FASIHI
HUCHOTA MAUDHUI YAKE KUTOKA KATIKA HALI HALISI ZA JAMII. JADILI KAULI HII KWA
KUREJELEA HADITHI TEULE.
Maudhui katika kazi ya
fasihi ni jumla ya mawazo yote yanayozungumzwa pamoja na mtazamo wa mwandishi
juu ya mawazo hayo. Maudhui hujumuisha mawazo pamoja na mafunzo mbalimbali
yaliyomsukuma msanii hadi akatunga na kusanii kazi fulani ya kifasihi.
Vipengele vya maudhui ni pamoja na dhamira, migogoro, falsafa ujumbe na
msimamo.
Mwandishi
wa kazi ya fasihi huwa na jukumu kubwa la kuichuja, kuiongoza, kuielekeza au
kuikashifu jamii bila kusahau kuisifu mahali pafaavyo. Ikumbukwe kuwa mwandishi
yuyu huyu wa kazi ya fasihi huwa kioo cha jamii kiasi kwamba kupitia kwake
tunaweza kufahamu hali halisi inayoikumba jamii husika. Hii ni kwa sababu yale yote
ambayo mwandishi huyaandika, msingi wake huwa ni jamii ambapo yupo au
ameshuhudia swala husika likitendeka.
Maudhui
haya huwa ni picha halisi ya matukio au matendo katika jamii inayomhusu
mwandishi hivyo basi huitumia kazi yake kama kielelezo au kipiga-debe huhusu
hali husika. Katika kazi hii tutazama katika tamthilia ya Mstahiki Meya
iliyoandikwa na Timothy Eregi. Yafuatayo ni maudhui ambayo yamebainika wazi
katika tamthilia ya Mstahiki Meya na ambayo yanadhihirika wazi kati jamii zetu
ni yafuatayo:
(i)
Uongozi mbaya
(ii)
Umaskini
(iii)
Ukoloni mamboleo
(iv)
Ufisadi
(v)
Ufeministi/Nafasi ya mwanamke.
v
Uongozi mbaya.
Uongozi
mbaya ni hali ambapo aghalabu kiongozi anatumia mamlaka yake visivyo kwa
kujinufaisha na kunufaisha vibaraka wake badala ya kuwatumikia raia wan chi au eneo
husika kwa kuendeleza sera potovu na hata kutozingatia sheria za nchi. Viongozi
wanaotekeleza sera za kiutawala zinazokandamiza au kurudisha nyuma maendeleo ya
watawaliwa huwa ni viongozi wabaya. Maudhui mengi katika tamthilia hii
yamejitokeza kutokana na maudhui makuu ya uongozi mbaya. Maudhui ya uongozi
mbaya yamejitokeza katika tamthilia hii ya Mstahiki Meya pakubwa.
·
Uongozi wa Baraza la Cheneo unaoongozwa na
Meya Sosi ni mbaya kwa kuwa unapalilia ufisadi. Meya Sosi anatumia mamlaka yake
kunyakua ardhi ya umma, kuwaongeza mshahara wafuasi wake kiholela. Kuwapa
marupurupu na kuwaajiri watu kazi bila kuzingatia ufaafu wao bali kwa
kuzingatia mapendeleo ya kifisadi.
·
Usugu
wa viongozi wa Cheneo hasa Meya Sosi kuvunja sheria bila kuhofia adhabu yoyote
ni dhihirisho la uongozi mbaya. Licha ya kuwa Meya Sosi amefilisi barasa la
Cheneo, anamzungumzia Daktari Siki kwa ujeuri na kusuma kuwa raia wangemchagua
hata mara nne akitaka kwa kuwa tayari walikuwa wamemchagua mara mbili.
·
Uongozi mbaya pia unaonekana katika baraza la
Cheneo pale tunaona ule ukatili na unyama unaotendewa raia hao. Wanayimwa haki
yao ya kugoma wakipigania nyongeza ya mishahara na kutuma polisi wawatawanye na
hata kuwaua.
·
Utawala wa Cheneo chini ya Meya unavunja
kanuni za Baraza hasa pale anapokataa kuzizingatia na badala yake kusikiza Bili
na ushauri wake kuhusu utoaji wa kandarasi za Baraza. - Ukosefu wa sera mwafaka
na utaratibu wa kutatua matatizo
·
ukosefu wa dawa ni dhihirisho kuwa hakuna
mikakati madhubuti ya kuhakikisha hali kama hizi zinashughulikiwa. - Mishahara
ya wafanyakazi wa Baraza kucheleweshwa na vilevile kulipwa nusunusu (uk. 23).
·
Licha ya kuwa baadhi ya madiwani wanasema
uchumi wan chi umeimarika lakini haumnufaishi mwananchi wa kawaida (uk. 23).
Uongozi
wa mabavu au wa ki imla (Autocratic Leadership) unaweza kuwa mfano mzuri wa
uongozi mbaya. Uongozi wa aina hii kiongozi hujiona kwamba ni yeye tu ndiye
ajuaye kila kitu. Hasikilizi wala haombi mawazo au mawaidha kutoka kwa walio
chini yake. Maamuzi yote huyafanya yeye. Yeye ni mtu wa kutoa amri na maelekezo
tu. Hajali mawazo na fikira za mwenzake.Inaaminika kuwa huenda mwandishi wa
tamthilia hii kwa njia moja au nyingine ameaathiriwa na utawala wa aina huu
ambao unampamsukumo wa kutaka kupiga vita uozo huu wa uongozi katika jamii
zetu.
Swala
uongozi mbaya limeyakumba mataifa mbalimbali ulimwenguni. Uongozi hu mbaya
umekuwa chanzo cha matukio yanayodamamiza maendeleo katika mataifa husika. Bara
la Afrika limekumbwa pakubwa na swala hili la uongozi mbaya. Kiongozi wa
upinzani nchini Kenya Mh.Raila Odinga. Akiongea
na Sauti ya Amerika (Mei 26, 2009) muda mfupi kabla ya kutoa hotuba yake katika
chuo kikuu cha Buffalo, New York, Odinga alisema kuwa mfumo mbaya wa uongozi
umewanyima Waafrika haki ya kupanga namna ya kujiletea maendeleo yao wenyewe.
Mh.Odinga alisema kuwa Afrika inahitaji
mabadiliko yatakayosaidia kupunguza mamlaka kupita kiasi yaliyowekwa katika
taasisi za urais. Alisema hili litasaidia kuondokana na mifumo ya kidikteta, na
kuingia mfumo wa uongozi wa kidemokrasia utakao wapatia mamlaka
wananchi.Isitoshe ,viongozi wa nchi za Afrika wakiwa kwenye makongamano yao
mbalimbali ya uongozi wanakiri kwa
vinywa wazi kuwa , uongozi mbaya wa watawala wa bara hili ndio unaoitishwa
Afrika mgogoro wa wakimbizi.Haya yalitokea wazi wakiwa mjini Kampala, Uganda na
kuongeza kuwa, utawala mbaya, uongozi usiofaa na dhaifu ndiyo sababu kuu ya
kuvamiwa nchi hizo na wimbi kubwa la wakimbizi kutoka maeneo mengine.
Rais
Yoweri Museveni wa Uganda alisikika akinadi hivyo kwenye "kikao cha mshikamano" na
kuongeza kuwa, taasubu za kikabila na kukosekana wapinzani wa kuaminika ni
katika mambo yanayozusha mapigano ya umwagaji wa damu katika baadhi ya nchi za
Kiafrika ambayo yanawalazimisha wakazi wa nchi hizo kuyakimbia makazi
yao. Ukitoa Uturuki na Pakistan, Uganda ni nchi ya tatu yenye wakimbizi
wengine duniani na ni ya kwanza barani Afrika. Hivi sasa kuna wakimbizi karibu
milioni moja wa Sudan Kusini pekee nchini Uganda.
Uongozi
mbaya huathiri uchumi swala ambalo linajitokeza katika mataifa mengi ya bara la
Afrika. Mengi ya mataifa ya bara hili yamedidimia kiuchumi kwa kutokuwa na
uongozi ufaao. Mfano mzuri ni kuporomoka kwa uchumi wa Uganda wakati wa utawala
mbaya wa Iddi Amin Dada. Uongozi wake duni ulipelekea shilingi ya taifa la
Uganda kukosa thamani ambapo kufufuka kwayo ni muhali sana. Waaidha uongozi mbaya katika jamii zetu huwa
kizuizi kikubwa sana kwa utangamano kiasi kwamba kundi moja hujiona kuwa bora
zaidi kwa kufyonza mirija ya uchumi na mali huku kundi jingine likijiona kuwa
bure kabisa. Hili pia huwa kikwazo na uwiano katika jamii teule huwa mtihani
mgumu sana.
Waaidha uongozi kama huu
huwagandamiza waandishi wengi hasa mashuhuri ambao kwa njia moja au nyingine
huonekana kuipa hali halisi jamii ya uongozi uliopo ambao huwa kikwazo kikubwa
kwa maendeleo ya taifa. Wengi wa waandishi hawa hukimbilia uhamishoni hadi hali
inayowakubali inapofika katika mataifa yao ndipo wanaporudi. Mfano wa wale walioathirika
ni pamoja na Ngugi wa Thiong’o(nyakati za utawala wa rais mustaafu Moi) wa hapa
Kenya ,Wole Soyinka wa kutoka taifa la Naijeria na Nawal El Saadawi wa taifa la Misri
ambaye alisumbuliwa na kunyanyaswa mno
na serikali dhalimu aliposimama kidete kumtetea mtoto wa kike.
Kama hali ilivyo sasa, umefika wakati ambapo viongozi wa sasa wa mataifa ya
barani Afrika kuheshimu dhamana walizopewa kwa kuhakikisha wanazingatia misingi
ya uongozi bora wenye manufaa kwa wananchi waliowapatia ridhaa ya kuongoza.
Viongozi wetu watambue kwamba uongozi wa
kibabe, kidikteta na kidhalimu hautaishia kuwakosesha tu matakwa yao ya
kibinafsi , bali utawaweka katika hatari ya kuadhibiwa na nguvu ya umma, lakini
pia wataonekana wakosefu hata mbele za Mwenyezi Mungu.
Bara la Afrika limejaaliwa na
Mwenyezi Mungu utajiri wa rasilimali lukuki, zinazopaswa kutumiwa vizuri na
viongozi wetu ziweze kutuendeleza sote katika nyanya mbalimbali zikiwamo za
kielimu, kiuchumi na kijamii kwa jumla kulifanya bara hili kuwa mahali pazuri
pa kuishi duniani.
Waafrika wengi tungependa kama
si kutamani kuona viongozi wetu wanauenzi utukufu huo wa Mungu, kwa kuonesha
uongozi bora unaojali maslahi ya wengi badala ya kujikita katika kujitafutia maslahi
binafsi kiasi cha kukosa sifa za utu na kukaa kama vitu tu vyenye kutu.
v Ufisadi
Ufisadi
ni kule kujipatia mali au kuwezesha hali fulani kufaulu/kufanikiwa kwa kutumia
njia za mkato na zisizo za kimaadili kama ushawishi wa hela, mapendeleo ya
kinasaba/kikabila au hata msukumo wa cheo kwa minajili ya kujinufaisha.
Waaidha, ufisadi ni ulaji rushwa au matumizi ya hongo au mlungula. Ufisadi ni
maudhui ambayo yamejitokeza kwingi katika tamthilia ya Mstahiki Meya.
Ipo
mifano kadha wa kadha kutoka kwenye tamthilia hiyo. Hii ni pamoja na ifuatayo:-
v Panapotokea shida Meya huunda kamati za utatuzi japo hazina umuhimu kwa
Baraza la Cheneo. (uk.22 Diwani III) kamati hizi hutumiwa kudhibiti uongozi
dhalimu wa Mstahiki Meya. Wanakamati hawa hulipwa kwa huduma zao.
v Pendekezo la Diwani I kuwa vijana watunukiwe zawadi na waonyeshwe katika
vyombo vya habari kama fursa ya kuonyesha uzalendo wao. (uk.20). Hii ilikuwa
mbinu mojawapo ya kuwasahaulisha hali duni ya maisha yao.
v Nakisi ya milioni mia moja na
ishirini katika Baraza la Cheneo na Meya asema watafidia.
v Madiwani kujiondolea kodi ilhali watu wote hatamuuza ndizi anatozwa kodi
(uk.22)
v Meya anapoelezwa kuhusu nakisi anasema si neno akidai kuwa anajua diwani
wana njaa hivyo wasilipwe kodi.
v Meya kutaka walinzi wa Baraza waongezwe mshahara kulifaa zaidi kama
hospitalini, kiwanja cha ndege na wanaozoa taka hawalipwi mshahara, wacha
nyongeza.
v Ushauri wa Bili kwa Meya alipotaka kumpokonya aliyepewa kandarasi
unaashiria ufisadi. Anampendekezea Meya asikilizane na aliyepewa kandarasi kuwa
waikatize kandarasi yake, halafu mtu huyo amshitaki Meya. Korti ikiamua alipwe
kulingana na
mkataba wa kandarasi basi mwenye kandarasi ampe Meya sehemu yake.
Asemavyo,
‘Dawa
ya adui ni kummegea unachokula hakudhuru
tena’. (uk.29).
Kwa
yakini swala la ufisadi limekuwa donda sugu katika jamii zetu. Kwa kiwango
kikubwa
sana. Swala hili limeathiri pande zote
za mataifa ulimwenguni kuanzia mashinani hadi kitaifa.
Kufikia March 15, 2016
Ufisadi nchini Kenya ulikuwa umeongezeka na kufikia asilimia 73.9 mwaka wa
2015 ikilinganishwa na asilimia 67.7
mwaka wa 2012.Kwa mujibu wa ripoti kuhusu rushwa iliyotolewa na EACC, kulingana
na ripoti hiyo, wizara ya usalama wa ndani ikifuatiwa na ile ya afya na ardhi ndizo
zinazoongoza kwa ufisadi. Utafiti huu uliofanywa kuanzia agosti hadi octoba
2015 inaonyesha kaunti ya Murang’a inaongoza kwa ufisadi ikifuatiwa na embu na
Bomet.
Aidha asilimia 58 ya wakenya
walitoa hongo ikilinganishwa na asilimia 53 mwaka wa 2015.
Mwenyekiti wa tume hiyo philip kinisu anasema
kuwa miongoni mwa huduma za kitaifa ambazo wakenya wamekuwa wakiitishwa hongo
ni ile ya matibabu, upeanaji wa vitambulisho na vyeti vya kuzaliwa,vile vile
wamesisitiza umuhimu wa kila mkenya kuwajibika ili kukabili ufisadi
nchini.Kulingana na EACC kuna kesi takriban 400 zinazoshughuliwa kwa sasa.
Kwa kurejelea hapo ni kuwa
ni swala ambalo mwandishi analifahamu na kulishuhudia kwa macho yake hapa
nchini Kenya na ulimwengu kwa jumla.Vipovisa mbalimbali hapa Kenya ambavyo
vinatokea kiasi kwamba nchi inapoteza pesa nyingi sana. Hizi ni pamoja na
kashfa nyinyi ambazo taifa la Kenya limekumbana nazo tangu utawala wa Raisi
mstaafu Moi, akaja Kibaki kisha sasa
yupo Rais Uhuru Kenyatta. Kashfa hizi zimefanya Kenya ikapoteza mabilioni ya
pesa kwa njia zisizoeleweka kabisa. Kashfa hizi zitabaki ndonda sugu kwa
wakenya.
·
Goldenberg
·
Anglo
leasing
·
NYS
·
Eurobond
Mbali na kashfa hizi
inaonekana wazi kuwa walio na nguvu za serikali wana nafasi kubwa ya
Kuhakikisha kuwa ajira zile nzuri zinawafikia watu wao pekee huku wengine hata
kama wanafuzu wakibaki wakiguguna mifupa. Ukitazama katika Mstahiki meya
utapata kuwa Bili anajitokeza kuwa mshauri na mshirika mkuu wa Meya ingawa
hayupo popote katika utawala wa Baraza la mji wa Cheneo.
Migomo nchini imekuwa jambo
la kawaida kana kwamba serikali haina macho. Madaktari , wauguzi , wahadhiri na
wengine wengi wamekuwa kucha kutwa wakilalamikia haki yao ambapo kuwalipa
mishahara kulingana na mikataba inayowekwa ni ngumu sana. Hii ni kwa sababu
serikali inaelekeza hazina iliyopangiwa kwa maslahi ya wachache serikalini.
Bili ni kioo cha wengi
ambapo utagundua kuwa wameamua kuwateua watu maalum kuwa washirika wao katika
maswala ya uongozi na utawala.Miradi serikalini ina upendeleo wa kutaka kuona
kuwa faida ni kwa “vipenzi” wa watawala tu bali wasiotambulika hubakia midomo
wazi kabisa kwa kumeza tu mate. Vituko hivi na vingine vingi vilifanya Kenya
kuorodheshwa ya tatu fisadi duniani kulingana na gazeti la standard la Tarehe
27/02/2016.
Ufisadi
unaathiri taifa au jamii vibaya sana. Tukutazama wakazi wa Cheneo hawapati
huduma ya kufaa kwa kuwa viongozi wanajilimbikizia mali bila kuwajali
watawaliwa.
Ufisadi katika serikali umefafanuliwa kuwa matumizi mabaya ya
mamlaka ili kujinufaisha kibinafsi. Ufisadi ulianza zamani. Kwa mfano katika
Biblia, kuna sheria iliyowakataza watu kula rushwa walipokuwa wakishughulikia
kesi, kuonyesha kwamba zoea hilo lilikuwepo zaidi ya miaka 3,500 iliyopita. (Kutoka 23:8)
Bila shaka, ufisadi unahusisha mambo mengi, si kula rushwa tu. Nyakati nyingine
maofisa wa umma huiba mali, hukubali kupokea huduma ambazo hawastahili, au hata
kuiba pesa. Hata wakati mwingine wao hutumia vibaya vyeo vyao kuwanufaisha marafiki
na pia watu wao wa ukoo.
Ingawa ufisadi unaweza kutendeka katika shirika lolote lile
la kibinadamu, inaonekana kwamba ufisadi katika serikali umeenea zaidi. Ripoti
ya mwaka wa 2013 ya Kipimo cha Ulimwenguni Pote cha Ufisadi (Global Corruption Barometer)
iliyochapishwa na shirika la Transparency International, ilisema kwamba
ulimwenguni pote watu huviona vyama vya kisiasa, polisi, maofisa wa umma,
bunge, na mahakama kuwa taasisi zenye ufisadi mwingi zaidi. Acheni tuchunguze
ripoti kadhaa zinazozungumzia tatizo hilo.
·
AFRIKA: Mwaka
wa 2013, maofisa wapatao 22,000 wa umma nchini Afrika Kusini walishtakiwa
mahakamani kwa sababu ya kujihusisha na ufisadi.
·
AMERIKA KUSINI: Mwaka
wa 2012, nchini Brazili, watu 25 walipatikana na hatia ya kutumia pesa za umma
kuwashawishi wapiga kura wawaunge mkono. Miongoni mwa watu hao alikuwa waziri
mkuu wa zamani, mtu wa pili mwenye cheo kikubwa nchini humo.
·
ASIA: Mwaka
wa 1995, watu 502 walifia ndani ya duka moja kubwa jijini Seoul, nchini Korea
Kusini. Wachunguzi waligundua kwamba wajenzi waliojenga jengo hilo walijenga
kwa saruji ya hali ya chini na walipuuza viwango vya usalama. Walifanya
hivyo kwa kuwa maofisa wa jiji walikuwa tayari wamehongwa.
·
ULAYA: Cecilia
Malmström, Kamishna wa Mambo ya Ndani wa Tume ya Ulaya anasema, “Inastaajabisha
sana kuona jinsi tatizo hilo [ufisadi] lilivyoenea Ulaya. Viongozi wa kisiasa
wameshindwa kulikomesha.”
Si
rahisi hata kidogo kwa wanadamu kukomesha ufisadi katika serikali. Profesa
Susan Rose-Ackerman, mtaalamu wa kupambana na janga la ufisadi aliandika kwamba
ili mabadiliko yapatikane serikali inapaswa izingatie “kufanya mabadiliko
makubwa kuhusu utenda-kazi wake.” Ingawa huenda likaonekana kuwa jambo
lisilowezekana kupambana na ufisadi, Biblia inatuhakikishia kwamba kuna mabadiliko
makubwa yanayokuja, na hakika yatatimia.
v Umaskini
Umaskini (kutoka neno la Kiarabu) ni hali ya ukosefu wa mahitaji ya msingi ya binadamu kama vile chakula, maji salama, huduma za afya, mavazi na nyumba kutokana na kukosa uwezo wa kuvinunua. Hii pia inajulikana
kama umaskini uliokithiri au ufukara.
Umaskini wa kadri ni kuwa na raslimali chache zaidi au mapato madogo zaidi
kulingana na watu wengine katika jamii au nchi au
hali ya kadiri duniani. Hali hii pia hujulikana kama umaskini
halisi au unyonge. Umaskini linganishi ni hali ya kuwa na rasilimali chache au
kipato cha chini kuliko wengine kwenye jamii au nchi, au ikilinganishwa na
wastani duniani kote.
Umaskini unajumlisha pia matokeo yake upande
wa siasa na jamii.
Kupunguza ufukara ni kati ya malengo makuu ya taasisi
nyingi za kimataifa, kama vile Umoja wa Mataifa na Benki ya Dunia. Benki hiyo imekadiria kuwa watu milioni 702.1 walikuwa wakiishi kifukara mno mwaka 2015, wakati
walikuwa bilioni 1.75 mwaka 1990 (kutoka
37.1% hadi 9.6%).
Kati yao, milioni 347.1 hivi walikuwa Afrika Kusini kwa Sahara (35.2% za wakazi) na 231.3 Asia Kusini (13.5%), lakini ufukara ni changamoto kwa nchi zote duniani.
UNICEF imekadiria kwamba nusu ya watoto wote duniani wanaishi kifukara (bilioni 1.1).
Wataalamu mbalimbali wamesema sera za uliberali mpya zinazofuatwa na taasisi za kiuchumi za
kimataifa (kama vile IMF na Benki ya Dunia) zinazidisha tofauti za kiuchumi kati ya
binadamu.
Ipo
mifano mbalimbali kutoka kwenye tamthilia ya ya Mstahiki Meya.
·
Wagojwa wanaofika zahanatini hawana pesa za
kulipia huduma wanazohitaji. Siki asema “hawa watu hawana pesa” (uk.2)
·
Wagojwa wengine hata karatasi ya kunakilia
udodosi wao hawana (uk.3)
·
Wafanyakazi kama mama mwenye mtoto mgojwa
zahanatini anasema amemlisha mtoto kiporo cha makombo aliyotoa kwa Mstahiki
Meya. Asema chakula hicho kilikuwa kidogo hivyo yeye hakukila (uk. 4).
·
Mama anapoulizwa na daktari iwapo alikitokosa
chakula anasema hakuweza kwa sababu bei ya makaa na mafuta ya taa imepanda
mno.
·
Wafanyakazi wa Mstahiki Meya hula chakula
kilichopimiwa mbwa nao hukila wasidhurike (uk.5).
·
Waridi anazungumzia umaskini wan chi (uk.3)
anaposema, ‘…… nchi yenyewe maskini; ombaomba’.
·
Watoto wana utapia mlo, umaskini unawakosesha
watu lishe bora. Nesi anasema; ‘Kitoto chenyewe kiriba chaongoza’ (uk.
5-6).
·
Nesi ni mkali (uk.3) na anawazungumzia
wagojwa kwa dharau lakini umaskini unawafanya kumsihi ili angalau wahudumiwe
kwenye zahanati hiyo kwa sababu hawana namna.
·
Umaskini wa nchi unadhihirika katika
utegemezi wa mikopo kutoka nchi geni.
·
Wengi
wa wakazi wa Cheneo ni maskini kiasi kwamba hawawezi kujikimu kwa chakula cha
bei ya chini kama sukuma na dona. Hawawezi kugharamia elimu, aidha wanaishi
mabandani. Medi anasema watoto wao anakula vya kuokota! (uk.61).
Kwa yakini umaskini umekuwa donda sugu katika
jamii zetu. Madharayake yanakuwa chungu nzima.
Ripoti
mbalimbali za benki ya duniaz inasema,
zaidi watu maskini duniani tayari wameumizwa na matukio yanayosababishwa na
mabadiliko ya tabia nchi ikiwemo pamoja na kuongezeka kwa joto, njaa na
mafuriko na kwamba hii inasababishwa na maisha ya watu hao kutegemea ardhi na
kwamba wanaishi katika ukanda ambao uko katika hatari kutokana na ukosefu wa
huduma za jamii."Watu masikini wapo katika hatari zaidi ya majanga
yanayosababishwa na mabadiliko ya hali ya hewa ikilinganishwa na watu matajiri,
kwasababu watu matajiri wanauelewa zaidi na kwamba masikini wanakosa mifumo ya
kifedha na mifumo ya usalama wa kijamii ambayo ingewawezesha kujiandaa vema na
kukabiliana na mabadiliko ya hali ya hewa," zinasema sehemu ya ripoti
hizo.
Umasikini
una athari mbalimbali katika jamii zetu. Mojawapo wa athari hizi ni afya.Theluthi moja ya vifo - watu milioni 18 hivi
kwa mwaka au watu 50,000 kwa siku - vinatokana na sababu zinazohusiana na
umaskini. Kwa jumla, watu milioni 270, wengi wao wakiwa wanawake na watoto,
wamefariki kutokana na umaskini tangu 1990. Wale ambao wanaishi katika
umaskini wanateseka kwa viwango visivyo sawa kutokana na njaa au hata ukosefu wa chakula na magonjwa.
Wale wanaoishi kwa umaskini huishi miaka
michache zaidi. Kulingana na Shirika la Afya
Duniani (WHO), njaa na ukosefu
wa lishe borandilo tishio kuu zaidi kwa afya ya umma
duniani na ukosefu wa lishe bora ndio unaochangia pakubwa vifo vya watoto, katika nusu ya kesi zote. Kila mwaka karibu
watoto milioni 11 wanaoishi katika umaskini hufa kabla ya kufikisha miaka
mitano. Watu bilioni 1.02 hulala bila chakula kila siku. Umaskini huongeza
hatari ya ukosefu wa makazi. Kuna zaidi ya watoto wasio na makao milioni 100
duniani.
Ongezeko la tishio la matumizi ya madawa ya kulevya pia linaweza kuhusishwa na umaskini. Kulingana na Kipimo cha Kiwango Cha Njaa Duniani, Asia ya Kusini ina kiwango kikubwa zaidi
duniani cha watoto wanaokosa lishe bora. Karibu nusu ya watoto wote
nchini Uhindi hawapati chakula cha kutosha, mojawapo wa viwango vikubwa zaidi
duniani na ni karibu mara mbili ya kiwango cha Kusini kwa Sahara barani Afrika
Kila mwaka, zaidi ya wanawake nusu milioni wanakufa kutokana na mimba au wakati wa
kujifungua. Karibu asilimia tisini za vifo vya wakina
mama hutokea katika Asia na kusini kwa
Sahara barani Afrika, ikilinganishwa na chini ya asilimia moja katika nchi
zilizoendelea duniani.
Mbali na afya, elimu vile vile huathirika.Uchunguzi umedhihirisha ya kuwa watoto wanaotoka katika jamii zenye mapato
ya chini wanakumbana na tishio kubwa la kutofanya vyema katika masomo yao. Mara
nyingi, jambo hili huanza kuwadhuru watoto hawa wakiwa wangali katika kiwango
cha shule ya msingi. Katika mfumo wa elimu wa Amerika, watoto hao hupata tishio kubwa zaidi,
ikilinganishwa na watoto wengine, ya kutopata gredi nzuri shuleni, kuwekwa
katika maeneo maalum yaliyotengwa wakati wa masomo shuleni na hata kukosa
kumaliza masomo yao ya shule ya upili Kuna mambo kadhaa yanayoeleza sababu za
wanafunzi kuwa na mazoea ya kuacha shule.
Kwa watoto walio na rasilimali kidogo, tishio linatokana na sababu kama
vile viwango vya watoto waliovunja sheria, viwango vya juu vya watoto waliopata mimba, wakiwa wachanga na kutegemea kiuchumi mzazi au wazazi wenye mapato
ya chini.
Waaidha
umasikini umesababisha utovu wa nidhamu katika jamii kwa kuwa vijana
wamejiingiza katika vitendo viovu. Baadhi ya vitendo hivi ni wizi hata wa
kimabavu, ukahaba na kadhalika. Vitendo kama hivi huidhalilisha jamii kabisa
kiasi kwamba huonekana kama gofu tu.
Sehemu
nyingi za mabanda hapa nchini Kenya zinaimarika kwa kuwa viwango vya umaskini
vinazidi kukwea ngazi kucha kutwa.
v Ukoloni mamboleo
Ukoloni Mamboleo ni neno linalotumiwa na wakosoaji
wa ukoloni kuelekezwa kwa nchi tajiri kuendelea kuingilia masuala ya nchi zinazoendelea baada ya ukoloni wenyewe kwisha kwa
ukiukaji wa azimio la Umoja wa Mataifa. Wanakosoa mataifa ya kibepari kuhusika
na dhuluma katika biashara ya kisasa na yaliyokuwa makoloni.
Wakosoaji wanasisitiza kwamba wafanyabiashara binafsi na makampuni ya biashara ya
kigeni huendelea kunyonya rasilimaliza mataifa baada ya enzi ya ukoloni kama
ilivyotekelezwa kutoka karne ya 16 hadi karne ya 20.
Katika matumizi mapana, Ukoloni Mamboleo
huweza kumaanisha ule ushiriki wa nchi zenye nguvu katika mambo ya nguvu chini
ya nchi; hii ni muhimu hasa Amerika kusini.
Kwa maana hii, Ukoloni Mamboleo huweza kutaja
aina ya kisasa ya ukoloni, uchumi wa ubeberu: kwamba mataifa yenye nguvu kuishi kama
wakoloni, na tabia hii inafananishwa na ukoloni.
Kwa
hivyo ukoloni mamboleo ni ile hali ya mataifa wafadhili au ya kigeni
kudhihirisha ushawishi wake kwa mataifa ya ulimwengu wa tatu kwa kushurutisha
uwepo wa masharti ya kiuchumi, kiasa, kijamii na hata kiteknolojia. Ukoloni
mkongwe nao ni hali ya nchi kuidhibiti au kuikalia nchi nyingine kimabavu kwa
misingi ya kisiasa na kiuchumi kama wakati mataifa machanga barani Afrika
yalipotawaliwa moja kwa moja na wakoloni kutoka bara Uropa.
Wakoloni
hapa walipoondoka na mataifa haya machanga kupata uhuru, bado wameendelea
kuaathiri mataifa haya. Athari hizi hudhihirika kupitia masharti yanayowekewa
mataifa haya machanga na mahusiano ya kiuchumi na kisiasa baina yao na
waliowatawala. Huu ndio ukoloni mambo leo.
·
Dawa inaagizwa kutoka nchi za mbali. (uk.2)
shehena zasemekana ziko bahari kuu.
·
Watoto wa tabaka tawala wanasomea ng’ambo na
akina yakhe ndio wa kung’ang’ana na elimu inayotolewa miaka hamsini baada ya
uhuru. (uk.26).
·
Meya anapotahadharisha kwamba kukaidi mipango
ya mataifa ya nje kuhusu malengo ya milenia ambayo ni ya wafadhili ni hatari.
(uk.14).
·
Siki
kulalamikia hali ya kufuata ushauri wa nchi za kigeni ambao hawakushirikishwa
ni ukoloni mamboleo.
·
Kugawana gharama za huduma ni wazo la mataifa
ya kigeni ilhali wananchi hawana uwezo kifedha. (uk.3).
·
Dhana
ya ubwana na utumwa inadhihirika katika mahusiano baina ya bwana Meya na
wafanyakazi wake Gedi na Dida. Hii ni ishara ya ukoloni mamboleo tunaoupata
katika mataifa mengi machanga miaka mingi baada ya kuondoka kwa wakoloni. Gedi
kila anapoitwa na Meya anaitika ‘yes Sir’. Meya anapokosa hisani
anapopewa pole na Dida katika uk. 9 inagogoteza hali hii.
·
Hali
ya nchi kiuchumi ingali ileile ya ombaomba miaka hamsini baada ya uhuru.
Uongozi wa Baraza unawanyonya wafanyakazi namna walivyofanya wakoloni. Kwa
mfano wafanyakazi wa Baraza hawalipwi mishahara, wanapolipwa ni nusunusu na
wanatozwa kodi, ilhali madiwani wanajipa nyongeza na kukwepa kulipa kodi.
·
Utegemezi wa mikopo kutoka nchi za kigeni kwa
mambo ya kimsingi kama vile kulipa mishahara ya wafanyakazi. (uk.20)
·
Hali ya kupewa ufadhili kwa masharti, kwa
mfano kupewa mkopo lakini kulazimishwa kupunguza idadi ya wafanyakazi. (uk.20).
Ukoloni
mamboleo ni hali ambayo mataifa ulimwenguni hasa nchi zinazoendelea haziwezi
kuepuka kamwe.Katika jamii zetu za sasa inadhihirika wazi kuwa swala la Ukoloni
mamboleo limekita mizizi. Hali hii hujitokeza katika njia mbalimbali kama
zifuatazo:
Ø Mashirika ya
kimataifa
Wakosoaji wa Ukoloni Mamboleo pia wanasema
kuwa uwekezaji na mashirika ya kimataifa uliimarisha maendeleo
duni. Katika baadhi ya nchi, ubinafsishaji wa rasilimali za kitaifa ulifuatiwa na kuongezeka kwa
kiwango cha ukosefu wa ajira, umaskini, na kushuka kwa mapato. Hii ni kweli hasa katika mataifa ya Afrika Magharibi ya Guinea-Bissau, Senegal, na Mauritania ambapo uvuvi una historia
muhimu kwa uchumi wa wenyeji. Kuanzia mwaka 1979, Umoja wa Ulaya ulianza kubana haki za uvuvi katika
pwani ya Afrika Magharibi kinyume cha Mkataba wa Umoja wa Mataifa juu ya bahari ambao unatambua umuhimu
wa uvuvi kwa jamii.
Ø Taasisi za fedha
za kimataifa
Wakosoaji wa Ukoloni Mamboleo walitaka
kukataa mikopo (hasa isiyolipika) kutoka kwa taasisi za fedha za kimataifa kama
vile Shirika la Fedha
la Kimataifa (IMF)
na Benki ya Dunia (WB). Wao wanasema kwamba ili wapewa
mikopo, na aina nyingine za misaada ya kiuchumi, mataifa dhaifu yanalazimika
kuchukua hatua kwa maslahi ya kifedha ya IMF na Benki ya Dunia lakini dhidi ya
uchumi wao yenyewe. Marekebisho ya miundo hayo yana athari ya
kuongeza kuliko kupunguza umaskini ndani ya taifa. Watuhumiwa wa kushiriki
katika ubeberu huo ni pamoja na Benki ya Dunia, Shirika la Biashara
Duniani, G8 na World Economic
Forum.
Wale ambao wanasema kwa hakika na ukweli
kwamba Afrika leo inalipa pesa zaidi kila mwaka katika huduma ya malipo ya
madeni ya IMF na Benki ya Dunia kuliko inayopata katika mikopo kutoka kwao, na
hivyo mara nyingi kunyima wenyeji wa nchi hizo mahitaji halisi. Utegemezi huu
unaruhusu IMF na Benki ya Dunia kulazimisha mipango yao juu ya mataifa
haya. Marekebisho yanayotokana na mipango hiyo, hasa ubinafsishaji, husababisha kuzorota kwa afya, elimu, na kutoweza
kuendeleza miundombinu, na maisha kwa jumla.
Ø Ushawishi Mbadala
Kutokana na akiba kubwa ya fedha, serikali
ya China imeanza kucheza nafasi muhimu dhidi ya ushawishi wa IMF, kwa
kukopesha baadhi ya nchi, kama vile Angola mwaka 2006. Katika
miaka ya karibuni, Jamhuri ya Watu wa
China imejenga sana mahusiano na Afrika,China kwa sasa ni wa pili kwa uhusiano mkubwa na Afrika, baada ya Marekani. Mnamo Agosti 2007, kulikuwa na raia 750,000 hivi wa Uchina wakifanya
kazi au kuishi katika nchi mbalimbali za Afrika wakijipatia rasilimali
- mafuta, madini - ili kulisha uchumi wa nchi yao na kupanua masoko ya makampuni
yake. Mwaka 2006, biashara kwa njia mbili iliongezeka hadi dola bilioni
50.
Mwaka 2007, serikali ya
China na Kongo-Kinshasa ziliingia katika mkataba ambapo makampuni ya Kichina
yanayomilikiwa na serikali yatatoa huduma mbalimbali (miradi ya miundombinu)
katika kubadilishana na shaba ya
migodi.
Watetezi wa haki za binadamu na wapinzani wa serikali ya Sudan wanaonyesha
jinsi China ilivyotoa silaha na ndege ili kupata petroli na gesi ya asili namna ya kikoloni ili kudumisha
udhibiti wao wa maliasili. Kulingana na wakosoaji wa China, China
inayotolea Sudan msaada wake kutishia kutumia kura ya turufu kwenye Baraza la
Usalama la Umoja wa Mataifa kulinda Khartoum kutoka vikwazo juu ya Darfur ili kulinda maslahi yake nchini Sudan.
Ø Korea ya Kusini na
ununuzi wa ardhi
Serikali tajiri na makampuni ya kimataifa
yenye nguvu kutoka Korea ya Kusini zimenunua haraka mamilioni ya hekta za ardhi
ya kilimo katika nchi zinazoendelea katika jitihada za kupata
chakula.Hivyo, serikali ya Korea Kusini sasa hutumia rasilimali za nchi maskini
kwa kununua ng'ambo nishati na chakula, ili kuwa mmoja wa uchumi unaokua kwa
kasi zaidi.
Park Yong-soo wa Korea ya Kusini alisisitiza
kuwa "taifa halizalishi tone moja ya mafuta yasiyosafishwa na viwanda vingine muhimu madini. Kwa nguvu ya ukuaji wa uchumi na kusaidia
maisha ya watu, hatuwezi kusisitiza mno kiasi kwamba kupata rasilimali asili
katika nchi za nje ni lazima kwa maisha yetu ya baadaye.
Mkuu wa Shirika la Chakula na Kilimo (FAO), Jacques Diouf, ameonya kwamba kupanda katika nchi utata
mikataba inaweza kutengeneza fomu ya "ukoloni mamboleo", kwa mataifa
maskini kuzalisha chakula kwa ajili ya matajiri kwa gharama zao wenyewe
na njaa ya watu.
v Utamaduni
Ukoloni Mamboleo unaeneza utamaduni
wa kigeni ili kudhibiti mataifa mengine upande wa maadili na mitazamo kupitia vyombo vya habari, lugha, elimu na dini, hatimaye kwa
sababu za kiuchumi. Kwa mfano, waandishi wanachapa vizuri zaidi himaya ya
kikoloni katika historia ya karne ya 19.
Kuna seti ya nadharia katika falsafa, filamu, siasa, sayansi na fasihi inayoshughulika na historia ya
utamaduni wa utawala wa ukoloni.
v
UFEMINISTI
Ufeministi ni istilahi inayotumiwa kueleza
nadharia ambayo imewekewa misingi na msukumo mkubwa pamoja na nia ya kupigania
ukombozi wa wanawake kutokana na pingu za kiutamaduni na kidini zilizomfunga
kwa muda mrefu. (Malenya, 2012)
Katika Wamitila (2002:235), Ufeministi ni
nadharia inayopinga asasi zote za kijamii zinazochangia katika kudhulumiwa kwa
mwanamke.
Irib (2014) anasema, Ufeministi ni harakati
za ukombozi zilizoanzishwa na wanawake ili kupinga mfumo dume ambao
unawakandamiza wanawake katika nyanja mbalimbali
Hivyo basi, ufeministi ni harakati
zinazofanywa na wanawake kujikomboa katika Nyanja mbalimbali kama; kifikra,
kiuchumi, kisiasa, kijamii na kiutamaduni kutoka katika mifumo ya ukandamizwaji
.
o
Historia ya Ufeministi
Dhana ya ufeministi ilianza kujitokezaa kwa
mara ya kwanza baada ya Simone De Beauvoi aliyezaliwa huko Ufaransa akiwa ni
mtoto wa kike na wa kipekee katika familia yao na ambaye alionekana kama
muhamasishaji wa kwanza juu ya Ufeministi. Hii ilitokana na uwezo mwingi
aliokuwa nao katika kufikiri, hekima na bidii katika kazi vilivyosababisha
kusifiwa daima na baba yake. (Njogu & Chimera, 1999).
Hali hii ilianza
kuibua mtazamo hasi dhidi ya wanawake baada ya baba yake kudai kuwa, uwezo wa
akili alionao unafanana na wake na wala sio kama wa mama yake. (Njogu &
Wafula, 2007). Hali hii ilimfanya Simone De Beauvoi kujenga dhana ya
unyanyasaji wa wanawake na hata kumfanya asifikilie kuolewa bali ajikite na
harakati za ukombozi kwa wanawake
Kupitia harakati zake aliamsha hisia na hari kwa wanawake kutaka
kujikomboa. Baadhi ya nyanja zilizoonekana kumkandamiza mwanamke ni pamoja na
asasi za kijamii kama vile dini, tamaduni na uandishi mbalimbali wa kazi za
fasihi
o
Aina za Ufeministi:
Ufeministi wa Kiharakati; huu ni ukombozi
unaotambua kuwa mwanamke ananyanyaswa na kukandamizwa na mwanaume hivyo kuona
umuhimu wa kuwaelimisha wanawake kukataa unyanyaswaji na ukandamizwaji dhidi
yao.
Ufeministi wa Kiutamaduni; ni aina ya
ufeministi unaotoa wito kwa kila mwanamke kuona umuhimu na wajibu wa kushiriki
katika ukombozi wa mwanamke.
Ufeministi wa Kidhahania; ni aina ya
ufeministi ambao unamwonesha mwanamke kama kiumbe huru mwenye uwezo wa kuteua,
kujilinda na kujitazama atakavyo mwenyewe. Aidha, mwanamke anaona kuwa hakuna
haja ya mawazo yake kuamuliwa na mwanaume au mtu yeyote katika jamii. Kutokana
na dhana hii, jamii imeanza kuwapata wanawake wanajeshi, wazalishaji mali,
walimu na matabibu.
Ufeministi wa kiutamaduni; hii ni aina ya
ufeministi ambayo inautizama utamaduni kama nyenzo kubwa katika kumdhalilisha
na kumfanya mwanamke aamini kuwa anapaswa kuwa na hali aliyonayo mfano;
kukandamizwa, kudhalilishwa na kukosa uhuru wa kutoa maoni.
Maudhui
ya nafasi ya mwanamke yanahusu masuala ya kijinsia hasa vile ambavyo
mhusika wa kike amesawiriwa katika kazi ya kifasihi. Wanawake huwa wanakweza au
kutwezwa katika kazi za kifasihi.Mwandishi wa tamthilia ya Mstahiki Meya amewatumia
wahusika wachache katika mchezo huu. Hata hivyo, nafasi alizowapa hawa wachache
katika mchezo hii. Hata hivyo, nafasi alizowapa hawa wachache zinadhihirisha
kwamba, mwanamke hajaachwa nyuma katika shughuli za mapambano katika jamii.
Yeye (mwanamke) amejifungata masombo kuhakikisha kwamba haki na usawa
vinadumishwa katika jamii kwa minajili ya manufaa ya vizazi vijavyo.
Mmojawapo
wa wahusika wa kike ambaye nafasi yake inajitokeza vizuri zaidi ni
Waridi. Waridi na Nesi katika hospitali ya Baraza la Cheneo. Wanafanya kazi na
wenzake katika hospitali hiyo pamoja na Daktari Siki. Waridi ni mhusika ambaye
anaweza kudaiwa kwamba hajapevuka kamwe kuhusu matatizo yanayokumba nchi yake.
Kwake, ukosefu wa dawa pale hospitalini ni jambo linalosababishwa na hali ya
nchi yake kuwa changa na maskini (uk.3). Haya si madai wala imani ya kweli kwa
kuwa Baraza la Cheneo lina utajiri mkubwa ila tu limeachwa
kuongozwa
na viongozi walafi.
Ingawa
ni mwanamke, ni kinaya kwamba mhusika huyu anamlazimisha mama
mwenye mtoto mgojwa kupiga foleni bila kujali kuwa mtoto yuko katika hali mbaya
kiafya. Kwa hiyo, tunaweza kudai kwamba hana utu wala huruma (uk.3). Je, adui
wa
mwanamke ni mwanamke mwenzake katika jamii? Vilevile, anasisitiza kuwa wagojwa
wazidi kusubiri dawa na kwamba wanaotaka kulazwa walipie gharama hiyo (uk.7).
Hiki ni kinyume na Siki (mwanamume) ambaye anawahurumia wagojwa hao ambao ni
mafukara.
Waridi pia anakata tamaa kutokana na hali mbaya ya mambo pale hospitalini. Dawa
walizokuwa wakisubiri hazikuletwa. Wagojwa waliendelea kufariki pale
hospitalini
kutokana na ukosefu wa dawa. Mambo haya yanamfanya kutamauka na kujiuzulu
(uk.35). Kwa hivyo, ni mhusika asiyekuwa mvumilivu wala hana stahamala.
Hata hivyo, tukigeuza upande wa pili wa sarafu, kuna mwanamke mwenzake ambaye
anapambana bega kwa bega na wanaume katika kukabiliana na dhuluma
zinazoikumba jamii. Huyu ni Tatu ambaye sawa na Medi na Beka ni viongozi na
wafanyakazi. Wao ndio waliotumwa na wafanyakazi kwenda kuwakilisha mbele ya
Meya na kuwasilisha malalamiko yao. Kwa hiyo, katika kiwango hiki, mwandishi
amemsawiri mwanamke kama mshirika mwenza wa mwenzake mwanaume katika
jitihada za kupigania ukombozi.
Tatu
ni mtetezi wa haki za wafanyakazi wenzao. Yeye na wenzake wanapofika mbele ya
Mstahiki Meya, wanawasilisha matatizo ya wenzao jinsi walivyotumwa
(uk.66-72).Katika kutekeleza hili, wanaonyesha ujasiri na hawachelei kumkosoa
Meya. Hawatereki kamwe katika kuutafuta ukweli na wanamwambia Meya ukweli wa
mambo yalivyo katika himaya anayoiongoza. Kwa mfano, wanamwambia bayana ukweli
kuhusu tofauti za maisha kati ya viongozi (matajiri) ambao ni watawala na
maskini (watawaliwa) (uk.69). Maswala kuwahusu Wanawake yamekuwa yakiangaziwa
katika jamii zetu tangu jadi.
Hata
kwa sasa kila jamii inajaribu Kuhakikisha kuwa wanawake wanapewa nafasi yao
kama inavyostahili. Mfano katiba ya Kenya inapendekeza thuluthi ya uwakilishi
wa wanawake kudhihirika wazi katika nyanja mbalimbali. Ukitazama utagundua kuwa
upo wadhifa maalum ambao umetengwa hasa kwa wanawake ambao ni Wawakilishi wa
wanawake(Women Rep) ambacho hicho ni kiti maalum kwa kina mama.
Mbali
na hapo Tumeona wanawake wa Kenya wakitambulika hata kwenye kiwango cha kitaifa
na kimataifa. Hii nikwa sababu ya juhudi zao mbalimbali za kumkomboa mwanamke
na kumpa hadhi yake kama inavyofaa.Waaidha hawa wanawake ni wale wenye
ushawishi mkubwa zaidi kulingana na Ripoti ya www.ureport.co.ke iliyotolewa 09th Mar 2017
Hawani
pamoja na Martha Karua ambaye ni mwanasiasa mtajika nchini Kenya na ambaye amekuwa mbuge wa eneo bunge
la Gichugu kwa muda mrefu. Mbali na hapo alikuwa baadhi ya wanawake wenye
ushawishi mkubwa serikalini wakati wa serikali ya aliyekuwa rais wakati huo,
Mwai Kibaki. Ikumbukwe kuwa yeye pia alikuwa miongoni mwa wajumbe walioteuliwa
na serikali kutafuta uwiano wa taifa hili na upinzani baada ya uchaguzi wa 2007
ulioleta maafa na utata nchini kati ya serikali na upinzani.
Lupita
Nyong’o ambaye aliingia katika kioo cha ulimwengu katika mwaka wa 2014
alipocheza mchezo wa kuigiza kama Patsey katika Steve McQueen 12 years a slave. Shughuli hiyo ilimfanya kupokea tuzo 25
kuanzia mwaka wa 2013 hadi 2014 pamoja na ile tuzo bora zaidi ya Oscar. Kwa
sasa ni mwanamke mtajika na balozi wa Afrika.
Marehemu Wangari Maathai naye pia atakumbukwa na wengi
kitaifa na kimataifa katika utetezi wa mazingira. Mwaka wa 1977 aliannzisha
Green Belt Movement ambayo ilikuwa na lengo la kuhifadhi misitu. Katika mwaka
wa 2004 alikuwa mwanamke wa kwanza mwafrika kupokea tuzo ya Nobeli.
Mkewe rais Margaret
Kenyatta anapendwa na wengi kwa kuanzisha Miradi mbalimbali ambayo inagusa afya
ya watu.Baadhi ya Miradi hiyo ni kupunguza vifo vya watoto na kina mama hata
wanapojifungua. Mradi wake umepewa jina, Beyond Zero Campaign. Oktoba 2014
alitajwa kuwa mwanamke wa mwaka na Umoja wa Mataifa.
Mifano ya wanawake kama
hawa hapa nchini Kenya ni mingi mno ikiwa pamoja na Njoki Ndungu ambaye ni hakimu katika mahakama
ya rufaa nchini,Gina Din ambaye ni mwanzilishi wa kampuni ya Public
Relations Afrika Mashariki na pia balozi wa Msalaba mwekundu. Waidha yupo
Catherine Kasavuli ambaye amekuwa maarufu katika uga wa uanahabari,
Hitimisho
Kama inavyodhihirika katika
makala haya ni kuwa mwandishi yeyote wa kazi ya fasihi huyapata na kuyajenga
maudhui yake kutokana na hali halisi ya jamii. Kwa kupitia tamthilia ya
Mstahiki Meya imekubalika kuwa mtuzi huyu ameyapachua maudhui yake katika jamii
anamoishi au ufahamu wake kutokana na mazingira mbalimbali ambyo amekumbana
nayo.
Maudhui makuu ambayo
yamejadiliwa yamefungamana na mengine madogo ambayo kwayo yanaathiriwa moja kwa
moja na yale makuu. Haya ni pamoja na: udhalimu/unyanyasaji ,utabaka ,ubarakala/ukaragosi,utu
na uadilifu ,matatizo ya uchumi ,usaliti,nafasi ya sheria,haki,uwajibikaji na
mapuuza ,ubinafsi na umangimeza ,unafiki na huduma za kijamii. Kwa hivyo kwa
kuichukua jamii kama kioo cha kumwongoza mwandishi yeyote yule basi atainasa jamii
moja kwa moja.
Marejeleo
a) T.M. Arege(2013)
Mstahiki Meya,Vide Muwa, Nairobi Kenya.
b) C-
Brooks na R.P. Warren, Understanding Fiction, F.S. Crofts
& Co., Inc. 1943.
c) .B.
Deutsch, Poetry Handbook, Jonathan Cape, Thirty Bedford
Square, 1965.
d) W.
Blair (na wenzake), Literature, Scott, Foresman and Company,
New York: 1966.
e) C.H.
Holman, A Handbook to Literature, The Odysey
Press, New York, 1936.
f) R.
Wellek na A. Warren, Theory of Literature, A Harvest/HBJ Book
London 1975.
g) F-V.
Nkwera, Sarufi na Fasihi: Vyuo na Sekondari, TPH, 1978
h) S.D-
Kiango na T.S.Y. Sengo, Hisi Zetu - I . TUKI, 1973.
i)
P. Muhando na N. Balisidya, Fasihi na
Sanaa za Maonyesho, TPH, 1976
j)
H. Arvon, Marxist Aesthetics Cornell
University Pres, 1973.
k) A.
Zis, Foundations of Marxist Aesthetics, Progress Publishers,
Moscow, 1977.
l)
M.Mulokozi, na K-K- Kahigi, Kunga. za
Ushairi na Diwani Yetu", TPH, Dar es Salaam: 1979.
m) F.E.M.K
Senkoro, Fasihi, Press and Publicity Centre, Dares Salaam:
1979.
n) Irib world Service
(march 14, 2014) Matatizo ya Wanawake katika Ulimwengu wa Magharib.www.kiswahili.irib.ir/38823
o) Malenya, M.
M.(2012), Matumizi ya Lugha katika
Fasihi Simulizi. Mwanza: Inland Press.
p) Wamitila, K. M.
(2002), Uhakiki wa Fasihi, Misingi na Vipengele vyake. Nairobi: Phoenix.
q) Njogu, K. &
Chimera, R. (1999). Ufundishaji wa Fasihi. Nairobi. Jomo Kenyatta
Foundation.
r) Njogu, K &
Wafula, R.M (2007). Nadharia za Uhakiki wa Fasihi. Nairobi. Jomo
Kenyatta Foundation