TUKI
(2004), wanadai kwamba lahaja ni tofauti katika matamshi, maumbo na matumizi ya
maneno katika maeneo mbalimbali kwa lugha yenye asili moja.
Aidha
Msanjila na wenzake (2009), wanadai kuwa lahaja ni lugha mojawapo kati ya lugha
ambazo kimsingi huesabiwa kuwa ni lugha isipokuwa inatofautiana katika baadhi
ya vipengele mbalimbali kama vile lafudhi, fonolojia, miundo. Lakini fasili hii
inaibua utata ambao ni lugha, wanatumia istilahi lugha kufasili lahaja, kwani
lahaja ni sehemu ya lugha.
Kwa
ujumla, lahaja ni tofauti ndogondogo za kiusemaji zinazojitokeza katika lugha
moja.
Lugha
ya kiswahili ina lahaja nyingi na kiswahili sanifu ni mojawapo ya lahaja hizo,
katika lugha ya kiswahili uainishaji wa lahaja umezingatia utengano wa kijiografia.
Mfano pemba- kipemba, unguja – kiunguja, kipate- pate, kimakunduchi-
makunduchi. Aidha lahaja nyingi zinapatikana katika upwa wa Afrika mashariki.
Wataalamu
kama Nurse na Spear (1985), wanagawa lahaja za kiswahili katika makundi mawili,
lahaja za kaskazini na kusini, lahaja za kaskazini ni Chimiini, kibajuni,
kipate, kiamu, kimvita, kijomvu, chichifundi na lahaja za kusini kuna
kitumbatu, kimakunduchi, kipemba, kiunguja, kimtang’ata , kivumba, kimafia,
kimgao, kimakunduchi.
Aidha
Iribemwangi na Mukhawa (2010), wanazigawa lahaja katika makundi mawili ambayo
ni lahaja za kijamii ambazo tunapata lahaja kama vile lahaja za kijinsia,
lahaja za kidini, lahaja za kitabaka, na lahaja za kiuchumi, pili ni lahaja za
kijiografia hapa wanataja mfano wa lahaja hizo kama vile lahaja ya kipemba,
kiunguja, kiamu, kipate hizi zinatengwa kutokana na mahali zinapotumika, tatu
ni lahaja za kihistoria ambapo wanaeleza kwamba hapa tunapata lahaja kutokana
na historia, mfano wa lahaja hizo ni lahaja ya kingozi. Lahaja za kiswahili
zinatofautiana kati ya sehemu na sehemu katika vipengele tofauti tofauti kama
vile;
Msamiati,
TUKI (1990), wanadai kwamba msamiati ni jumla ya maneno yanayotumika katika
lugha fulani, baadhi ya lahaja za kiswahili zinatofautiana katika kipengele cha
msamiati usio kuwa wa msingi,
Mfano
Chimbalazi kimvita
Chala-
kidole
chanda-kidole
Kingare kimvita
Biti
– bichi
danga- bichi
Aidha,
lahaja za kiswahili hutofautiana katika kipengele cha semantiki, Richards
(1985), wanadai kwamba semantiki ni stadi ya maana.
Mfano,
Kimakunduchi kiunguja
Bonge-
mwanamke mtu mnene
Asa- kuacha ziwa kutoa onyo
Tembo- uchi wa mwanamke Mnyama
Hivyo,
kutokana na data hiyo ni wazi kwamba maana ya maneno kati ya lahaja moja na
lahaja nyingine unatofautiana.
Aidha
utofauti mwingine upo katika kipengele cha mofolojia kati ya lahaja moja na
nyingine Aurbach (1971), anadai kuwa mofolojia ni neno linalotumiwa kuainisha
utanzu wa isimu unaoshughulikia muundo wa maneno.
Kivumba Kiunguja
Wampigani wamempiga nani
Nyumba yani nyumba ya nani
Hivyo
kutokana na mifano hapo juu ni dhahiri kwamba lahaja ya kivumba inayozungumzwa
sehemu ya wasini na vanga inatofautiana
na lahaja ya kiunguja kimaumbo.
Pia
, fonolojia kati ya lahaja moja na nyingine zinatofautiana. chunguza mifano
kutoka lahaja ya kivumba
Lahaja ya kivumba Kiunguja
Wera waita
Katika
mfano hapo juu tunaona kwamba lahaja ya kivumba inayozungumzwa vanga
inatofautiana na kiswahili sanifu.
Aidha
lahaja hutofautiana na kiswahili sanifu katika kipengele cha msamiati kama vile
Mfano,
kipemba kiswahili
sanifu
Mfereji
bomba
Aidha
lahaja za Kiswahili zinatofautiana katika kipengele cha semantiki,
mfano
Kimakunduchi kiswahili sanifu
Bonge-mwanamke mtu mnene
Asa- kuacha ziwa
kutoa onyo
Pia
lahaja hutofautiana na kiswahili sanifu katika kipengele cha mofolojia.
Mfano
Kingazija
kiswahili sanifu
Soha shoka
Hari kati
Aidha
lahaja nilizozitumia katika kazi hii ni lahaja za kijiografia kwa kuzingatia
namna ambavyo zilivyoainishwa katika maeneo tofauti, aidha Nurse na Spear
(1985), anazigawa lahaja za kiswahili katika makundi mawili lahaja za kaskazini
ni kama vile Chimiini, kibajuni, kipate, kiamu, kimvita, kijomvu, chichifundi
na lahaja za kusini kuna kitumbatu, kimakunduchi, kipemba, kiunguja,
kimtang’ata , kivumba, kimafia, kimgao, kimakunduchi.
Kwa
ujumla, lahaja za Kiswahili sanifu huweza kutambuliwa kwa kipengele cha
msamiati wa msingi ingawa kuna vipengele vingine kama vile lafudhi, mofolojia ,
semantiki, fonolojia, pia lahaja zimesaidia sana katika Kiswahili sanifu.
MAREJELEO
Aubach,
et al (1971) Transformational Grammar : A Guide for Teachers. Research
Associates Inc Washngton
Habwe
J & Karanja P (2007) Misingi ya sarufi ya Kiswahili: Nairobi: phoenix
publishers
Iribemwangi,
P.I & Mukhwana A (2010) Isimu jamii:
Kenya: focus publishers ltd.
Massamba,
D. Kihore, Y. na Msanjila Y. (2004) Isimu
jamii sekondari na vyuo. TUKI.
Nurse,
D na Spear (1985) The Swahili Reconstructing the History and
Language of an African
society.
Philadelphia University of Pennsy Ivania.
Richard
et al (1985) Dictionary of applied linguistics. Longman: harlow.
TUKI
(2013) Kamusi ya Kiswahili sanifu:
Dar es salaam: Oxford University Press.