kwa
kulinganisha
lugha
mbalimbali
na
kuziainisha.
Wanaisimu
wanaangalia
hali
ya
kufanana
na
kutofautiana
kimuundo
kwa
lugha
za
wanadamu
hata
kuzitofautisha.
7 Isimu Jamii
Taaluma
inayochunguza
athari
za
vipengele
vya
kijamii
jinsi
lugha
inavyotumika
katika
jamii.
Pia
wanaisimu
wanachunguza
jinsi
lugha
tofauti
zinavyoathiriana
wakati
wazungumzaji
wa
lugha
hizo
wanapokutana.
8 Isimu Kompyuta
Taaluma
inayohusika
na
utumiaji
wa
mbinu
za
kikompyuta
na
kimantiki
katika
kuchakata
lugha.
Tuangalie
kwa undani juu ya Fonetiki
Fonetiki
FONETIKI
Fonetiki
ni
taaluma
inayoshughulika
na
kuchunguza
sauti
za
lugha.
Inachunguza
sauti
hizo
zilivyo,
zinavyotolewa,
zinavyomfikia
msikilizaji,
nk.
Fonetiki
inachunguza
sauti
zote
ambazo
zinaweza
kutumika
katika
lugha
yoyote
ile
na
kutoa
sifa
za
sauti
hizo
bila
kujali
zinatumika
katika
lugha
gani
au
kwa
njia
gani.
Kwa
kusikiliza
sauti
hizo,
wanafonetiki
wanaweza
kuzipanga
sauti
hizo
katika
makundi
na
kuzipa
au
kuzitolea
sifa
ambazo
zinaweza
kutofautisha
sauti
moja
na
nyingine.
Matawi
ya
Fonetiki
Fonetiki
imegawanyika
katika
makundi
makuu
matatu
– Fonetiki matamshi, fonetiki safirishi na fonetiki masikizi.
a) Fonetiki matamshi (articulatory phonetics)
Huchunguza
jinsi
sauti
za
lugha
zinavyotolewa
na
viungo
vya
sauti
vya
mwanadamu
na
kuziweka
katika
matabaka.
Huangalia
viungo
vinavyohusika
katika
utoaji
wa
sauti
fulani,
pia
huchunguza
sifa
za
sauti
hizo
na
kuangalia
zinatofautianaje
na
zinafananaje.
b) Fonetiki safirishi au fonetiki akustiki (acustic phonetics)
Huchunguza
jinsi
sauti
za
lugha
zinavyosafiri
kutoka
kwa
msemaji
hadi
kumfikia
msikilizaji
husika
na
jinsi
mawimbi
ya
sauti
yanavyotengenezwa
na
jinsi
yanavyosafirishwa
hewani
hadi
kufikia
sikio
la
msikilizaji.
c) Fonetiki masikizi (auditory phonetics)
Huchunguza
lugha
zinavyopokelewa
na
msikilizaji
na
jinsi
zinavyotafsiriwa
na
sikio
na
akili
ya
msikilizaji,
hivyo
kuwezesha
kuwepo
masikilizano
kati
ya
msemaji
na
msikilizaji.
Fonetiki
Matamshi
Fonetiki
matamshi
inachunguza
mambo
yafuatayo:
i)
Ala
za
sauti
ii)
Mahali
pa
kutamkia
iii)
Namna
ya
utamkaji
iv)
Mikondo
ya
hewa
v)
Aina
za
vitamkwa
vi)
Sifa
bainifu
za
toni
vii)
Unukuzi
wa
toni
Ala
za
sauti
Ala
za
sauti
ni
viungo
vya
mwali
wa
binadamu
vinavyotumika
kumwezesha
mwanadamu
kutoa
sauti.
Pamoja
na
kutumika
kutolea
sauti,
viungo
hivi
pia
vina
kazi
nyingine
za
kibiolojia
k.m.
mapafu
hufanya
kazi
ya
kupeleka
hewa
kwenye
damu;
nyuzi
sauti
katika
koromeo
hufanya
kazi
ya
kufunga
koo
wakati
wa
kula
ili
kuzuia
chakula
kisipite
kwenye
mrija
hewa;
ulimi
na
meno
hutumika
kuonja
na
kula
chakula.
Ala za sauti
Ala
za
sauti
ni
viungo
vya
mwanadamu
vinavyotumika
katika
kutoa
sauti
mbalimbali.
Viungo
vifuatavyo
ni
ala
za
sauti
ambavyo
hushiriki
katika
utoaji
wa
sauti
1.
Midomo
2.
Meno
3.
Ufizi
4.
Kaakaa
gumu
5.
Kaakaa
laini
6.
Uvula
(kidaka
tonge)
7.
Pua
8.
Ncha
ya
ulimi
9.
Pembe
ya
ulimi
10.
Ulimi
sehemu
ya
mbele
11.
Ulimi
sehemu
ya
nyuma
12.
Shina
la
ulimi
13.
Koromeo
14.
Chemba
cha
pua
15.
Chemba
cha
kinywa
16.
Kongomeo
17.
Kimio
18.
Nyuzi
sauti
Ala
za
sauti
zinaweza
kugawanywa
katika
makundi
makubwa
mawili
ambayo
ni:
i)
Ala
sogezi
ii)
Ala
tuli
Ala
sogezi
ni
zile
ambazo
husogea
sogea
wakati
mtu
anapozungumza,
mfano
ulimi,
midomo,
nk.
Ala
tuli
ni
zile
ambazo
huwa
zimetulia
tu
hazisogeisogei
wakati
mtu
anapozungumza,
mfano
ufizi,
kaakaa,
meno,
nk.
Meno
ni
miongoni
mwa
ala
tuli.
Meno
hushiriki
katika
kutamka
baadhi
ya
foni
za
lugha,
mfano
mtu
anapotamka
[s]
na
[z]
hewa
huruhusiwa
kupenya
kati
ya
meno
na
kwa
hali
hiyo
meno
hushiriki
katika
kuzitamka
foni
hizo.
Midomo
ni
ala
sogezi
ambazo
mtu
anapozungumza
huwa
hazitulii
bali
husogeasogea.
Midomo
hushiriki
kiasi
cha
kutosha
katika
utamkaji
wa
vitamkwa
vya
lugha.
Vitamkwa
ambavyo
hutamkiwa
katika
midomo
ni
kama
vile
[m],
[p],
na
[b].
Ufizi
ni
kiungo
kinachoshiriki
kutamka
baadhi
ya
foni.
Ufizi
ni
ala
tuli,
hivyo
hausogeisogei
wakati
wa
kutamka
foni.
Baadhi
ya
foni
za
Kiswahili
zinazotamkwa
kwenye
ufizi
ni
pamoja
na
[n],
[t],
[d],
[z],
[l]
na
[r].
Foni
nyingi
za
Kiswahili
hutamkiwa
kwenye
ufizi
kuliko
mahali
pengine
popote.
Ufizi
unaoshiriki
zaidi
ni
ule
wa
juu.
Kaakaa
gumu hii
ni
sehemu
tuli
inayopakana
na
ufizi.
Hii
ni
sehemu
mojawapo
inayotumika
kutamka
foni
kama
vile
[ts],
[j].
Kaakaa
laini
hii ni sehemu
tuli
inayopakana
na
kaakaa
gumu.
Hutumiwa
kutamka
baadhi
ya
foni
kama
vile
[k],
[g],
ng'].
Koromeo
huu ni uwazi
unaoanzia
kwenye
kongomeo
(kisanduku
cha
sauti)
linapokomea
hadi
chemba
cha
pua
kinapoanzia.
Uwazi
huu
hupokea
sauti
inapotoka
kwenye
kisanduku
cha
sauti.
Ulimi
Mojawapo
ya
ala
sogezi
muhimu
sana
katika
mfumo
mzima
wa
uzungumzaji.
Ulimi
umegawanyika
katika
sehemu
kuu
tatu:
-
Sehemu
ya
mbele
(ncha
ya
ulimi)
-
Sehemu
ya
kati
(ubapa)
-
Sehemu
ya
nyuma
Sehemu
ya
mbele
(ncha
ya
ulimi)
hutumiwa
kutamka
vitamkwa
mbalimbali
kwa
mfano,
[n],
[t],
[d],
nk.
Sehemu
ya
kati
ya
ulimi
(bapa)
hutumika
kutamka
vitamkwa
kama
vile
[ts]
Sehemu
ya
nyuma
ya
ulimi
(mzizi
wa
ulimi)
huenda
juu
au
chini,
mbele
au
nyuma
wakati
wa
kutamka
vitamkwa.
Kusogea
huko
huathiri
umbo
la
chemba
cha
kinywa
na
hii
huathiri
sauti
zinazotamkwa.
Kidakatonge
huwa
hakitumiki
kutamka
vitamkwa,
lakini
huzuia
chakula
kisipitie
kwenye
njia
ya
hewa
hasa
wakati
mtu
anapokula
akiwa
anaongea.
Nyuzi
sauti
ni misuli
miwili
yenye
uwezo
wa
kunyumbulika
ambayo
huwepo
kwenye
kongomeo.
Misuli
hii
huumba
sura
mbalimbali
za
glota.
Wakati
mwingine
hufunga
kabisa
njia
na
kufungua
kwa
ghafla.
Wakati
mwingine
hukaa
kwa
namna
ambayo
sauti
itokayo
huwa
ghuna
au
sighuna.
Nyuzi
sauti
huibadilisha
hewa
inayotoka
mapafuni
kuwa
sauti
ya
kusikika.
Urefu
na
ukubwa
wa
nyuzi
sauti
huathiri
sauti
inayotolewa
– nyuzi
fupi
na
nyembamba
hutoa
sauti
ya
juu
(kali)
na
nyuzi
nene
na
ndefu
hutoa
sauti
nzito.
Kongomeo
(kisanduku
cha
sauti) hii
ni
sehemu
ambapo
nyuzi
sauti
huhifadhiwa.
Makongomeo
yanatofautiana
kati
ya
mtu
na
mtu.
Kuna
wengine
wana
makongomeo
makubwa
na
wengine
madogo.
Koo hili
ni
bomba
lenye
uwazi
ambapo
hewa
inayotoka
mapafuni
hupitia
kwenda
kwenye
mapafu
au
kurudi
kutoka
mapafuni.
Uwazi
huu
huanzia
mapafuni
hadi
kwenye
kongomeo.
Pua
Husaidia
kuchuja
sauti
inayotoka.
Watu
wenye
mafua
au
walioumia
pua
sauti
zao
huwa
hazichujwi.
Baadhi
ya
vitamkwa
kama
vile
nazali,
hutamkwa
kwa
kupitishia
mawimbi
mengi
zaidi
ya
sauti
kwenye
chemba
cha
pua
na
pua.
Chemba
cha
pua
ni
uwazi
ambao
upo
kuanzia
kwenye
pua
kuelekea
ndani
hadi
kwenye
koromeo.
Husaidia
kusafirisha
na
kuchuja
sauti.
Chemba
cha
kinywa
kuna
sehemu
nyingi
katika
chemba
cha
kinywa
ambazo
hutumika
kutamkia
sauti
mbalimbali.
Mahali
muhimu
pa
kutamkia
foni
za
konsonanti
ni
pamoja
na
ala
zifuatazo
za
sauti:
i)
Midomo
miwili
wa
juu
na
chini
– sauti
hutamkwa
kwa
kuikutanisha
midomo
yote
miwili
(wa
juu
na
wa
chini)
na
kupata
sauti
[b],
[m],
[p],
nk.
ii)
Mdomo
na
meno
– sauti
hutamkwa
wakati
mdomo
wa
chini
unapokuwa
umeyagusa
meno
ya
juu,
mfano
[f]
na
[v].
iii)
Meno
– Baadhi
ya
foni
hutamkiwa
kwenye
meno.
Vitamkwa
vya
kwenye
meno
huitwa
foni
za
meno.
Wakati
wa
kutamka
ulimi
huwekwa
katikati
ya
meno
ya
juu
na
chini
na
hususan
hugusa
meno
ya
juu,
mfano
[th]
iv)
Ufizi
– Wakati
wa
kutamka
foni
za
ufizi
ncha
ya
ulimi
hugusa
ufizi,
mfano
[t].
v)
Kaakaa
na
ufizi
– Wakati
wa
kuzitamka
foni
sehemu
ya
mbele
ya
ulimi
hugusa
sehemu
ya
kati
ya
ufizi
na
kaakaa
gumu,
mfano
[s].
vi)
Kaakaa
gumu
– Foni
nyingine
hutamkiwa
kwenye
kaakaa
gumu.
Wakati
wa
kutamka
foni
hizi
sehemu
ya
kati
ya
ulimi
huinuliwa
na
kugusa
kaakaa
gumu,
mfano
[ts]
na
[j].
vii) Kaakaa
laini
– Wakati
wa
kutamka
foni,
sehemu
ya
kati
au
nyuma
ya
ulimihuinuliwa
hadi
kukaribia
au
kugusa
sehemu
hiyo
ya
kaakaa
laini,
mfano
[k],
[g],
[kh].
viii)
Midomo
na
kaakaa
laini
– foni
chache
katika
lugha
hutamkiwa
katika
sehemu
mbili
tofauti
na
ambazo
hazipo
karibu
yaani
midomo
na
kaakaa
laini,
mfano
[w].
ix)
Koromeo
– Wakati
mwingine
baadhi
ya
foni
katika
lugha
hutamkiwa
kwenye
koromeo.
Wakati
wa
kuzitamka
foni
hizi
koromeo
hubanwa
kiasi
fulani
ili
kuruhusu
sauti
kutoka.
x)
Glota
– Uwazi
ulio
kati
ya
nyuzi
sauti
zilizopo
katika
kongomeo.
Uwazi
huu
hubadilikabadilika
kutegemea
kile
kinachotamkwa.
Sauti
za
glota
hutokea
wakati
nyuzi
sauti
zinapokutanishwa
kwa
muda
mfupi.
Sauti
hizi
ni
chache
katika
lugha,
mfano
[h].
UAINISHAJI
WA
SAUTI:
IRABU
NA
KONSONANTI
Sauti
za
lugha
zimegawanyika
katika
makundi
makubwa
mawili: konsonanti na irabu.
Tofauti
kati
ya
konsonanti
na
irabu
inaonekana
katika
utamkaji
wake.
Wakati
wa
kutamka
irabu
hewa
haizuiwi
au
kubanwa
mahali
popote,
yaani
hewa
hupita
kwa
urahisi
bila
kuzuiliwa.
Uainishaji
wa
irabu
Katika
uainishaji
wa
irabu
wanafonetiki
wameangalia
na
kubainisha
sifa
mbalimbali
.
Mojawapo
ya
sifa
zinazoangaliwa
ni
pamoja
na
mkao
wa
ulimi
katika
kinywa
wakati
wa
utamkaji,
mkao
wa
mdomo
wakati
wa
utamkaji
na mahali
pa
kutamkia
irabu.
Mahali
pa
kutamkia
irabu
– mahali
pa
kutamkia
irabu
ni
sifa
inayozingatia
mahali
ambapo
ulimi
huwapo
wakati
wa
kuzitamka
irabu
husika.
Wanafonetiki
wamebainisha
sehemu
tatu
za
kutamkia,
yaani
sehemu
ya
ulimi
inayohusika
wakati
wa
kutamka.
Sehemu
ya
ulimi
inayohusika
katika
utamkaji
ni
ile
ya
mbele,
kati
na
nyuma
ya
ulimi.
Kwa
mfano
katika
Kiswahili
irabu
[i]
na
[e]
hutamkwa
kwa
kutumia
sehemu
ya
mbele
ya
ulimi,
kwa
hali
hiyo
hizi
huitwa
irabu
za
mbele.
Irabu
[u]
na
[o]
hutamkwa
kwa
kutumia
sehemu
ya
nyuma
ya
ulimi
nazo
huitwa
irabu
za
nyuma.
Irabu
[a]
hutamkwa
kwa
kutumia
sehemu
ya
kati
ya
ulimi,
hivyo
huitwa
irabu
ya
kati.
Sifa
ya
mkao
au
mwinuko
wa
ulimi
inatumika
kuangalia
ulimi
unakuwa
chini,
umeinuka
juu
kiasi
au
juu
kabisa
wakati
wa
utamkaji
wa
irabu.
Kutokana
na
sifa
hii
ya
mwinuko
wa
ulimi,
irabu
zinaweza
kuainishwa
katika
makundi
matatu
ambapo
[i]
na
[u]
hutamkwa
wakati
ulimi
ukiwa
juu
na
[e]
na
[o]
hutamkwa
ulimi
ukiwa
katikati
na
[a]
hutamkwa
wakati
ulimi
ukiwa
chini.
Kutokana
na
sifa
hizo
zilizotajwa,
irabu
zinaweza
kuainishwa
kwa
kufuata
vigezo
vitatu:
- Kuangalia
mkao
wa
ulimi
kama
umeinuka
juu
au
upo
chini.
- Kuangalia
kuwa
sehemu
gani
ya
ulimi
imehusika
katika
kutamka
irabu.
- Kuangalia
midomo
ikoje
wakati
wa
utamkaji.
a) Kwa kutumia
kigezo
cha
mkao
wa
ulimi
kuwa
juu
au
chini
irabu
zinaweza
kuainishwa
kama
ifutavyo:
Irabu
juu
[i, u]
ulimi
unakuwa
umeinuka
juu.
Irabu
chini
[a] ulimi unakuwa chini.
Irabu
kati
[o, e]
ulimi
unakuwa
umeinuka
hadi
katikati.
b) Kwa kuangalia
kigezo
cha
sehemu
ya
ulimi
iliyoinuliwa
juu
au
kushushwa
chini
tunaweza
kuziainisha
irabu
kama
ifuatavyo:
Irabu
mbele
[i,
e]
ulimi
unakuwa
umeinuliwa
na
kupelekwa
mbele
Irabu
nyuma
[u,
o]
ulimi
unakuwa
umerudishwa
nyuma
Irabu
kati
[a]
ulimi
hauwi
nyuma
wa
mbele
bali
katikati.
Mkao
wa
midomo
– wakati
wa
kutamka
irabu
midomo
inaweza
kuwa
imeviringwa
au
haikuviringwa.
-
wakati
wa
utamkaji
wa
irabu,
midomo
inaweza
kuwa
imeviringwa
na
irabu
zitakazotamkwa
zitakuwa
viringo,
mfano
[o,
u].
-
midomo
inaweza
kuwa
imesambazwa
au
kupanuliwa
wakati
wa
utamkaji
na
kutoa
irabu
siviringo,
mfano
[i,
e,
o].
Kutokana
na
vigezo
tulivyoangalia
vya
uainishaji
wa
irabu
tunaweza
kupata
sifa
bainifu
za
kila
irabu
kama
ifuatavyo:
[i] irabu
juu
mbele
siviringo.
[u] irabu
juu
mbele
viringo
[e] irabu
kati
mbele
siviringo
[o] irabu
kati
nyuma
viringo
[a] irabu
chini
kati
siviringo
Uainishaji
wa
konsonanti
Konsonanti
ni
sauti
au
foni
ambazo
wakati
wa
kutamkwa
hewa
huzuiwa
kwa
namna
fulani.
Wakati
mwingine
hewa
huzuiwa
kabisa
na
wakati
mwingine
huzuiwa
kiasi
mahali
fulani
baada
ya
kupita
kongomeo.
Katika
kuainisha
konsonanti
zimeangaliwa
sifa
za
jumla
za
konsonanti
ambazo
ni
jinsi
konsonanti
hizo
zinavyotamkwa
na
mahali
konsonanti
hizo
zinapotamkiwa.
Namna
ya
utamkaji
Kwa kuzingatia
namna
konsonanti
zinavyotamkwa
konsonanti
zimegawanywa
katika
aina
kuu
sita
ambazo
ni:
- vizuiwa
au
vipasuo
- vikwamizwa
au
vikwamizi
- vizuiwa-kwamiza
- vitambaza
- vimadende
- nazali
Vizuiwa
au
vipasuo
Foni
hizi
zinapotamkwa
kwanza
hewa
kutoka
mapafuni
husukumwa
nje
kwa
nguvu
na
kuzuiwa
kabisa
kabla
ya
kuachiliwa
ghafla
na
kutoa
sauti
ambayo
hufanana
na
sauti
inayosikika
wakati
kitu
kinapolipuka.
Kutokana
na
hali
hiyo
ya
kutoa
sauti
ya
mpasuko
wanafonetiki
wengine
wameziita
konsonanti
hizi
vipasuo.
Katika
Kiswahili
kuna
vizuiwa
vifuatavyo:
[p],
[b],
[t],
[d],
[k]
na
[g].
Vikwamizwa
au
vikwamizi
Wakati
wa
kutamka
foni
hizi
ala
za
sauti
hukaribiana
kiasi
cha
kutosha
kuweza
kusikia
mkwaruzo
unaotokea
wakati
hewa
inapopita
kati
ya
ala
hizo.
Katika
Kiswahili
kuna
vikwamizwa
kadhaa
ambavyo
ni
kama
vifuatavyo:
[f],
[v],
[s],
[z],
[Ɵ],
[Ɣ],
[ʃ],
[h],
[x]
na
[dh]
Vizuiwa-kwamiza
Wakati
wa
kutamka
konsonanti
hizi
hewa
husukumwa
nje
kwa
nguvu,
huzuiwa
kisha
nafasi
ndogo
huachwa
ili
hewa
ipite
ikiwa
na
mkwaruzo.
Katika
Kiswahili
vizuiwa-kwamiza
ni
[ts]
na
[j].
Vitambaza
Wakati
wa
kutamka
vitambaza
hewa
husukumwa
nje,
huzuiwa
na
kuruhusiwa
ipite
pembeni
bila
mkwaruzo
mkubwa
sana.
Katika
Kiswahili
kitambaza
ni
kimoja
tu
ambacho
ni
[l].
Vimadende
Ni konsonanti
ambazo
wakati
wa
kutamka
ncha
ya
ulimi
huwa
inakuwa
imeugusa
ufizi
lakini
kutokana
na
nguvu
ya
hewa
inayopita
kati
ya
ncha
ya
ulimi
na
ufizi,
ncha
ya
ulimi
hupigapiga
kwa
harakaharaka
kwenye
ufizi.
Katika
Kiswahili
kipo
kimadende
kimoja
ambacho
ni
[r].
Nazali
Konsonanti
ambazo
hutamkwa
kwa
kukishusha
kimio
kwa
namna
ambayo
hewa
nyingi
kutoka
mapafuni
huelekezwa
kupitia
kwenye
chemba
cha
pua.
Katika
Kiswahili
kuna
nazali
zifuatazo:
[n],
[m],
[ng']
na
[ny].
Mahali
pa
Kutamkia
Sifa
hii
inahusu
ala
za
sauti
zinazohusika
katika
kuzuia
mkondohewa
katika
bomba
la
sauti.
Wakati
wa
kutamka
sauti
za
konsonanti,
alasogezi
husogea
kuelekea
kwenye
alatuli
au
wakati
mwingine
alasogezi
husogeleana
kama
vile
mdomo
wa
juu
na
wa
chini
inaposogeleana.
Aghalabu
mara
nyingi
sauti
huainishwa
kwa
kuzingatia
alatuli
iliyohusika
isipokuwa
kama
hakuna
alatuli
iliyohusika.
Kulingana
na
sifa
ya
mahali
pa
kutamkia
sauti
za
konsonanti
za
Kiswahili
zinaweza
kugawanywa
katika
makundi
nane
makuu
ambayo
ni:
- Sauti
za
midomo
- Sauti
za
mdomo
na
meno
- Sauti
za
meno
- Sauti
za
ufizi
- Sauti
za
kaakaa
gumu
- Sauti
za
kaakaa
laini
- Sauti
za
midomo
na
kaakaa
laini
- Sauti
za
glota
Sauti
za
midomo
Hizi
ni
sauti
ambazo
hutamkwa
kwa
kuikutanisha
midomo
yote
miwili,
yaani
mdomo
wa
juu
na
chini.
Midomo
yote
ni
alasogezi
ambazo
hukutana
kutamka
sauti
kama
vile
[p],
[b],
[m],
nk.
Sauti
za
mdomo
na
meno
Utamkaji
wa
sauti
kwa
kushirikisha
ala
hizi
za
sauti
hufanyika
kwa
kukutanisha
mdomo
wa
chini
na
meno
ya
juu.
Mdomo
wa
chini
ambao
ni
alasogezi
husogelea
meno
ya
juu
ambayo
ni
alatuli
na
kutamka
sauti
kama
vile
[f],
[v].
Sauti
za
meno
Sauti
zenye
sifa
hii
hutamkwa
huku
ncha
ya
ulimi
ikiwa
katikati
ya
meno
ya
juu
na
chini.
Vitamkwa
vinavyotamkiwa
kwenye
meno
hujulikana
kama
foni
za
meno.
Foni
za
meno
ni
pamoja
na
[ȶ],
[ɵ].
Sauti
za
ufizi
Ufizi
ni
mahali
ambapo
foni
za
lugha
hutamkiwa.
Ulimi
kama
alasogezi
huinuka
na
kugusa
sehemu
ya
ufizi.
Katika
lugha
ya
Kiswahili
ufizi
ndipo
mahali
ambapo
foni
nyingi
zaidi
hutamkiwa.
Foni
za
ufizi
ni
kama
vile,
[t],
[d],
[n],
[s],
[z],
[l],
[r].
Sauti
za
kaakaa
gumu
Kaakaa
gumu
ni
mahali
ambapo
baadhi
ya
foni
hutamkiwa.
Wakati
wa
kuzitamka
foni
hizi
sehemu
ya
kati
ya
ulimi
(bapa)
huinuliwa
hadi
kugusa
kaakaa
gumu.
Foni
zinazotamkiwa
mahali
hapa
ni
kama
vile
[ʦ],
[Ɉ].
Sauti
za
kaakaa
laini
Baadhi
ya
foni
hutamkiwa
katika
kaakaa
laini.
Wakati
wa
kuzitamka
foni
hizi
sehemu
ya
kati
au
nyuma
ya
ulimi
huinuliwa
hadi
kukaribia
au
kugusa
sehemu
ya
kaakaa
laini.
Foni
zinazotamkiwa
katika
kaakaa
laini
ni
kama
vile
[k],
[g],
[x]
na
[ɣ].
Sauti
za
midomo
na
kaakaa
laini
Foni
hizi
ni
chache
katika
lugha
ya
Kiswahili
ambazo
hutamkiwa
katika
sehemu
mbili
tofauti
ambazo
hazipo
karibu.
Mdomo
na
kaakaa
laini
ni
sehemu
zilizo
mbali
baina
yao.
Foni
zinazotamkiwa
katika
sehemu
hizo
ni
[w].
Sauti
za
glota
Glota
ni
sehemu
ambayo
hutumika
kutamkia
konsonanti
za
aina
mbalimbali.
Glota
ni
uwazi
ulio
kati
ya
nyuzi
sauti
zilizo
katika
kongomeo.
Uwazi
huu
huweza
kubadilika
kulingana
na
kile
kinachotamkwa.
Foni
za
glota
hutamkiwa
katika
glota
bila
kuvihusisha
viungo
vingine.
Katika
lugha
ya
Kiswahili
foni
ya
glota
ni
moja
ambayo
ni
[h].
Sifa
ya
Hali
ya
Glota
Sifa
hii
hutumika
kutofautisha
foni
ambazo
zinatamkwa
wakati
nyuzi
sauti
zikiwa
zinatetema
na
zile
ambazo
hutamkwa
huku
nyuzi
sauti
zikiwa
hazitetemi.
Foni
zile
ambazo
hutamkwa
nyuzi
sauti
zikiwa
zinatetema
huwa
ghuna
(yaani
hutoa
sauti
kubwa)
na
zile
ambazo
hutamkwa
nyuzisauti
zikiwa
hazitetemi
huwa
si
ghuna
(yaani
sauti
haiwi
kubwa).
Sauti
ghuna
ni
kama
vile
[z],
[b],
[d],
[g],
[v],
[ɣ]. Na
foni
ambazo
si
ghuna
ni
kama
vile
[s],
[p],
[t],
[f],
[k],
nk.
Namna
ya
kutamka |
Mahali
pa
kutamkia |
|||||||
|
|
Midomo |
Midomo-meno |
Ufizi
-
meno |
Ufizi |
Kaakaa
gumu |
Kaakaa
laini |
Koromeo
(glota) |
Vipasuo |
Ghuna |
b |
|
|
d |
|
g |
|
Si
ghuna |
p |
|
|
t |
|
k |
|
|
Vizuio
Kwamiza |
Ghuna |
|
|
|
|
Ɉ |
|
|
Si
ghuna |
|
|
|
|
ʦ |
|
|
|
Vikwamizi |
Ghuna |
|
v |
ȶ |
z |
|
ɣ |
h |
Si
ghuna |
|
f |
ɵ |
s |
|
|
|
|
Nazali |
|
m |
|
|
n |
ɲ |
ŋ |
|
Vitambaza |
|
|
|
|
l |
|
|
|
Vimadende |
|
|
|
|
r |
|
|
|
Viyeyusho |
|
w |
|
|
|
j |
|
|
Unukuzi
Unukuzi
ni
uwakilishaji
wa
sauti
ya
lugha
kwa
kutumia
alama.
Data ya aina moja inaweza kunukuliwa kwa njia zaidi ya moja. Kuna mifumo
mbalimbali ya unukuzi inayotumika kwa madhumuni ya aina mbalimbali. Madhumuni
hayo yanaweza kujumuisha ufafanuzi wa kifonetiki, nadharia ya Fonolojia,
ufundishaji wa lugha, leksikografia, nk.
Mnamo
mwaka 1886 kikundi cha waalimu wa Kifaransa na Kiingereza, wakiongozwa na
mwanaisimu Paul Passy, waliunda kilichojulikana baadaye kuanzia mwaka 1887 kama
Chama cha Kimataifa cha Fonetiki. Alfabeti yao ya kwanza ilitokana na
marekebisho ya tahajia kwa Kiingereza ilijulikana kama alfabeti ya Kirumi,
lakini ili iweze kutumika katika lugha nyingine, iliruhusiwa kubadili kutoka
lugha moja hadi nyingine. Hivyo, wanafonetiki
walibuni
alama
za
kifonetiki
za
aina
mbalimbali
zinazotumika
kuwakilisha
sauti
mbalimbali.
Alama
hizi
maalum
zinajulikana
kama
alfabeti
ya
kifonetiki
ya
kimataifa
(IPA).
Hii
ni
seti
ya
alama
za
alfabeti
zipatazo
karibu
mia
moja
pamoja
na
alama
nyingine
zisizo
za
alfabeti.
Ingawa
alama
hizi
nyingi
zinafanana
na
herufi
za
kawaida
za
tahajia
ya
kirumi,
lakini
kuna
baadhi
yao
zinatofautiana
na
herufi
hizo.
Orodha
ya
alama
hizo:
a – [a]
b – [b]
ch – [ʦ]
d – [d]
e – [ɛ]
dh - [ȶ]
f – [f]
g – [g]
gh – [ɣ]
h – [h]
i – [i]
j – [Ɉ]
k- [k]
kh – [x]
l – [l]
m – [m]
n – [n]
ng' [ŋ]
ny – [ɲ]
o – [ɔ]
p – [p]
r – [r]
s – [s]
sh – [ʃ]
t – [t]
th – [ɵ]
u – [u]
v – [v]
w – [w]
y – [j]
z – [z]
Sifa Bainifu za Sauti
Sifa bainifu ni sifa ambazo
hutumiwa kuzibainisha sauti mbalimbali za lugha. Kila sauti huweza
kupambanuliwa kwa kutumia sifa maalum za sauti fulani na jumla ya sifa hizo
ndizo ambazo huipambanua sauti hiyo na pia kuitofautisha na sauti nyingine.
Irabu zina sifa bainifu tofauti
na sifa bainifu za konsonanti.
Sifa bainifu za irabu
Irabu hubainishwa kwa kutumia
sifa kuu tatu ambazo ni:
- Mahali
pa kutamkia
- Mwinuko
wa ulimi
- Mkao
wa midomo
Mahali pa kutamkia
Sifa hii inaweza kutumiwa
kuzinainisha na kuzitofautisha irabu. Zipo sehemu tatu za kutamkia irabu ambazo
ni
-
Sehemu
ya mbele ya ulimi – sauti zinazotamkwa ni [i], [e]
-
Sehemu
ya kati ya ulimi – sauti inayotamkwa ni [a]
-
Sehemu
ya nyuma ya ulimi – sauti zinazotamkwa ni [0], [u]
Mwinuko wa ulimi
Sifa hii pia hutumika
kuzipambanua irabu kwa kuangalia mwinuko wa ulimi kama ulimi umeinuka au upo
chini. Kutokana na sifa hii ulimi unaweza kuwa umeinuliwa juu kabisa, nusu juu
au chini.
Mwinuko wa ulimi unapokuwa juu
sauti zinazotamkwa ni [i], [u]
Mwinuko wa ulimi unapokuwa kati
sauti zinazotamkwa ni [a]
Mkao wa midomo
Hii ni sifa mojawapo inayotumika
kuzipambanua irabu. Imeonekana kuwa wakati wa kuzitamka irabu midomo huwa
katika namna kuu mbili za mkao ambazo ni:
Mkao wa mviringo na mkao wa
mtandazo.
Inaonekana kuwa irabu zote
zinazotamkiwa mbele wakati wa utamkaji wake midomo huwa imetandazwa na irabu
zote za nyuma hutamkwa wakati midomo ikiwa mviringo.
Sifa Bainifu za Konsonanti
Konsonanti zinaweza kubainishwa
kwa kutumia sifa mbalimbali. Sifa hizo bainifu zinaweza kuwa kimatamshi,
kiakustika au kimasikizi. Wanaisimu mbalimbali wameeleza sifa mbalimbali
zinazopambanua konsonanti. Mfano Jacobson na Halle (1950) walizipambanua
konsonanti kwa kuonyesha sifa bainifu za kiakustika na walizigawa sifa hizo
katika makundi matatu ambayo ni:
-
Sifa
ya usonoranti
-
Sifa
ya uprotensi
-
Sifa
ya utoni
Sifa za usonoranti
Sauti zenye sifa ya usonoranti ni
zile ambazo utamkaji wake hewa hupita bila kizuizi au huzuiwa kidogo sana
kupitia chemba cha pua.
Sifa za usonoranti ni sifa
bainifu zinazotumika kutofautisha sauti kama vile:
-
Sauti
za irabu na zisizo irabu – katika ubainishaji wao irabu huonyeshwa kuwa na
usonoranti [+usonoranti] na konsonanti huonyeshwa kuwa haina usonoranti
[-usonoranti]. Pamoja na irabu kuwa na usonoranti pia zipo baadhi ya konsonanti
ambazo zina sifa ya ukonsonanti.
-
Sauti
za konsonanti na zisizo konsonanti – wakati wa kuzibainisha sauti za konsonanti
zitaonyeshwa kuwa na ukonsonanti [+ukonsonanti] na zile sauti zisizo za
konsonanti zitaonyeshwa kuwa hazina ukonsonanti [-ukonsonanti]
-
Sauti
zenye unazali na zisizo na unazali – Wakati wa kuzibainisha sauti za nazali
zitaonyeshwa kuwa na unazali [+unazali] na zisizo na unazali zitaonyeshwa
kutokuwa na unazali [-unazali]
-
Sauti
ghuna na sauti zisizo ghuna – katika kuzibainisha sauti hizi zile zilizo ghuna
zitaonyeshwa kuwa ghuna [+ghuna] na zile zisizokuwa ghuna zitaonyeshwa kuwa si
ghuna [-ghuna]
Sifa ya Uprotensi
Sifa ya uprotensi ilitumiwa
kutofautisha sauti ambazo zina mkazo zaidi na zile ambazo ni hafifu.
Sifa ya utoni
Ilitumiwa na wanaisimu
kuzitofautisha sauti ambazo ni
-
shadidi
na zile ambazo ni kali
-
kali
na ambazo si kali
Baadaye wanaisimu Morris Halle na
Noam Chomsky walizigawa upya sifa hizo katika makundi matano:
- Sifa
za makundi makuu
- Sifa
za chemba
- Namna
ya kutamka
- Sifa
za chasili
- Sifa
za kiarudhi
Sifa za makundi makuu
Zilitumiwa kuzitenganisha sauti
ambazo zinatofautiana mno. Hapa walitenganisha irabu na konsonanti na pia
walitenganisha aina mbalimbali za konsonanti.
Hapa zilitumiwa sifa za 1
usonoranti na 2 ukonsonanti.
Sifa za chemba
Sifa za chembe zilitumika kueleza
mkao wa chemba cha kinywa na pia mahali kitamkwa fulani kinapotamkiwa katika
chemba cha kinywa kama ni sehemu ya mbele, kati au nyuma ya kinywa. Hapa sifa
mbili ziliangaliwa 1. korona 2 anteria.
Sifa ya Korona
Sifa ya korona ilitumiwa
kuzipambanua zile sauti ambazo wakati wa kuzitamka bapa la ulimi huwa
limeinuliwa kutoka nafasi yake ya kawaida chini kuelekea juu kwenye kaakaa
gumu. Ulimi unaweza kuwa nusu chini au nusu juu alimradi haupo chini.
Sifa ya Anteria
Sifa ya anteria hutumiwa
kuzipambanua sauti zote zinazotamkiwa mbele ya kaakaa gumu, kwa ujumla
zinazotamkiwa sehemu ya mbele ya kinywa kwa kuzitofautisha na zile
zinazotamkiwa baada ya kaakaa gumu ambazo zinatamkiwa nyuma ya chemba chembe
cha kinywa. Sauti hizi hupewa sifa ya [+anteria] na zile za nyuma hupewa sifa
ya kutokuwa za mbele [-anteria].
Sifa za namna ya utamkaji
Sifa za namna ya utamkaji
zilitumika pia kupambanua sauti mbalimbali za lugha. Sifa hizi zilizotumika ni
pamoja na:
-
Sifa
za kuwa vifulizwa au la. Vifulizwa ni vitamkwa ambavyo hutamkwa kwa mwendeleo
mfano [l, r, f au s]. Sauti zote ambazo zilitamkwa kwa kuendelea zilipewa sifa
ya ya [+ kifulizwa] na zile ambazo hazitamkwi kwa kuendelea zilipewa sifa ya
kutokuwa vifulizwa [-kifulizwa]
-
Sifa
nyingine za namna ya kutamka zilizoangaliwa ni zile zinazotofautisha sauti kali
na zile hafifu. Sauti kali ni zile ambazo wakati wa utamkaji nyuzi sauti huwa
zimekaza na hafifu huwa nyuzi sauti zinakuwa zimelegea.
Sifa za chasili
Katika sifa ya chasili
ziliangaliwa sifa kuu mbili ambazo ya kwanza ni sifa ya ughuna na pili ni sifa
ya stridenti na melo
-
Sifa
ya ughuna imetumika
kuzibainisha sauti ambazo hutamkwa wakati nyuzi sauti zinapokuwa zinatetema.
Sauti ghuna hupewa sifa hiyo kwa kuwekewa alama ya [+ghuna] ambayo
huzitofautisha na sauti zile ambazo si ghuna kwa kuziwekea alama [-ghuna]
kuonyesha kuwa si ghuna. Sauti ambazo ni ghuna wakati wa kuzitamka nyuzi sauti
zinakuwa zinatetema na sauti si ghuna wakati wa kuzitamka nyuzi sauti huwa
hazitetemi.
-
Sifa
za Stridenti
imetumika kuzitofautisha zile sauti ambazo hutamkwa zikiwa na nguvumkazo za juu
na pia kuwa na kasimawimbi ya juu kiasi kuwa kasimawimbi ya chini huzidiwa.
Mfano ni kama vile f, v, th, dh, s, z. sh, zh, h.
-
Sifa
za Melo zimetumika kuzibainisha sauti
ambazo zimetulia zaidi na hazina nguvumkazo za juu sana na kasimawimbi ni ya
chini. Sauti zenye sifa ya melo huwekewa alama [+melo]
Sifa za kiarudhi
Sifa bainifu za kiarudhi ni zile
sifa ambazo huwekwa kwenye vipashio vikubwa kuliko sauti au foni. Sifa hizo
zinaweza kuwekwa kwenye silabi, neno, kirai au sentensi. Baadhi ya sifa za
kiarudhi zilizotumiwa ni pamoja na mkazo, kidatu, kiimbo na toni.
Mkazo ni sifa ya kiarudhi
inayohusu jinsi watu wanavyotamka maneno kwa nguvu zaidi katika sehemu fulani
fulani. Kwa kawaida lugha nyingi huwa na mikazo ya aina kuu mbili ambayo ni
mkazo katika sentensi na mkazo katika neno.
Mkazo katika sentensi huwekwa mahali fulani katika
sentensi kulingana na aina ya sentensi. Kwa mfano mkazo katika sentensi ya
maelezo ni tofauti na mkazo katika sentensi ya kuuliza.
Mkazo katika neno huwekwa katika silabi fulani
kwenye neno. Kila lugha huwa na utaratibu wake wa kuweka mikazo katika maneno
ya lugha hiyo. Lugha nyingine mahali pa mikazo katika neno hapabadiliki lakini
kuna lugha nyingine ambazo mahali pa mikazo hubadilika badilika. Mfano katika
Kiswahili mkazo huwekwa katika silabi ya pili kutoka mwisho.
Kidatu ni sifa ya kiarudhi ambayo
inahusu kasi ya mitetemo ya nyuzi sauti. Wanafonetiki hupima kidatu kwa
kuhesabu mizunguko ambayo nyuzi sauti huifanya katika nukta moja. Mizunguko
inahesabiwa kwa kuangalia idadi ya mitetemo ambayo hufanywa na nyuzi sauti kwa
nukta moja. Nyuzi sauti zitakapofanya mizunguko mingi zaidi basi sauti
itakayotoka huwa ya kidatu cha juu, yaani ni kali, lakini nyuzi sauti zikifanya
mizunguko michache katika nukta sauti inayotoka huwa ya kidatu cha chini kwa maana
inakuwa sauti ya chini. Kidatu kinaweza kuwa cha juu, cha kati au cha chini.
Hivyo kidatu kinahusiana moja kwa moja na kiwango cha sauti inayosikika. Mtu
akiwa anazungumza hubadilisha vidatu kutokana na hali aliyo nayo, mfano kama
akiwa na furaha, huzuni, hofu, hasira anaweza kubadilisha vidatu vyake ili
kuonyesha hali hiyo.
Toni ni kiwango cha kidatu pamoja na
mabadiliko yake ambayo hutokea wakati mtu anapotamka silabi au maneno. Katika
lugha za toni mabadiliko ya toni hubadili maana ya yale yanayosemwa. Katika
lugha hizo toni ni miongoni mwa sifa bainifu za lugha hizo. Kiswahili si lugha
ya toni hivyo toni si sifa bainifu katika lugha hii.
Kiimbo ni utaratibu wa upandaji na
ushukaji wa mawimbi ya sauti katika usemaji wa lugha. Kiimbo ni umbile zima la
uzungumzaji wa mtu au kundi la watu. Kiimbo kinahusisha mambo yote
yanayohusiana na uzungumzaji. Katika kiimbo kuna kidatu, mkazo, toni, uzuri wa
sauti na sifa nyingine zote za uzungumzaji. Kiimbo kinatusaidia kutambua lengo
la usemaji uliokusudiwa na mzungumzaji, tunaweza kutambua kama mzungumzaji
anatoa maelezo, anauliza swali au anatoa amri.
Kutokana na mabadiliko ya kiimbo
ambayo yanaonyesha lengo au maana anayokusudia mzungumzaji, tunaweza kupata
aina kuu nne za viimbo ambavyo ni kiimbo cha maelezo, kiimbo cha maulizo,
kiimbo cha amri na kiimbo cha mshangao.
Katika kiimbo cha maelezo
mawimbisauti ya usemaji wake kwa kawaida huwa yanakuwa yamelingana.
Katika kiimbo cha maulizo vidatu
huwa tofauti kutegemea aina ya swali linaloulizwa na kawaida mwishoni msemaji
hupandisha kidatu.
Katika kiimbo cha amri,
mzungumzaji hutumia kidatu cha juu zaidi kuliko ilivyo kwenye kiimbo cha
maelezo.
Mawimbisauti ya kiimbo cha
mshangao hutolewa huku yakiambatana na kupandisha, kushusha na kupandisha
kidatu katika silabi za mwishoni mwa neno.
Wakaa ni sifa ya kiarudhi ambayo
hujidhihirisha katika lugha nyingi. Wakaa ni ule muda ambao hutumika kutamka
sauti fulani. Mara nyingi sauti huwa na wakaa wa aina tatu: wakaa wa kawaida,
wakaa mfupi kuliko kawaida na wakaa mrefu kuliko kawaida. Katika baadhi ya
lugha wakaa huwa ni sifa bainifu, hivyo watumiaji huteua wakaa unaofaa.
FONOLOJIA
Fonolojia ni nini?
Fonolojia kama taaluma inayohusu
lugha ni tawi la Isimu linaloshughulikia uchambuzi wa mfumo wa sauti za lugha
fulani.
Fonolojia ni tawi la isimu ambalo
hujishughulisha na uchunguzi, uchambuzi na uainishaji wa sauti pambanuzi ambazo
hutumika katika mifumo mbalimbali ya sauti za lugha za binadamu (FOKISA).
Fonolojia hujishughulisha hasa na
zile sauti ambazo hutumika katika kutofautisha maana za maneno katika lugha
mahsusi.
Fonolojia hujihusisha na sheria
au kanuni zinazoandamana na utoaji na utumiaji wa sauti hizo pambanuzi.
Fonolojia hujishughulisha na
vipengele mbalimbali ambavyo vinahusiana na sauti na mpangilio wake wa uundaji
wa maneno katika lugha mbalimbali. Vipengele hivyo ni kama vile matamshi,
kiimbo, mkazo, lafudhi, toni, mfuatano wa sauti katika kuunda silabi, mfuatano
wa sauti katika kuunda mofimu, mfuatano wa mofimu katika kuunda maneno na
otografia.
Tofauti kati ya Fonetiki na
Fonolojia
Fonetiki na Fonolojia ni matawi
mawili ya isimu yaliyo jirani sana na wakati wote matawi haya hutegemeana na
kukamilishana.
Matawi yote mawili yanachunguza
kitu kimoja ambacho ni sauti za lugha.
Hata hivyo, ingawa taaluma hizi
huchunguza sauti za lugha, lakini Fonetiki huzichunguza sauti bila kuzingatia
mfumo ambamo sauti hizo hutumika, huchunguza sauti zote za lugha kwa ujumla,
lakini Fonolojia huzichunguza sauti zilizo katika mfumo mmoja yaani lugha
mahsusi. Kwa hali hiyo taaluma ya fonetiki ni moja tu, lakini Fonolojia ni
nyingi kama ilivyo idadi ya lugha duniani. Hivyo tuna fonolojia za lugha
mbalimbali kama vile fonolojia ya Kiswahili, fonolojia ya Kihehe, fonolojia ya
Kichaga, Fonolojia ya Kifaransa, nk. Ina maana kila lugha ina fonolojia yake
ambayo ni tofauti na fonolojia ya lugha nyingine.
Wanafonetiki wamekusanya sauti
nyingi kutoka katika lugha mbalimbali duniani na bado wanaendelea kukusanya.
Fonolojia ya lugha fulani hutumia sehemu ndogo tu ya sauti hizo zilizokusanywa.
Fonetiki ni sawa na seti kuu ambamo sauti za lugha mbalimbali duniani hutunzwa
na Fonolojia ya lugha ni sehemu ya seti hiyo.
Seti kuu (Fonetiki) ni seti isiyo
na kikomo, lakini Fonolojia zote zina kikomo. Inaaminika kuwa lugha nyingi
duniani hutumia wastani wa sauti kati ya ishirini na arobaini tu. Kiswahili
kina fonimu thelathini na moja tu.
Katika kiwango cha Fonetiki sauti
zote huorodheshwa na kutolewa ufafanuzi makini ambao huonyesha tofauti zote za
kifonolojia katika foni. Ufafanuzi wa kifonolojia huzionyesha zile sifa bainifu
ambazo ni bainifu katika lugha mahsusi inayoshughulikiwa, yaani sifa ambazo si
bainifu katika lugha fulani si lazima zitumike kuzifafanua fonimu za lugha
hiyo.
Kipashio cha ufafanuzi wa
kifonetiki ni foni, ambacho ni kipande kidogo kabisa cha sauti ambacho
hakihusishwi na lugha yoyote. Kipashio kidogo kabisa cha ufafanuzi wa
kifonolojia ni fonimu.
Uchambuzi wa kifonetiki
hauzingatii mfumo maalum wa lugha, lakini uchambuzi wa kifonolojia huzingatia
mfumo maalum wenye taratibu maalum na hauishii katika kuzichambua fonimu tu,
bali huchunguza mambo mengine pia kama vile mfuatano wa fonimu katika kuunda
silabi, neno, nk.
Katika sifa za kiarudhi, fonetiki
huzibainisha na kuzieleza sifa hizo kama zinavyotokea katika lugha mbalimbali.
Fonolojia hushughulikia zile sifa za kiarudhi ambazo ni bainifu katika lugha
inayoshughulikiwa na kuziacha zile ambazo si sifa bainifu katika lugha mahsusi
inayochunguzwa.
Fonetiki na Fonolojia hutegemeana
na kukamilishana. Uchambuzi wa kifonetiki husaidia uchambuzi wa kifonolojia na
uchambuzi wa kifonolojia husaidia uchambuzi wa kifonetiki.
Fonetiki ni msingi imara ambao
husaidia uchambuzi wa kifonolojia. Mtu asipokuwa na ujuzi wa Fonetiki atapata
shida kufanya uchambuzi wa kifonolojia, mfano kuziorodhesha sauti mbalimbali
anazosikia katika lugha fulani kwa kutumia alama maalum zinazowakilisha sauti
na kuzifafanua sauti hizo kwa kutumia sifa bainifu.
Fonetiki huzipata foni zote
kutoka lugha mbalimbali, yaani kutoka fonolojia za lugha mbalimbali, hivyo
inaaminika kuwa kama zisingekuwepo fonolojia za lugha mbalimbali, wanafonetiki
wasingekuwa na cha kuchunguza. Hivyo uchunguzi wa kifonolojia hutarajiwa kuwa
nyenzo ya uchambuzi wa kifonetiki ambao hutuwezesha kuelewa muundo wa lugha
inayochunguzwa.
Dhana ya fonimu
Fonimu zimeshughulikiwa na
wanaisimu mbalimbali na baada ya uchunguzi wa muda mrefu wamefikia kuifafanua
dhana ya fonimu kwa mitazamo mitatu:
-
Fonimu
ni tukio la kifonetiki
-
Fonimu
ni tukio la kisaikolojia
-
Fonimu
ni tukio la kifonolojia
Fonimu kama tukio la kifonetiki
Fonimu ni kundi la sauti katika
lugha fulani lenye sauti muhimu (fonimu yenyewe) pamoja na sauti zinazohusiana
nayo na ambazo hutumiwa mahali pake katika miktadha maalum (alofoni). Ina maana
kuwa fonimu zinaweza kutambuliwa na kutofautishwa na fonimu nyingine kwa
kuangalia sifa za kifonetiki za fonimu hizo.
Fonimu kama tukio la kisaikolojia
Mtazamo huu unaoangalia fonimu
kama tukio la kiasikolojia unaungwa mkono na wanaisimu wa Sarufi Zalishi.
Mwasisi wa Sarufi Zalishi alikuwa Noam Chomsky akidai kuwa lugha ina mambo
makuu mawili yaani umilisi na utendaji. Anadai kuwa mtu anapojifunza lugha
huanza na umilisi. Anaendelea kuwa umilisi ni ule ujuzi wa lugha walio nao
wazawa wa lugha fulani.
Mwanaisimu mwingine Boduin de
Courtney anadai kuwa fonimu ni tukio la akilini ambalo huwa na nia ya
mzungumzaji au jinsi anavyomwelewa mzungumzaji au vyote kwa pamoja. Ina maana
kuwa watumiaji wa lugha fulani huzijua fonimu zote za lugha yao.
Pia wanaeleza kuwa fonimu ni
dhana ya kisaikolojia kwa kuwa ni kipandesauti ambacho picha yake huwa akilini
mwa mtu ambaye hukusudia aitoe wakati anapoongea.
Watetezi wa mkabala huu wanadai
kuwa kila fonimu ina sifa zake katika lugha inamotumika na sifa hizi zote
hufahamiwa na watumiaji wa lugha husika – kisha huwekwa akilini mwao. Wakati wa
kuzungumza au kusikiliza mtu mwingine akiongea picha hiyo ya akilini ndiyo
ambayo humwongoza aseme kile anachosema na aelewe kinachosemwa na wengine. Hii
ndiyo sababu inayofanya fonimu ionekane kama tukio la kisaikolojia.
Fonimu kama tukio la kifonolojia
Mtazamo huu unawakilishwa na
kikundi cha wanaisimu wa Prague chini ya mwanaisimu maarufu kwa jina Trubetskoy
(1890-1938). Wanaisimu wa kundi hili walisisitiza mkabala wa kuangalia aumilifu
wa vijenzi mbalimbali vya lugha. Walidai kuwa fonimu ni kipashio cha
kifonolojia ambacho ni lazima kitazamwe ndani ya mfumo wa fonolojia
kinamotumika. Ili kuielewa fonimu ni lazima kuchunguza uamilifu wa fonimu hiyo
katika mfumo mzima wa fonolojia inamotumika.
Hapa mkazo unawekwa kwenye kazi
mbalimbali ambazo hufanywa na fonimu fulani katika lugha maalumu.
Mtazamo huu haukatai kuwa kuwa
kila fonimu ina sifa zake za kifonetiki, bali mtazamo huu unadai kuwa ingawa
fonimu zote zina sifa za kifonetiki lakini sifa hizo za kifonetiki sizo zinazoifanya
fonimu ya lugha fulani iwe fonimu, bali uamilifu wa fonimu ya lugha fulani
huifanya kuwa fonimu.
Pia wanadai kuwa ili fonimu iweze
kuwa fonimu katika lugha fulani lazima iwe bainifu kwa maana kwamba kama fonimu
hiyo ikiwekwa mahali ambapo palikuwa na fonimu nyingine, maana ya neno jipya
lazima ibadilike au ipotee. Mfano:
/p/ + /a/ +/k/ + /a/ - paka
/t/ + /a/ +/k/ + /a/ - taka
/s/ + /a/ +/k/ + /a/ - saka
/d/ + /a/ +/k/ + /a/ - daka
Kwa mifano hiyo tunaweza kusema
foni [p], [t], [s], [d] ni fonimu katika lugha ya Kiswahili kwa sababu ni
bainifu, yaani zinaweza kutofautisha maana katika maneno.
Trubetzkoy alitoa fasili ya
fonimu kuwa ni kipashio kidogo kabisa katika lugha chenye uamilifu wa
kutofautisha maana katika maneno.
Kila lugha ina namna yake ya
kuziweka fonimu pamoja ili kupata vipashio vikubwa zaidi, kama vile silabi,
maneno, nk. Kwa maneno mengine ni kuwa kila fonimu ina nafasi yake maalum
katika kushirikiana na fonimu nyingine katika lugha inamotumika. Mfano /i/
katika Kiswahili ina uamilifu tofauti na /i/ katika Kiingereza. Kwa hali hiyo
utaona wazi kuwa sauti za lugha mbalimbali huweza kufanana kifonetiki lakini
matumizi ya sauti hizo yanaweza kutofautiana baina ya lugha moja na nyingine.
Fonimu katika lugha tofauti zina
uamilifu tofauti haufanani na uamilifu wa fonimu ya lugha nyingine yenye sifa
zinazofanana kifonetiki. Sababu mojawapo ya lugha kutofautiana ni kutokana na
kuwa na fonimu tofauti na pia sababu nyingine ni kuwa uamilifu wa fonimu katika
lugha mbalimbali hutofautiana. Ili kuielewa vizuri fanimu inabidi kuangalia
uamilifu wa fonimu hiyo katika fonolojia ya lugha inamotumika fonimu hiyo
(ndiyo maana likaitwa tukio la kifonolojia).
Baada ya kuangalia mitazamo hiyo
mitatu tutaona kuwa yote inaeleza mambo yanayofaa na mazuri, tofauti zipo
katika mambo yanayotiliwa mkazo.
Mtazamo wa kwanza wa kifonetiki unasisitiza kuwa kila fonimu
lazima iwe na sifa zake za kifonetiki kwa kuwa fonimu ni sauti ambayo hutamkwa
ikasikika.
Mtazamo wa kisaikolojia unasisitiza umilisi na utendaji
kwa maana kwamba watumiaji wa lugha huzifahamu fonimu za lugha yao na ufahamu
huo ndiyo sehemu ya umilisi au ujuzi wa lugha. Ujuzi huu hukaa akilini mwao
ambao unajumuisha kujua sifa za
kifonetiki za fonimu na sifa za kifonolojia za fonimu zote na namna fonimu hizi zinavyotumika katika
lugha.
Mtazamo wa kifonolojia unaosisitiza uamilifu wa fonimu
unaeleza kuwa ili kuijua fonimu fulani lazima ujue matumizi yake. Na ili ujue
matumizi yake ni lazima ujue sifa za kifonetiki za fonimu hiyo.
Sifa za Fonimu
Fonimu zina sifa za jumla
zifuatazo:
- Kila
fonimu inazo sifa zake za kifonetiki zinazoweza kuelezwa ili kuifafanua
fonimu hiyo.
- Kila
fonimu inazo sifa zake za kifonolojia ambazo huonyesha uamilifu wa fonimu
hiyo katika lugha mahsusi.
- Watumiaji
wa lugha fulani huzielewa sifa zote za fonimu za lugha yao ikiwa ni sehemu
ya umilisi wao wa lugha hiyo.
- Kila
fonimu hushiriki kujenga na kutofautisha maana katika maneno.
- Fonimu
moja peke yake haina maana, yaani si kiashiria cha kiashiriwa chochote.
- Ukibadili
fonimu katika neno bila shaka maana ya neno hilo itabadilika.
- Ukiongeza
fonimu katika neno lolote maana ya neno hilo itabadilika au kupotea.
- Ukipunguza
fonimu katika neno lolote maana ya neno hilo itabadilika au kupotea.
- Ukipangua
mpangilio wa fonimu katika neno maana ya neno hilo itabadilika au kupotea.
- Kila
lugha ina fonimu zake na fonimu za lugha tofauti hazifanani katika
uamilifu wake.
Alofoni
Sauti mojawapo miongoni mwa sauti
kadhaa zinazoiwakilisha fonimu moja. Alofoni hutokea katika mazingira mahsusi
(Hartman 1972).
Alofoni ni sura au maumbo
mbalimbali ya fonimu moja yanayotokea katika mazingira tofauti. Fonimu za lugha
moja huweza kupata sura tofautitofauti kulingana na mazingira ambamo hutokea.
Ina maana kuwa fonimu inaweza kubadilika na kuchukua umbo moja kutokana na
kutokea kwake katika mazingira fulani na inaweza kubadilika na kuchukua umbo
jingine kutokana na kutokea kwake katika mazingira mengine tofauti. Mfano
katika Kiswahili tunaweza kupata alofoni za fonimu zifuatazo:
ki + ti ki + refu [kiti kirefu]
ki + ti ki + eusi [kiti cheusi]
fonimu /k/ inapofuatiwa na irabu kukawa na mpaka wa mofimu, kisha kufuatiwa na
irabu e hubadilika kuwa ch /tʃ/ kieusi – cheusi. Mfano wa maneno
mengine ni kama kioo kieupe – kioo cheupe.
U + limi m + refu [ulimi mrefu]
n + limi n + refu [ndimi ndefu]
fonimu /l/ inapotanguliwa na
nazali n hubadilika na kuwa d (n + limi = ndimi). Hii ina maana kuwa katika
mazingira haya sauti ch ni alofoni ya fonimu /k/ na d ni alofoni ya fonimu /l/.
Mbinu za kuzitambua Fonimu
Njia mbalimbali zinaweza kutumika
kuzibainisha fonimu za lugha. Njia hizo ni pamoja na:
-
Kufanana
kifonetiki
-
Jozi
za mlinganuo finyu
-
Mgawanyo
wa kiutoano
-
Mpishano
huru
Kufanana kifonetiki
Sauti zinazofanana kifonetiki ni
sauti zilizo na sifa bainifu zinazofanana. Sifa bainifu tumeshazijadili katika
vipindi vilivyotangulia. Tuliona kuwa irabu zina sifa bainifu zao na konsonanti
zina sifa bainifu zao. Kila lugha huteua baadhi ya sifa bainifu zinazotumika
kubainisha foni katika kiwango cha fonetiki na kuzitumia kuzifafanua fonimu za
lugha hiyo.
Sauti zinazoweza kufikiriwa kuwa
ni fonimu moja lazima zifanane sana kifonetiki. Mfano hatuwezi kufikiria kuwa
[i] na [a] ni fonimu moja kwa sababu zinatofautiana sana kifonetiki yaani sifa
bainifu zao ni tofauti sana. [i] +irabu, +mbele, +juu, -mviringo na [a] +irabu,
+mbele, +chini, -mviringo. Kwa kuangalia sifa za irabu hizi utaona kuwa hizi ni
irabu tofauti kwa kuwa hazifanani kwa sifa zote za kifonetiki, na kwa hali hiyo
haziwezi kuwa sauti za fonimu moja.
Hii ni mbinu mojawapo inayosaidia
kutambua sauti za fonimu moja ni kufanana kwao kifonetiki.
Jozi za mlinganuo finyu
Mlinganuo finyu ni tofauti ndogo
kabisa ya kifonolojia iliyopo baina ya maneno fulani. Maneno hayo mara nyingi
huwa na:
-
idadi
sawa ya fonimu,
-
fonimu
zinazofanana isipokuwa moja,
-
mpangilio
wa fonimu ulio sawa.
Mfano wa mlinganuo finyu ni kama
vile maneno /pita/ na /piga/ maneno haya yana tofauti ya mlinganuo finyu kwa
sababu:
-
Yana
idadi sawa ya fonimu (yote yana fonimu nne).
-
Fonimu
zilizopo zinafanana isipokuwa moja, yaani maneno yote yana fonimu /p/, /i/ na
/a/. tofauti ni katika fonimu /t/ na /g/.
-
Mpangilio
wa fonimu unafanana kwa kuwa /p/ na /i/ zinaanza na fonimu /t/ na /g/ zipo
kwenye nafasi ya tatu na hizi ndizo zinazotoautiana kisha mwishoni kuna /a/.
Baada ya kuona mlinganuo finyu
utaona unapatikana kwa kulinganua maneno mawili yenye tofauti ndogo. Hivyo jozi
ya mlinganuo finyu ni maneno mawili au orodha mbili za maneno ambayo tofauti
zao ni ndogo.
Kigezo hiki cha mlinganuo finyu
ni cha kiuamilifu kwasababu ingawa maneno hayo yana tofauti ndogo lakini baada
ya kuweka fonimu yenye sifa tofauti za kifonetiki neno linalopatikana lazima
liwe la lugha husika na pia neno linalipatikana liwe na maana tofauti na neno
la awali.
Mgawanyo wa kiutoano
Hii ni mbinu nyingine ya kutambua
fonimu. Mbinu hii hutumiwa kuonyesha uhusiano uliopo baina ya sauti mbili au
zaidi za fonimu moja ambazo haziwezi kutokea katika mazingira yanayofanana.
Sauti ina mazingira maalum ambayo hayawezi kukaliwa na sauti nyingine. Mbinu
hii inatuwezesha kutofautisha fonimu na alofoni. Tuangalie mfano ki + eusi = ch
+ eusi pale k ilipofuatiwa na i kwenye mpaka wa mofimu na kufuatiwa na e
ilibadilika kuwa ch.
Mpishano huru
Maneno mawili yanaweza kuwa na tofauti ya fonimu moja tu lakini ukiangalia
fonimu hizo zilizo tofauti utaona kuwa fonimu hizo kwanza zinatofautiana sana
kifonetiki na haziwezi kuwa alofoni za fonimu moja. Pili, utaona fonimu hizo
zinazotofautiana kifonetiki hazipo kwenye uhusiano wa kiutoano yaani zinaweza
kutumika katika mazingira yaleyale kwenye neno lakini ingawa fonimu hizi ni
tofauti hazisababishi tofauti za maana katika maneno zinamotokea.
Katika mpishano huru fonimu mbili
ambazo ni tofauti kabisa zinaweza kubadilishana, yaani kila moja inaweza
kutumiwa badala ya nyingine bila kubadili maana katika maneno hayo.
Hii ni kinyume na hoja ya msingi
ya fonimu inayosema kuwa ukibadili fonimu yoyote katika neno maana ya neno
itabadilika.
Tofauti kati ya mpishano huru na
mgawanyo wa kiutoano:
-
Mpishano
huru unahusisha fonimu mbili au zaidi zilizo tofauti kabisa, wakati mgawanyo wa
kiutoano huzihusisha alofoni mbili au zaidi za fonimu moja zinazofanana sana
kifonetiki; za aina moja na zinazotamkiwa sehemu moja.
-
Mpishano
huru unhusisha fonimu mbili zinazobadilishana nafasi moja katika neno, wakati
mgawanyo wa kiutoano unahusisha alofoni ambazo zimegawana mahali tofauti pa
kutokea. Kila moja ina muktadha wake maalum ambao alofoni nyingine haiwezi
kutokea.
-
Kufanana:
katika mpishano huru na mgawanyo wa kiutoano maana za maneno hazibadiliki.
Mifano ya mpishano huru:
angalau – angalao /u/ na /o/
wasia – wosia /a/ na /o/
badili – badala /i/ na /a/
amkia – amkua /i/ na /u/
baibui – buibui /a/ na /u/
Fonimu za Kiswahili
Fonimu za Kiswahili zinaweza
kugawanywa katika aina kuu tatu ambazo ni:
- Fonimu
za irabu
- Fonimu
za nusu irabu au viyeyusho
- Fonimu
za konsonanti
Sifa za bainifu za fonimu ni sawa
na sifa za foni zilizojadiliwa katika vipindi vilivyotangulia.
SILABI
Silabi ni kipashio cha
kifonolojia ambacho kwa ukubwa kipo kati ya fonimu na neno. Silabi ni ndefu
zaidi kuliko fonimu na fupi kuliko neno.
Kipashio cha kifonolojia
kinachohusu matamshi ambacho sauti za lugha hutamkwa mara moja kwa pamoja kama
fungu moja la sauti.
Kwa hali hiyo maneno ya lugha
hutamkwa kwa kufuata utaratibu wa silabi.
Ingawa maneno ya lugha hutamkwa
kwa kufuata utaratibu wa silabi, lakini kila lugha ina muundo wake wa silabi na
namna ya utamkaji wake. Fonimu zinapokaa pamoja hujenga silabi ambazo huweza
kutamkwa kama kitu kimoja.
Aina za silabi
Wanaisimu wamegundua kuwa zipo
aina mbili za silabi katika lugha:
-
Silabi
huru au wazi
-
Silabi
funge
Silabi huru au wazi
silabi huru ni silabi ambazo mara
nyingi huishia na irabu. Sauti za silabi huru huwa na msikiko au mvumo wa juu.
Kutokana na kuishia na irabu silabi huru huwa zinakuwa na msikiko mkubwa
zaidi.
Silabi funge
Ni silabi ambazo huishia na
konsonanti. Silabi funge kwa kawaida huwa na msikiko ambao ni hafifu. Kutokana
na kuishia na konsonanti msikiko wake huwa na mvumo hafifu.
Wanafonolojia walio wengi
wanaamini kuwa kwa kawaida silabi ina sehemu kuu tatu ambazo ni
-
mwanzo
wa silabi
-
kilele
cha silabi
-
mwisho
wa silabi
Sehemu ya mwanzo na mwisho wa
silabi ni sehemu ambazo husaidia kuweka mipaka ya kati ya silabi zinazofuatana
Sehemu ya mwanzo wa silabi
hujulikana kama kilele au kiini cha silabi huwa katikati ya silabi na husikika
kwa nguvu zaidi kuliko sehemu ya mwanzo na sehemu ya mwisho. Katika lugha
nyingi irabu hukaa kwenye kiini cha silabi.
Mara nyingi kila silabi inakuwa
na irabu kama kilele chake, iwe silabi huru au silabi funge.
Irabu ikiwa peke yake au miongoni
mwa sauti nyingine zinazounda silabi, irabu husikika kuwa kilele cha silabi.
Kuna baadhi ya lugha ambazo
hutumia baadhi ya konsonanti pekee kama silabi, mfano nazali [m] na [n] na
kitambaza [l]. Katika Kiswahili nazali [m] na [n] huweza kusimama peke yake
kama nazali, mfano /m-tu/, /m-ka-te/.
Miundo ya silabi za Kiswahili
Lugha ya Kiswahili inayo miundo
kadhaa ya silabi. Miundo hiyo ni kama hii ifuatayo:
- silabi
za irabu
- silabi
za konsonanti
- silabi
za konsonanti + irabu
- silabi
za konsonanti + konsonanti + irabu
- silabi
za konsonanti + nusu irabu +irabu
- silabi
za konsonanti + konsonanti + nusu irabu + irabu
- silabi
za konsonanti + konsonanti + konsonanti + irabu
- silabi
za konsonanti + irabu + konsonanti (silabi funge)
Silabi za irabu
Kiswahili kina irabu tano ambazo
kila moja huweza kuwa silabi katika miundo ya maneno mbalimbali mfano:
u + a = ua
o+ a = oa
a + u + au
pa + u + a = paua
te + u + a = teua
silabi za konsonanti
Lugha ya Kiswahili huziruhusu naadhi
ya konsonanti kuwa silabi katika maneno. Konsonanti zinazoweza kuwa silabi
katika Kiswahili ni nazali /m/ na /n/ tu. Konsonanti hizi huwa silabi katika
mazingira maalum na mara nyingi huwa zinakuwa katika nafasi ya mwanzoni au
katikati ya neno. Mifano ni maneno kama:
m+ pa + ka = mpaka
m + ga + nga = mganga
n + chi = nchi
n + ta = nta
na + m + na = namna
n + ne = nne
pa + m + pu = pampu
pa + n + cha = pancha
silabi za konsonanti + irabu
Muundo huu wa silabi wa
konsonanti + irabu ndio ulioshamiri zaidi si katika Kiswahili pekee, bali
katika lugha nyingi duniani. Katika muundo huu maneno huweza kuwa na silabi
moja, silabi mbili au zaidi.
Mfano:
pa
la
ka + ka = kaka
da + da = dada
sa + ma + ki = samaki
ta + pa + ta + pa = tapatapa
ta + ka + ta + ka = takataka
silabi za konsonanti + konsonanti
+ irabu
Katika Kiswahili konsonanti za
mwanzo katika muundo huu wa silabi huwa ni vitamkwa vya nazali /m/ na /n/.
Vitamkwa hivi huwa vinafungamana na konsonanti inayofuata ili kuunda muundo
huu. Mfano:
pe + nda = penda
u + nga = unga
nja + ma = njama
mba + li = mbali
mbe + ya = mbeya
Pamoja na muundo huu wa nazali
kutangulia, pia kuna baadhi ya silabi zenye kuanza na vitamkwa visivyo nazali.
Muundo huu pia unahusisha konsonanti zisizo nazali. Konsonanti zinazokabiliana
katika muundo huu wa silabi huwa hazikubaliani katika muundo wa lugha za
kibantu. Mfano:
la + bda = labda
da +fta +ri = daftari (mgulu
ameiita funge)
fa + ksi = faksi
se + kta = sekta
sto + o = stoo
silabi za konsonanti + nusu irabu
(kiyeyusho) +irabu
Kiswahili kina muundo mwingine wa
silabi za konsonanti + kiyeyusho + irabu. Muundo huu hushirikisha vitamkwa /w/
na /y/ na kawaida konsonanti huwa mwanzoni zikifuatiwa na kiyeyusho, mfano:
mwa + nga = mwanga
a + fya = afya
pwe + za = pweza
m + pya = mpya
kwa + ni = kwani
silabi za konsonanti + konsonanti
+ konsonanti + irabu
Muundo huu unatumika zaidi kwa
maneno ambayo yamekopwa kutoka lugha nyingine. Mfano:
skru + bu = skrubu
spri + ngi = springi
silabi za konsonanti + irabu +
konsonanti (silabi funge)
Kiswahili kinazo pia silabi
chache ambazo huishia na konsonanti, na zinajulikana kama silabi funge. Silabi
funge zinapatikana zaidi katika maneno yasiyo ya kibantu, au maneno ya mkopo.
Kumekuwa na utata mara nyingi kuhusu mahali pa kuweka mpaka wa silabi, yaani
konsonanti ya mwisho ikae wapi? Mfano:
lab + da = labda
al + ha + mi + si = alhamisi
il + ha + li = ilhali
tek + no + lo + ji + a =
teknolojia
MOFOLOJIA
Mofolojia ni nini?
Tawi la Isimu ambalo huchunguza
maneno na aina za maneno.
Tawi la Isimu linalochunguza
maumbo ya maneno na hususani maumbo ya mofimu.
Mofolojia huchunguza mofimu na
alomofu zake na jinsi ambavyo hukaa pamoja kuunda maneno mbalimbali katika
lugha zinamotumika.
Mfumo kamili wa mofimu katika
lugha fulani. Hapa mofolojia inahusika na uchunguzi wa mofimu za lugha moja,
yaani mofolojia ya lugha husika.
Mofolojia kama taaluma ya Isimu
inalo jukumu la kuchunguza maneno ili kuelewa maumbo yao.
Mofolojia kama kiwango kimojawapo
cha kila lugha, inatofautiana na viwango vingine vya lugha ambavyo ni
fonolojia, sintaksia na semantiki.
Mofimu, mofu na alomofu
Mofimu ni kipashio kidogo amilifu
katika maumbo ya maneno.
Mofimu ni kipashio kidogo kabisa
cha kisarufi kilicho na maana.
Mofimu ni kipashio kidogo kabisa
katika lugha chenye maana na zaidi ya hayo, maana hiyo hutofautiana na mofimu
nyingine katika lugha hiyo.
Kipashio kidogo kina maana umbo
la neno au umbo katika neno lisiloweza kugawanyika katika sehemu nyingine ndogo
zaidi. Udogo wa kipashio si udogo wa kiumbo bali ni kiwango ambacho mofimu hiyo
haiwezi kugawanywa zaidi na kulete maana. Hivyo mofimu inaweza kuwa kubwa
kiwango cha neno mfano maneno dawa, moshi, jiwe, nk. na mofimu inaweza kuwa na
kipashio kimoja kidogo kabisa kiumbo kama vile m katika umbo m-tu.
Kipashio kuwa amilifu maana yake
ni kwamba kina kazi maalum kisarufi. Kazi hizo ni kama ile ya kuwa kiini
kinachobeba maana ya msingi katika neno au kuwa kiambishi kinachowakilisha
dhana au kipashio cha kisarufi. Mfano umbo m-toto, kipashio m ni mofimu
inayofanya kazi kuonyesha umoja, na kubainisha kundi la nomino ambamo nomino
hiyo imo na kipashio toto ni mofimu inayobeba maana ya msingi.
Mofimu inazo sifa kadhaa
zinazoibainisha, na tatu kati ya hizo ni muhimu. Sifa hizo ni kama vile:
-
Mofimu
ni kipashio chenye umbo halisi
-
Mofimu
huwa na maana
-
Kila
mofimu huwa na nafasi yake ya kisintaksia katika kushirikiana na vipashio
vingine kuunda vipashio vikubwa zaidi.
Ubainishaji wa mofimu hufanyika
kwa kuzingatia kuwa neno linaweza kugawanyika katika vipande. Mfano,
mtu – m+tu
mto – m+to
kitabu – ki-tabu
Katika lugha pia yapo maneno
ambayo maumbo yake hayawezi kugawanyika katika vipande amilifu. Mfano katika
Kiswahili ni kama vile:
panga, kisu, suruali, tunda,
papai, godoro, nk.
Mofimu zinaweza kugawanyika
katika makundi mawili, kundi la kwanza ni zile mofimu ambazo zinatokana na
kugawanyika kwa umbo la neno na kuna mofimu ambazo ni sawa na neno kamili.
Mofu
Kipashio cha kimofolojia
kinachowakilisha mofimu.
Mofu ni umbo la neno ambalo
huwakilisha mofimu na ambalo hudhihirika kifonolojia na kitahajia. Mofimu
ambazo ni elementi dhahania huwakilishwa na mofu ambazo hudhihirika ama
kifonolojia kama sauti za kutamkwa au kitahajia zikiwa ni alama za kuandikwa.
Mfano /f/, /l/, /n/, /p/ au d, g, m, t.
Tunaweza kusema
Mofu ni maumbo halisi ya maneno
ambayo hutamkwa wakati watu wanapozungumza au kuandikwa wakati watu
wanapoandika maneno.
Mofu hudhihirika kifonolojia na
kitahajia – mofu mbalimbali hudhihirika kifonolojia zinapotamkwa na pia
kimaandishi zinapoandikwa.
Mofu huwakilisha maana – katika
neno lolote katika lugha yoyote kuna maana na maana hiyo imehifadhiwa katika
mofu zilizo katika neno hilo.
Mofu ni kipashio kidogo kabisa
cha neno chenye maana – mofu ni sehemu ndogo kabisa ambayo hubeba maana na
sehemu hiyo haiwezi kugawanywa katika sehemu ndogo zaidi zenye maana.
Kiumbo mofu huweza kulingana sawa
na fonimu na wakati mwingine huweza kulingana na neno zima. Mofu inaweza kuwa
kiambishi cha neno na pia mofu inaweza kuwa mzizi wa neno, mfano: m-toto,
m-ti, mbwa, baba, samaki, nk.
Alomofu
Umbo mojawapo kati ya maumbo
kadhaa tofauti yanayowakilisha mofimu moja.
Ni viwakilishi viwili au zaidi
vya mofimu moja lakini ambavyo hujitokeza katika mazingira tofauti ya mtoano.
Mfano katika Kiingereza kiambishi tamati /s/ cha wingi kina alomofu zifuatazo:
/s/ katika maneno cats, books,
cakes, nk.
/z/ katika maneno dogs, bags,
tables
/iz/ katika maneno classes,
boxes, boys
Katika Kiswahili mofimu kiambishi
m, mw, mu hujitokeza, mfano:
m-tu
m-ti
m-toto
mw-ana
mw-angaza
mu-uguzi
m hujitokeza kabla ya mashina ya
maneno yanayoanza na konsonanti wakati mw hujitokeza kabla ya mashina
yanayoanza na baadhi ya irabu na mu hutokea kabla ya mashina yanayoanza
na irabu u. Hivyo m, mu, mw ni alomofu za mofimu mu katika
mazingira tofauti.
Hivyo mofimu inapokuwa na umbo
moja tu, umbo hilo linaitwa mofu na wakati mofimu moja inapokuwa na maumbo
zaidi ya moja yanayoiwakilisha mofimu hiyo, maumbo hayo yataitwa alomofu za
mofimu hiyo. Tunaweza kusema kuwa alomofu ni mofu mojawapo miongoni mwa mofu za
mofimu moja.
Aina za mofimu
Mofimu zinaweza kugawanyika
katika aina mbili – mofimu funge na mofimu huru.
Mofimu funge ni vipande vya
maneno ambavyo haviwezi kusimama kila kimoja peke yake kisarufi. Mofimu funge
ikiondolewa kwenye muktadha wake hukosa maana na ni vigumu kujua maana yake
bila kuiweka katika muktadha wake.
Mofimu funge zinaweza kutokea
kama mizizi ya maneno mfano:
kat-
imb-
pot-
Pia mofimu funge inaweza kutokea
kama kiambishi, mfano:
m-
ki-
-ish-
-ik
Mofimu huru ni maumbo yanayoweza
kusimama peka yake kimaumbo, kileksika na kisarufi.
Ni mofimu ambazo zinaweza
kusimama peke yao kama maneno kamili, mfano ni kama:
baba, mama, samweli, kuku, jani,
safi, nk.
Mofimu ni kipashio dhahania cha
umbo fulani ambacho kinaweza kuwakilishwa na mofu tofautitofauti katika mazingira
anuwai.
Mofolojia kama taaluma inaweza
kugawanywa katika matawi makuu mawili ambayo ni:
-
Mofolojia
ya minyambuliko ya maneno
-
Mofolojia
ya uundaji wa maneno
Mofolojia ya minyambuliko ya
maneno hushughulikia zaidi minyambuliko ya maneno ambayo huwekwa kwenye mizizi
ya maneno kuwakilisha maana mbalimbali lakini minyambuliko hiyo haibadili aina
ya neno hilo. Mfano katika Kiswahili mzizi wa neno -toto unaweza kuwekewa
viambishi m-, ka-, wa- kupata maneno m-toto, ka-toto, wa-toto, nk. Hapa utaona
aina ya neno haikubadilika baada ya kunyambulishwa.
Mofolojia ya uundaji wa maneno
hushughulikia uundaji wa maneno kwa kuweka viambishi kwenye mizizi ya maneno na
kiambishi nyambuaji huweza kubadili aina ya neno. Wakati viambishi mbalimbali vinapopachikwa
kwenye mzizi wa neno, huwa linapatikana neno jipya na neno jipya linalopatikana
si lazima liwe la aina moja na neno la awali na pia si lazima liwe la aina
tofauti na neno la awali. Mfano katika Kiswahili: mzizi wa neno piga ni pig-
tunaweza kuweka viambishi na kupata maneno kama ifuatavyo
pig-o
ma-pig-ano
m-pig-aji
Tofauti iliyopo kati ya mofolojia
ya minyambuliko na mofolojia ya uundaji wa maneno ni kuwa katika mofolojia ya
minyambuliko ya maneno hakuna maneno mapya yanayoundwa, lakini katika mofolojia
ya uundaji wa maneno ni kuwa maneno mapya huweza kuundwa tofauti na maneno ya
awali.
Maneno katika lugha mbalimbali
yanaweza kugawanywa katika aina kuu mbili, ambazo ni:
-
maneno
yasiyoambishwa au yasiyoweza kuwekewa viambishi
-
maneno
yanayoambishwa au yanayoweza kuwekewa viambishi
Maneno yasiyoambishwa na
yanayoambishwa huweza kutokea kwa viwango tofauti katika lugha mbalimbali.
Baadhi ya lugha huwa na maneno yasiyoambishwa mengi zaidi kuliko yale
yanayoambishwa, na lugha nyingine huwa na maneno mengi zaidi yasiyoambishwa
kuliko yale yanayoambishwa.
Maneno yasiyoambishwa ni maneno
yale ambayo hayawekewi viambishi vyovyote wakati wote yanapotumika, na mara
nyingi maneno haya huwa ni mizizi. Mfano majina ya watu, Juma, Ali, Samweli;
majina ya miji kama vile Moshi, Kibaha, Kisarawe; majina ya nchi kama vile
Tanzania, Uganda, Kenya, nk.
Maneno yanayoambishwa ni yale
maneno ambayo mizizi yao inaweza kuwekewa viambishi mbalimbali vinavyobeba
maana mbalimbali. Katika Kiswahili yapo maneno mengi yanayoweza kuambishwa. Tunaweza
kuweka viambishi kabla ya mzizi wa neno au baada ya mzizi wa neno. Mfano
ki-tabu, vi-tabu, m-tu, pig-a
CCCCCCCCCCCCCCCCCCCCCCCCCCCCCCCCCCCCCCCCCCCCCCCCC
Mizizi, Viambishi na Mashina
Mzizi ni nini?
Mzizi ni umbo msingi la neno
ambalo haliwezi kuchanganuliwa zaidi tena katika sehemu nyingine ndogo bila
kupoteza uamilifu wake na utambulisho wake wa kisemantiki.
Mzizi ni mofimu katika neno
ambayo huwakilisha taarifa ya kileksika.
Mzizi sehemu ya neno baada ya
kuondoa viambishi vyote.
Aina za mizizi
Lugha nyingi duniani zina aina
mbili za mizizi ambayo ni:
mizizi funge na mizizi huru.
Mzizi funge
Mzizi funge ni mzizi ambao
hauwezi kujitegemea wenyewe, yaani hauwezi kusimama peke yake kama neno.
Mfano:
paka – pak + a
pakia – pak + i + a
mpaka – m + pak + a
mpako – m + pak + o
upakaji – u + pak + a + ji
Hapa umbo la msingi ni pak
na utaona kuwa halibadiliki wakati wote bali linaongezewa viambishi, huu ndio
mzizi wa neno. Utaona kuwa mzizi kama umbo la msingi huwa halibadilikibadiliki.
Katika lugha yoyote maneno
yanayohusiana kimaana, huwa yanakuwa na umbo moja la msingi au mzizi ambalo
linalojitokeza mara kwa mara.
Mzizi ambao ni umbo la msingi
lina kawaida ya kutobadilikabadilika katika maneno yote yanayohusiana nalo,
lakini maumbo mengine yote yanayobakia katika kila neno huweza
kubadilikabadilika. Kubadilika kwa maumbo hayo mengine mara nyingi huongezea
maana za ziada zinazohusiana na maana ya msingi inayobebwa na mzizi.
Mzizi huru
Mzizi huru ni mzizi ambao unaweza
kusimama peke yake kama neno kamili. Umbo la mzizi huu haliwezi kuchanganuliwa
katika sehemu ndogo zaidi bila kuathiri maana yake ya msingi. Mfano:
panga, godoro, bega, redio,
jengo, gereza, mbwa, chui, ng'ombe, nk.
maneno hayo yote utaona kuwa
yanajitegemea kimaana. Maneno hayo hayawezi kuchanganuliwa zaidi katika vipande
vidogo zaidi bila kupoteza maana ya msingi.
Viambishi
Viambishi ni mofimu
zinazoambatishwa kwenye mzizi wa neno ili kuwakilisha hali au dhana mbalimbali
zinazofungamana na neno pamoja na mofimu hizo.
Viambishi ni mofu ambazo
huongezwa kwenye mizizi ya maneno mbalimbali na viambishi hivyo huwakilisha
maana fulani.
Viambishi mara nyingi huwa na
maana za kisarufi zaidi na havina maana za kileksika.
Kulingana na nafasi katika neno
viambishi vipo vya aina tatu:
-
viambishiawali
-
viambishindani
au viambishikati
-
viambishitamati
Kulingana na majina yao,
viambishi vinaweza kuwekwa mwanzoni, katikati au mwishoni mwa neno. Katika
lugha nyingi viambishi huwekwa mwanzoni na mwishoni mwa mzizi, Kiswahili ikiwa
moja ya lugha hizo.
Viambishiawali ni aina ya viambishi ambavyo
huwekwa kabla ya mzizi wa neno. Viambishi hivi hutamkwa kabla ya mzizi wa neno
wakati wa mazungumzo. Mfano m-toto; wa-toto; m-paka; ma-daftari
Viambishindani au viambishikati ni aina ya viambishi ambavyo
huwekwa katikati ya mzizi wa neno. Mfano wa viambishi hivi tunaweza kuipata
katika lugha nyingine, kama vile Kihaya, mfano neno a-bon-a (amepata) –
a-b-o-i-n-e (alipata). Lugha ya Kiswahili haina viambishi vya aina hii.
Viambishitamati ni viambishi ambavyo huwekwa
baada ya mzizi wa neno. Mifano:
kat-a; sak-a; saf-ish-a;
pig-a-n-i-a; njoo-ni; imb-i-a
Kwa kawaida viambishi vyote ni
maumbo tegemezi ambavyo hufanya kazi mbalimbali za kisarufi. Viambishi huwa
havina maana vinapokuwa peke yao.
Lugha ya Kiswahili inatumia viambishi
vya aina mbili tu ambavyo ni viambishiawali na viambishitamati.
Shina
Shina ni sehemu ya neno yenye
mzizi na viambishi ambapo hakuna neno jipya linaloundwa bali huleta mabadiliko
ya kisarufi katika neno hilihilo moja. Ni sehemu ya neno ambayo ikiambishwa
haisababishi kuundwa kwa neno jipya, mfano: piga; piga-ni-a; piga-n-ik-a;
a-li-piga.
Neno la msingi linabaki kuwa
lilelile na maana ya msingi pia inabaki kuwa ileile.
Piga ni shina ambalo kutokana
nalo tunapata hayo maumbo mengine bila kubadili maana ya msingi.
Mifano mingine ni baadhi ya
mashina ya nomino ambayo pia huweza kuwekewa viambishi na kusiwe na neno jipya
lililoundwa, mfano:
godoro; ma-godoro; ki-ji-godoro;
gari; ki-gari; kongamano; ma-kongamano
Kuna maneno ambayo hayawezi kuwa
mashina kwa sababu yakiwekewa viambishi huunda maneno mapya, mfano:
taifa – utaifa, taifisha,
utaifishaji
shamba – ushamba, mshamba,
kishamba
Tofauti nyingine kati ya mzizi na
shina ni kuwa mzizi huundwa na mofimu moja tu wakati shina linaweza kuundwa na
mofimu moja, ambayo ni mzizi, mfano mbegu, sahani, jembe; pia shina linaweza
kuundwa na mzizi na kiambishi, mfano pig-a, kat-a; na vilevile shina linaweza
kuundwa na mofimu mbili ambazo zote ni mizizi, mfano bata-mzinga,
nguruwe-mwitu.
Ingawa mzizi unaweza kuwa shina,
lakini si kila shina linaweza kuwa mzizi.
Viambishi
Viambishi ni mofimu
zinazoambatishwa kwenye mzizi wa neno ili kuwakilisha hali au dhana mbalimbali
zinazofungamana na neno pamoja na mofimu hizo.
Viambishi vya lugha ya Kiswahili
huweza kupachikwa mwanzoni au mwishoni mwa mzizi tu.
Upachikaji wa kiambishi kwenye
mzizi au shina la neno hujulikana kama uambishaji, mfano, k-isu, safi-sh-a,
tend-a, imb-ik-a, m-toto
Viambishi vinaweza kuainishwa kwa
namna mbili tofauti.
-
Vinaweza
kuanishwa kwa kuzingatia na nafasi vinamotokea katika neno.
-
Vinaweza
kuinishwa kwa kuzingatia uamilifu wao.
Uainishaji
kwa kuzingatia nafasi vinamotokea
Uainishaji
huu unaangalia mahali viambishi hivyo vinapopachikwa katika mzizi wa neno.
Uainishaji
kutokana na nafasi vinamotokea
Katika
lugha ya Kiswahili viambishi vinaweza kupachikwa mwanzoni na mwishoni mwa mzizi
wa neno.
Viambishi
vinavyojitokeza mwanzoni vinajulikana kama viambishi awali, mfano, m-zee,
ma-chungwa, m-som-i, a-pat-e, nk
Viambishi
vinavyojitokeza mwishoni mwa mzizi wa neno vinajulikana kama viambishi tamati,
mfano, chek-a, kimbi-a, tembe-a, safi-sh-a.
Uainishaji
wa Kiuamilifu
Uainishaji
huu unazingatia kazi za kisarufi zinazofanywa na viambishi hivyo. Katika
Kiswahili viambishi vina maumbo mbalimbali na kila kimoja kina kazi ya
kisarufi.
Kazi
hizi hutegemea mahali kiambishi kilipo katika umbo la neno na vilevile aina ya
neno kinamojitokeza.
Baadhi
ya kazi za viambishi ni kama vile upatanishi wa kisarufi, unyambulishi,
uwakilishi wa njeo, uwakilishi wa hali na ukanushi.
Viambishi
katika nomino
Viambishi
katika nomino hufanya kazi ya kuwakilisha ngeli, idadi na upatanishi wa
kisarufi.
Ngeli
na idadi
Viambishi
vinavyoonyesha idadi na ngeli katika nomino aghalabu hutokea mwanzoni kabla ya
mzizi wa neno. Viambishi vya aina hii vinafanya kazi za aina mbili, ya kwanza
ni kuwa vinawakilisha idadi (umoja na wingi) na pili vinawakilisha ngeli za
nomino, yaani makundi ya nomino. Mfano ni kama ifuatayo:
m
+ tu – wa + tu
ki
+ tu – vi + tu
ji
+ cho – ma + cho
n+guo
– n + guo
m
+ ti - mi + ti
Upatanishi
wa kisarufi
Viambishi
vya nomino vinahusiana na vingine vinavyojitokeza katika sehemu za mwanzo
katika aina nyingine za maneno katika sentensi.
Viambishi
hivyo hufanya kazi ya upatanishi wa kisarufi.
Upatanishi
wa kisarufi ni kukubaliana kwa viambishi vya nomino na vile vya kitenzi au
kivumishi, mfano,
ki-su
ki-moja ki-me-pote-a
wa-toto
wa-wili wa-mefik-a
ma-we
ma-wili ya-me-baki
Viambishi
vya unyambulishi
Viambishi
nyambulishi katika Kiswahili huambikwa kwenye mizizi ya nomino ili kuunda
maneno mapya. Viambishi hivi hufanya kazi pamoja na viambishi vya ngeli na
idadi kuunda nomino mbalimbali mfano:
-
kiambishi
nyambulishi -e mwishoni mwa umbo la jina huonyeshwa kitendwa, yaani kile
ambacho tendo hukifikia, km. tum-a – tum-e, ham-a ham-e
-
kiambishi
nyambulishi -o huonyesha kitumizi au kitendo, matokeo ya tendo au mahali tendo
linapotukia, mfano, pig-a pig-o; siki-a siki-o;
zib-a ki-zib-o; som-a ki-som-o
-
kiambishi
nyambulishi -ji huonyesha hali ya mazoea au ya kurudiwarudiwa
kwa
tendo, mfano sem-a m-sem-a-ji; ku-nywa ki-nywa-ji
-
viambishi
nyambulishi -vu na -fu hunyesha umbile au sifa inayostahiki kwa kile
kinachohusika na tendo, mfano, oko-a w-oko-vu; chaka-a u-chaka-vu; pungu-a
u-pungu-fu
-
kiambishi
nyambulishi -a huonyesha maana maalum kuhusika na tendo, mfano, wi-a; m-wi-a;
wi-w-a m-wi-w-a
-
kiambishi
nyambulishi -i kinaonyesha weledi wa mtu, mfano som-a m-som-i; pik-a mpish-i;
-
kiambishi
nyambulishi -zi huonyesha matokeo ya moja kwa moja ya tendo, mfano, poke-a
ma-poke-zi; tum-i-a ma-tumi-zi; poke-a ma-poke-zi.
Maumbo
yenye kiambishi tamati -o yanakuwa na viambishi awali ki-, vi, u na m hubeba
dhana ya kitumizi mfano, ki-zib-o, ki-funik-o, u-fung-u-o, m-teg-o.
Maumbo
hayo huwa na dhana ya matokeo yanapokuwa yametanguliwa na viambishi awali m-,
mi-, ji-, ma-, w-, au n-, mfano, m-sem-o, nen-o, pig-o, ny-imb-o, m-chez-o,
w-it-o. Nomino zinazoundwa kutokana na viambishi hivi mara nyingi hutokana na
vitenzi, yaani yanatokana na mizizi ya vitenzi.
Kiambishi
tamati -ni ni kiambishi ambacho si nyambulishi kinachotokea kwenye maumbo ya
nomino za Kiswahili. Kiambishi hiki kinaweza kuambikwa kwenye nomino zote
isipokuwa nomino mahsusi zinazohusu majina ya watu mfano, Ali, Yakobo, Yusufu;
majina ya mahali, mfano, Bagamoyo, Tanzania, Kilwa; wakati, mfano, Jumamosi,
Machi. Kiambishi hiki kikiambikwa kwenye nomino hubeba dhana ya mahali au ndani
yake, mfano, chumba-ni, mji-ni, kanisa-ni, shule-ni, nk.
Viambishi
katika vitenzi
Vitenzi
katika Kiswahili hubeba viambishi vingi kuliko vipengele vingine vya kisarufi.
Viambishi
vya unyambulishi katika vitenzi
Unyambulishaji
– ni upachikaji wa viambishi kwenye mzizi ili kuunda maneno mapya. Katika
Kiswahili kuna viambishi nyambulishi ambavyo hutumika katika uundaji wa vitenzi
vipya, mfano,
tembe-a
tembe-le-a
tembe-le-a-n-a
tembe-l-e-wa
tembe-l-e-k-a
Katika
Kiswahili kuna viambishi tamati nyambulishi vinane ambavyo huambikwa kwenye
mizizi ya vitenzi kama vifuatavyo:
1.
-w-
2.
-ik-/-ek-
3.
-ish-/-iz-/-esh-/-ez-
4.
-il-/-el-
5.
-o-/-u-
6.
-am-
7.
-an-
8.
-at-
Viambishi
vya nafsi
Viambishi
vya nafsi huambatana na vitenzi. Viambishi hivi ni pamoja na ni-, u-, a-, tu-,
m-, wa-, -ku-, -wa-, -tu-, nk, mfano ni-na-kuja, u-ta-pit-a, ni-me-wa-on-a, nk.
Viambishi
vinavyotangulia mwanzoni kabisa mwa neno vinawakilisha nafsi katika nafasi ya
kiima (mtenda)
Viambishi
vinavyokabiliana na mizizi ya kitenzi ni viambishi vya nafsi katika nafasi ya
yambwa (yaani ile inayopokea tendo).
Kiambishi tamati -ni kinapoambikwa mwishoni mwa
vitenzi vya Kiswahili hubeba dhana ya idadi hasa nafsi ya pili wingi, mfano,
ka-e-ni, kimbi-e-ni, njoo-ni, siki-e-ni.
Viambishi
vya njeo
Viambishi
vya njeo ni viambishi vinavyowakilisha dhana ya wakati. Kuna vinavyowakilisha
wakati uliopita, ambavyo ni viambishi, -li-, -me-, mfano ni kama a-li-kuja,
a-me-kuja. Kiambishi -li- huwakilisha wakati uliopita (kukubali) na kiambishi
-me- wakati uliopita hali timilifu
Kiambishi
-na-, mfano ni-na-kuja, a-na-enda kinawakilisha wakati uliopo (kukubali)
Kiambishi
-ta- kinawakilisha wakati ujao (kukubali), mfano wa-ta-rudi, ni-ta-lima
Kiambishi
-ku- kinawakilisha wakati uliopita (kukanusha), mfano, ha-ku-ja, si-ku-wa-ona.
Kiambishi
-ja- kinawakilisha wakati uliopita hali timilifu (kukanusha), mfano,
ha-ja-rudi, si-ja-fika, ha-tu-ja-mw-ona
Kiambishi
awali hu- kinawakilisha hali ya mazoea (kukubali), mfano hu-enda, hu-tembea,
hu-la, nk.
Viambishi
vya hali
Viambishi
vya hali ni vile vinavyoonyesha dhamira ya maelezo. Viambishi mbalimbali
vinawakilisha dhana mbalimbali kama ifuatavyo:
Kiambishi
-a ni kiambishi cha dhamira dhahiri, mfano kat-a, som-a, pak-a.
Kiambishi
-e ni kiambishi cha dhamira ya matilaba, yaani kuonyesha nia ya kutenda jambo,
mfano a-sem-e, a-kimbi-e, a-tembe-e.
Kiambishi
-po- ni kiambishi (cha sharti) cha kuonyesha mahala au muda, mfano,
ali-po-kuja, ali-po-fika.
Kiambishi
-ki- ni kiambishi cha sharti, mfano a-ki-rudi, wa-ki-fika, tu-ki-ja
Kiambishi
-ki- ni kiambishi cha tendo kuendelea, mfano alikuwa a-ki-tembea, tulikuwa
tu-ki-imba
Kiambishi
-li- ni kiambishi cha hali ya kuwa na, mfano a-li-ye na jembe.
Viambishi
-nge-/-ngali-/-ngeli- ni viambishi vya kudadisi tendo, mfano, wa-nge-kuona,
tu-nge-tembea
Viambishi
virejeshi
Viambishi
virejeshi ni viambishi vinavyowakilisha kitajwa katika umbo la vitenzi.
Viambishi hivi mara nyingi huungana na na kiambishi -li- kuunda aina nyingine
ya viambishi amilifu katika Kiswahili, mifano ni kama vile:
wa+o
mfano, wa-li-o-kimbia
u+o
mfano, u-li-o-dondoka
li+o
mfano, li-li-lo-pasuka
ch+o
mfano, ki-li-cho-katika
i+o
mfano, i-li-yo-anguka
vy+o
mfano, vi-li-vyo-letwa
zi+o
mfano, zi-na-zo-tofautiana
Viambishi
virejeshi vinapojitokeza katika maumbo ya vitenzi huwa vinarejelea kitajwa,
yaani nomino inayohusika na tendo.
Uundaji wa maneno
Kila lugha ina kanuni zake za
uundaji wa maneno. Katika lugha ya Kiswahili taratibu za aina mbili hutumika
katika uundaji wa maneno. Taratibu hizi zinajulikana kama uambishaji na
unyambulishaji.
Uambishaji
Uambishaji ni utaratibu wa kuweka
kiambishi kabla, katikati au baada ya mzizi wa neno.
Katika Kiswahili viambishi huweza
kujitokeza mwanzoni na mwishoni tu mwa mzizi, mfano:
m-toto; m-ti; pig-a; fuat-a;
pat-a, simam-ia
Mifano hiyo inaonyesha kuwa
viambishi vya Kiswahili vinaweza kutokea mwanzoni au mwishoni mwa mzizi.
Inawezekana kuwepo mpangilio wa
viambishi viliwili kutokea kabla ya mzizi, mfano, a-na-som-a, tu-ta-temb-ea.
Hivyo, uambishaji ni utaratibu wa
kuweka pamoja viambishi na mizizi katika maumbo mbalimbali ya neno. Hivyo,
uambishaji katika lugha ni uwekaji pamoja wa viambishi na mzizi kwa namna
mbalimbali bila kujali aina ya maumbo yanayopatikana.
Unyambulishaji
Unyambulishaji ni utaratibu wa
kuweka pamoja viambishi na mizizi au mashina ili kuunda maneno. Utaratibu huu
unaruhusu viambishi nyambulishi (undaji) kuwekwa pamoja na mizizi au mashina ya
maneno. Mifano ni kama vile maneno, umb-a umb-o; pig-a pig-o; safi saf-isha;
fupi fupi-sha; pika-mpishi-mpikaji, mapishi.
Matokeo ya unyambulishaji ni
kupatikana kwa maneno mengine. Katika mifano hiyo inaonekana kuwa umbo lenye
viambishi huweza kiuwa na kambishi kimoja au zaidi. Mizizi inayobeba viambishi
nyambulishi mara nyingi huwa ni mizizi funge.
Muundo wa nomino
Nomino ni nini?
Neno linalotaja kitu, kiumbe,
hali, dhana au tendo lolote.
Lugha mbalimbali huainisha nomino
kwa njia tofauti. Kiswahili huziainisha na kuzipanga nomino katika makundi
mbalimbali yanayojulikana kama ngeli.
Ngeli ni nini?
Utaratibu wa taaluma ya sarufi ya
lugha katika kupanga aina za nomino katika makundi. Utaratibu huu husaidia
kuzigawa nomino katika makundi mbalimbali kwa kuzingatia uwiano uliopo baina ya
nomino hizo na vipengele vingine vya kisarufi katika lugha.
Ngeli hutambuliwa kwa kuangalia
viambishi vya mwanzo vya nomino na upatanishi wake wa kisarufi. Uainishaji wa
nomino kwa kuzingatia viambishi awali hujulikana kama uainishaji wa
kimofolojia.
Mfano msomi kiambishi awali ni m-
na mzizi som- na kiambishi tamati -i ambacho hutumika kuundia nomino kutokana
na kitenzi.
Kiambishi awali kinajulikana kama
kiambishi ngeli
Ngeli za Kiswahili zimeainishwa
katika makundi mbalimbali kwa kuangalia hali ya umoja na wingi wa nomino hizo.
Kila kiambishi ngeli kimepewa
namba ya kukitambulisha. Kwa kutumia kigezo cha kimofolojia, nomino za
Kiswahili zimegawanyika katika ngeli kumi na nane kama ifuatavyo:
Ngeli 1 mu-
Ngeli hii huchukua nomino zenye
kiambishi ngeli mu-, pamoja na mw-, m- mfano muuguzi, mwalimu, mtoto. Kiambishi
hiki hupata tofauti zinazosababishwa na mabadiliko ya kifonolojia. Mabadiliko
hayo hutegemea muundo wa shina la nomino husika. Hii huweza kuathiri /u/ iliyo
katika kiambishi ngeli mu- inapokuwa imekaribiana na fonimu ya kwanza ya shina.
U hugeuka kuwa w inapokaribiana
na vokali isiyo u. Hali hii husababisha mofimu ngeli mu- kuwa na alomofu tatu ambazo ni mu-, mw-
na m-.
Ngeli 2 wa-
Hii huwalikisha wingi wa ngeli ya
kwanza. wa- ni kiambishi ngeli cha ngeli hii, mfano wa-toto, wauguzi, nk.
Kiambishi ngeli cha ngeli hii ya pili pia hupata mabadiliko ya kifonolojia
ambapo wa- huwa na alomofu w-, mfano wa-limu.
Ngeli 3 mu-
Nomino katika ngeli hii huchukua
kiambishi mu-, mfano muundo. Hata hivyo mofimu hii huwa na alomofu mu-, mw- m-.
mu- huwa mw- iwapo mzizi wa neno utaanza na vokali isiyo u, mfano mw-embe.
mu- huwa m- iwapo mzizi wa neno
utaanza na konsonanti, mfano m-ti.
Ngeli 4 mi-
Ngeli hii ni ya wingi wa nomino
za ngeli ya tatu mofu ngeli yake ni mi-, mfano mi-ti, mi-embe. Mofu hii huwa
haina alomofu.
Ngeli 5 ji-/ø
Nomino katika ngeli hii huchukua
kiambishi ji-, mfano ji-we, ji-tu, nk. Hata hivyo kuna nomino nyingine ambazo
huingizwa katika kundi hili la ngeli kwa kuzingatia upatanisho wao wa kisarufi
ingawa hazina kiambishi ngeli ji-. Mfano goti.
Ngeli 6 ma-
Ngeli hii huwakilisha wingi wa
ngeli ya tano. Mofu ngeli ya ngeli hii ni ma-, mfano ma-cho, ma-goti, ma-we.
Ngeli 7 ki-
Nomino katika ngeli hii huchukua
kiambishi awali ki-. Mfano ki-tu, ki-atu, kikombe.
Ngeli 8 vi-
Nomino za ngeli hii huchukua
kiambishi ngeli vi-. Hii huwakilisha wingi wa ngeli ya saba. Mfano vi-ti,
vi-atu.
Ngeli 9 n/ø
Hakuna kiambishi ngeli maalum
kinachowakilisha ngeli hii. Nomino za ngeli hii huendelezwa sawa katika umoja na
wingi wake katika ngeli ya kumi. Mfano nyumba, kalamu, nyama, meza.
Ngeli 10 n/ø
Ngeli hii huwakilisha wingi wa ngeli ya tisa.
Kiambishi ngeli cha ngeli hii ni sawa na kile cha ngeli ya tisa. Tofauti kati
ya ngeli ya tisa na kumi hudhihirika katika upatanisho wa kisarufi. Mfano
nyumba inaungua – nyumba zinaungua.
Ngeli 11 u-
Nomino zinazoingia katika ngeli
hii huwa na kiambishi ngeli u-, mfano u-limi, u-bao, u-jia.
Ngeli 12 ka-
Nomino za ngeli hii huwa na
kiambishi ngeli ka-. Mfano ka-toto, ka-gari.
Ngeli 13 tu-
Ngeli hii inawakilisha wingi wa
ngeli ya 12. Kiambishi cha ngeli hii ni tu-. Mfano tu-toto, tu-gari.
Ngeli 14 u-
Nomino za ngeli hii huchukua
kiambishi ngeli u-, mfano u-tukufu, u-gonjwa, u-chungu, u-zuri.
Ngeli 15 ku-
Nomino za ngeli hii huchukua
kiambishi ngeli ku-. Nomino za ngeli hii huundwa kutokana na vitenzi. Hizi ni
nomino zinazoelezea vitendo. Mfano ku-piga, ku-tembea.
Ngeli 16 pa-
Nomino za ngeli hii hurejelea
hali mbalimbali za mahali. Kiambishi ngeli ni pa-. Ngeli hii huonyesha mahali
mahsusi. Mfano pa-le, ha-pa.
Ngeli 17 ku-
Nomino za ngeli hii huonyesha
mahali kwa jumla. Mfano ku-le, hu-ku.
Ngeli 18 mu
Nomino za ngeli hii huonyesha
undani wa mahali. Mfano hu-mu.
Kanuni za uundaji wa maneno
Maneno ambayo uundaji wake kwa kiasi
kikubwa hutegemea miunganiko ya viambishi na mizizi ni nomino na vitenzi.
Unyambulishaji unaofanyika kwa
kupachika viambishi kabla ya mzizi unahusu zaidi nomino.
Unyambulishaji unaofanyika kwa
kupachika viambishi baada ya mzizi unahusu vitenzi.
Kanuni za uundaji wa nomino
Nomino za Kiswahili zina
viambishi mbalimbali mfano:
m-/wa-
m-/mi-
ji-/ma-
ki-/vi-
Uundaji wa nomino kutokana na
mizizi ya aina nyingine za maneno unajulikana kama unominishaji.