Wednesday

Je kiswahili ni kibantu?

0 comments

 Kiswahili ni Kibantu

Vipengele vinavyotumika katika kuihalalisha

nadharia inayodai kwamba Kiswahili ni Kibantu ni

ushahidi wa ki-Isimu, ushahidi wa ki-Historia na

kuichunguza lugha ya Kiswahili katika mfumo

mzima wa historia ya mgawanyiko wa kusambaa

kwa lugha za ki-Bantu. Wataalamu wa nadharia

hii wanahitimisha kwa kudai kwamba Kiswahili ni

mojawapo kati ya lugha katika jamii kubwa ya

lugha za ki-Bantu.

Baadhi ya wataalamu muhimu wanaoiunga mkono

nadharia hii ni Prof. Malcon Guthrie, Dkt. C.

Meinholf na Dkt. C. Rohl na Prof. Clement

Maganga.

Profesa Malcom Guthrie ni mtaalamu

(mwanaisimu) mashuhuri kutoka Chuo Kikuu cha

London, Uingereza. Alitumia miaka 20

kuchunguza uhusiano uliopo baina ya lugha za

Kibantu zilizoko katika eneo lote ambalo hukaliwa

na wabantu. Sehemu hii ni ile ambayo inajulikana

kama Afrika, Kusini mwa Jangwa la Sahara.

Alifanya uchunguzi wa mashina/mizizi (viini) ya

maneno 22,000 kutoka lugha 200 za Kibantu.

Katika uchunguzi wake alikuta mizizi (mashina)

2,300 imezagaa katika lugha mbalimbali za

Kibantu na Kiswahili kikiwemo. Mashina/mizizi

500 yalilingana katika lugha zote 200.

Mashina haya yalipatikana katika lugha zote za

Kibantu. Mashina haya yalikuwa ya asili moja.

Baadhi ya lugha hizo 200 zilizofanyiwa uchunguzi

Kiswahili kilionesha kuitikia ulinganifu sawa na

Kikongo kwa asilimia arubaini na nne (44%).

Katika kuchunguza ni asilimia ngapi za mashina

hayo 500 yaliyomo katika kila lugha, mgawo

uliojitokeza ulikuwa kama ifuatavyo:

Kiwemba kizungumzwacho Zambia -

54%

Kiluba kizungumzwacho Katanga -

51%

**Kikongo kizungumzwacho Zaire -

44%**

**Kiswahili kizungumzwacho Afrika

Mashariki 44%**

Kisukuma kizungumzwacho Tanzania

41%

Kiyao kizungumzwacho Tanzania/Msumbiji -

35%

Sotho kizungumzwacho Botswana

- 20%

*Kirundi kizungumzwacho Burundi -

43%*

Kinyoro kizungumzwacho Uganda -

37%

Kizulu kizungumzwacho Afrika Kusini -

29%

Baada ya kupata matokeo haya, Profesa Malcom

Guthrie anaiunga mkono nadharia hii ya kwamba

Kiswahili ni ki-Bantu kwa kudai kwamba:

(i) Kiswahili kilikuwepo kabla ya ujio wa

wageni;

(ii) Anaonyesha kwamba Kiswahili kina

uhusiano mkubwa na lugha za Kibantu;

(iii) Mwisho anasema Kiswahili kilianzia Pwani ya

Afrika Mashariki.

Dkt. C. Meinholf na Dkt. C. Rohl: Wataalamu

hawa wanaamini kwamba:

(i) Wakati wa utawala wa Shirazi katika

upwa wa mashariki ya Afrika kulikuwa na

kabila la Waswahili;

(ii) Kabila hili ni dhuria ya Wazaramo wa

leo.

(iii) Kwa kuwa hawa Wazaramo walikuwa

wamezaliwa katika harakati za kibiashara,

kwa hivyo wakafuata nyayo za wazazi

wao.

(iv) Lugha yao ilikuwa ya aina ya ki-Bantu.

(v) Kwa kuwa Wabantu ni wengi zaidi

kuliko jamii ya makabila mengine, lugha

yao ya Kiswahili ikaanza kutumika na

kuenea katika makabila mengine,

hususan katika ukanda wa pwani ya

Afrika Mashariki.

(vi) Baadaye, Waswahili hawa hawa

wakafanya biashara na wageni waliokuja

kuvinjari Afrika Mashariki, hususan

Waarabu, Washirazi, Wamalaysia, Wahindi

na Wareno ambao tayari walikuwa

wamefurika katika pwani hii ya Afrika

Mashariki miaka kadhaa kabla.

(vii) Vifaa na majina ya vitu vya biashara

vya wageni hao vikaselelea na kuingizwa

katika mfumo wa lugha hiyo ya Waswahili

ambayo ni ki-Bantu.

Madai ya nadharia hii yakichunguzwa, tunagundua

kwamba inazingatia mitazamo miwili yaani,

mtazamo wa ki-Isimu na mtazamo wa ki-Historia.

Kwa mantiki hii, nadharia hii inaelekea kukubalika

na wataalamu wengi kuwa ndiyo sahihi kuhusu

asili au historia ya Kiswahili.

Profesa C. Maganga, na uthibitisho wake kwamba

Kiswahili ni ki-Bantu. Kama tulivyoona, lugha ya

Kiswahili ilifanyiwa utafiti na uchambuzi na

wanataaluma kadhaa kwa madhumuni ya

kuiainisha kama ilikuwa yenye misingi ya ki-Bantu

au la. Prof. Maganga alifanya uchambuzi wa ki-

Isimu na wa ki-Historia kuhusu lugha hii. Matokeo

ya utafiti wake wa ki-Isimu kuhusu lugha ya

Kiswhili (au lugha kwa ujumla) unadhihirisha

mambo mengi, mojawapo ni asili ya lugha hiyo.

Amethibitisha kwamba Kiswahili ni lugha ya

Kibantu; na kwa hivyo, kuthibitisha kwa ushahidi

thabiti hoja ya Dkt. C. Meinholf na Dkt. C. Rohl

kama tulivyoieleza hapo juu.

(i) Ushahidi wa Kiisimu

(a) Msamiati

Matokeo ya utafiti alioufanya kuhusu msamiati wa

Kiswahili ulibaini kwamba 60% ya maneno yote

yanayoweza kuandikwa na kutamkika katika lugha

ya Kiswahili asili yake ni lugha za Kibantu, 30% ni

lugha ya Kiarabu na 10% ni lugha nyingine za

kigeni kama vile Kiingereza, Kireno, Kijerumani,

Kihindi, Kiajemi, Kifaransa, nk. Kinyume chake ni

kwamba msamiati wa Kiswahili na ule wa Kibantu

hautofautiani.

Mfano:

Kiswahili Kindali Kizigua Kijita

Kikurya Kindendeule

Mtu Umundu Mntu

Omun Omontu Mundu

Maji Amashi Manzi Amanji

Amanche Maache

Moto Umulilo Moto Omulilo

Omoro Mwoto

(b) Tungo (Sentesi) za Kiswahili

Miundo ya tungo (sentesi) za maneno ya Kiswahili

zinafanana sana na miundo ya tungo za maneno

ya ki-Bantu. Sentesi za Kiswahili na za lugha za

ki-Bantu zina kiima na kiarifu.

Mfano:

Lugha za Kibantu

Kiima kiarifu

Kiswahili

Juma anakula ugali.

Kizigua

Juma adya ugali.

Kisukuma

Juma alelya bugali

Kindali

Juma akulya ubbugali.

Kijita

Juma kalya ubusima.

Kindendeule

Juma ilye ughale.

(c) Ngeli za Majina

Wanataalamu wanakubaliana kuhusu ngeli za

majina kwa mujibu wa:

maumbo ya nomino (umoja na wingi wa majina)

pamoja; na

upatanisho wa kisarufi katika sentesi.

Kigezo cha maumbo ya majina: Kigezo hiki

hufuata maumbo ya umoja na uwingi katika

kuyaainisha majina. Majina yaliyo mengi katika

lugha ya Kiswahili na lugha za ki-Bantu hufuata

mkondo wa umoja na uwingi. Majina ya lugha ya

Kiswahili na lugha za ki-Bantu yaliyo mengi yana

maumbo dhahiri ya umoja na uwingi.

Mfano:

Lugha za Kibantu

Umoja Wingi

Kiswahili mtu -

watu

mtoto

- watoto

Kikurya omanto -

banto (abanto)

omona - bana (abana)

Kizigua mntu -

bhantu

mwana

- bhana

Kindali mundu -

bhandu

mwana

- bhana

Kindendeule mundu -

βhandu

mwana

- βhana

Kigezo cha upatanisho wa kisarufi katika sentesi:

Katika kigezo hiki tunaangalia uhusiano uliopo

kati ya kiima (jina na viambishi awali vya nafsi)

na vivumishi katika vitenzi vya Kiswahili na ki-

Bantu. Vivumishi, majina pamoja na viambishi

hivyo vya vitenzi hubadilika kutokana na maumbo

ya umoja na uwingi.

Mfano:

Lugha za Kibantu Umoja -

Wingi

Kiswahili Baba analima -

Baba wanalima

Kindali Utata akulima -

Abbatata bbakulima

Kikurya Tata ararema -

Batata(Tata)bararema

Kijita Tata

kalima - Batata

abalima

Kindendeule Tate ilima -

Akatate βhilima

(d) Vitenzi vya Kiswahili na Kibantu

Kuna uhusiano mkubwa sana kati ya vitenzi vya

Kiswahili na vile vya lugha zingine za ki-Bantu.

Vipengele vinavyothibitisha uhusiano huu ni:

Viambishi, mnyumbuliko, pamoja na mwanzo au

mwisho wa vitenzi, kama ifuatavyo:

Viambishi: vitenzi vya lugha ya Kiswahili na vya

lugha zingine za ki-Bantu hujengwa na mzizi

(kiini) pamoja na viambishi vyake vya awali na

vya tamati.

Mfano:

Kiswahili - analima = a –

na – lim - a

Kiikuyu - arerema = a

– re – rem–a

Kindali - akulima = a

- ku – lim – a

1 - 2 - 3 - 4

Sherehe:

1 - Kiambishi awali kipatanishi cha nafsi.

2 - Kiambishi awali cha njeo (wakati uliopo).

3 - Mzizi/Kiini.

4 - Kiambishi tamati.

Mnyambuliko wa vitenzi: Mnyumbuliko wa vitenzi

vya Kiswahili hufanana na ule wa vitenzi vya

lugha za ki-Bantu.

Mfano:

Kiswahili - kucheka -

kuchekesha - kuchekelea.

Kindali - kuseka -

kusekasha - kusekelela.

Kibena - kuheka -

kuhekesha - kuhekelea.

Kinyamwezi - kuseka -

kusekasha - kusekelela.

Kikagulu - kuseka -

kusekesha - kusekelela

Mwanzo wa vitenzi: Vitenzi vyote vya Kiswahili

na vile vya lugha za ki-Bantu huanza na

viambishi ambavyo ni viwakilishi vya nafsi, kama

ifuatavyo:

Mfano:

Kiswahili - N i-nakwenda

Kihaya - N i-ngenda

Kiyao - N- gwenda

Kindendeule - Ni- yenda

Mwishilizo wa vitenzi: Vitenzi vya lugha za ki-

Bantu na Kiswahili huishia na irabu –a.

Mfano:

Kiswahili kukimbi-a - kuwind-

a - kushuk-a

Kindali kukind-a - kubhing-

a - kukol-a

Kisukuma kupil-a - kuhwim-

a - Kutend-a

Kisunza kwihuk-a - kuhig-

a - kising-a

Kindendeule kuβhutuk-a - kuhwim-a

- kuhuk-a

tafiti wa Prof. Maganga kuhusu ushahidi wa ki-

Isimu wa kuthibitisha kama Kiswahili ni ki-Bantu

au la ungeweza kuelezwa kimuhtasari kwa mifano

mingine ifuatayo:

Mfano wa 1:

Lug

ha

Sentesi

Kisw

ahili

Kipa

re

Kind

amb

a

Kich

aga

Kiha

ya

Kika

guru

Kind

end

eule

Jon

go

Jon

go

Jon

go

Jon

go

Jon

go

Jon

go

Jon

go

anaf

uga

eris

ha

kafu

gha

nao

he

n’af

uga

kach

ima

ifug

a

mbu

zi

mbu

ji

men

e

mbu

ru

emb

uzi

m’

ehe

mbu

hi

kuk

u

nku

ku

ngu

ku

ngu

ku

enk

oko

ngu’

ku

ngu

ku

na

na

na

na

n’

na

na

ng’o

mbe

ng’o

mbe

sen

ga.

umb

e

ente

nn’o

mbe

ng’o

mbe

Katika mfano huu inaonekana kwamba mpangilio

wa maneno katika sentesi una ufanano kwa

sababu katika kila sentesi kuna kiima na kiarifu.

Katika kiima kuna nomino, yaani jina la mtenda

(Jongo) na katika kiarifu kuna kitendo

kinachofanyika na nomino mtendwa. Pia nafasi ya

viunganishi ni ile ile kwa lugha zote

zilizoonyeshwa katika mfano huu.

Kuna mfano mwingine wa ufanano wa mpangilio

huu.

Mfano wa 2:

Lugha Sentesi

Kiswahili

Kihaya

Kisukuma

Kinyaturu

Kipare

Kizigua

Sitamkuta kesho

Timushangemu nyenkya

Natusanga intondo

Tumuhanga fadyu

Nesikemkiche yavo

Sirambila luvi

Katika sentensi hizo mpangilio wa maneno una

ufanano kwa sababu kila sentensi ina kiima na

kiarifu chenye kitenzi na kielezi. Pia kiambishi cha

nafsi cha nomino ya mtenda kinajitokeza

mwanzoni mwa neno la kwanza la kila sentesi.

Sitamkuta; Timushangemu; Na tusanga;

Tumuhanga;

Ne sikamkiche; Si tambila.

Viambishi hivyo vya nafsi ya mtenda pia

vinaonyesha hali ya ukanushi katka kila sentesi

na nafasi yake ni ile ile kwa kila sentesi.

Viambishi vya urejeshi navyo vinajitokeza katika

kitenzi cha kila sentesi.

Viambishi {m}, {m}, {ti}, {tu} sita mkuta,

timushangemu, na tu sanga, tumuhanga,

nesikamkiche, na sita mbwila ni vya urejeshi;

vinawakilisha nomino mtendwa.

Kwa hivyo, hali hii inadhihirisha kwamba miundo

ya sentensi hizi inafanana na vitenzi vyake vina

tabia mbalimbali, kama vile:

(i) kubeba viambishi vya nafsi, mtenda na

mtendwa,

(ii) kuonyeshga hali ya ukanushi njeo za

wakati na kitendo kinachofanyika.

Mfano wa 3:

Lugha Sentesi

Kiswahili

Kizigua

Kihaya

Kisukuma

Kinyaturu

Kipare

Kindendeu

le

Akija mwambie

anifuate

Akeza umugambe

anitimile.

Kalaija

omugambile

ampondele

Ulu nahali

anikubije

Newaja mwele

ang’onge.

Ekiza umti

aniratere

Anda ahikite

n’nongerera

angobhekeraye

Katika sentesi hizo inaonekana kwamba sentesi

zote zinafanana kimpangilio. Pia maneno yake

yanakubali uambishaji, kwa mfano:

(i) Katika maneno ya mwanzo:

akija, akeza. kalaija, akuja, newaja, ekiza,

herufi zilizopigiwa vistari ni viambishi vya

nafsi vinawakilisha dhana ya mtenda.

(ii) Vivyo hivyo katika maneno:

anifuate, ampondele, anitimile, ang’nge,

aniratere, angobhekeraye, viambishi

vilivyoko katika viarifu vya sentesi hizo

vinawakilisha nafsi za watenda.

(iii) Pia vitenzi vya sentesi hizo vina tabia ya

kubeba virejeshi vya nafsi kama ilivyo

katika, mwambie, omu gambile,

na ha li, mbwele na umti, vinaonyesha njeo

na hali ya uyakinifu- hali inayoonyesha

ufanano wa maumbo ya maneno.

(iv) Licha ya kuwa na mpangilio unaofanana

na wa lugha nyingine za kibantu, kwa

mfano, katika mifano tuliyoiona hapo juu,

baadhi ya maneno yanafanana: tazama

maneno:

kafugha (Kindamba); nafuga (Kihaya);

nifuga (Kindendeule); anafuga (Kiswahili).

Pia maneno:

nkuku (Kipare); nguku

(Kindamba);

nguku (Kichaga); enkoko

(Kihaya);

ng’uku (Kikaguru);

nguku(Kindendeule);

nguku (Kindendeule)

Katika mfano wa 3, maneno yafuatayo yana

ufanano:

Akeza (Kizigua); kalaija (Kihaya);

alize (Kisukuma),

newaja (Kinyaturu); ekiza (Kipare);

anda ahikite,... (Kindendeule);

akija, (Kiswahili.)

Pia maneno;

umugambe (Kizigua); omugambile

(Kihaya); unongeraye (Kindendeule); na

mwambie (Kiswahili).

Ufanano huu wa msamiati, maumbo ya maneno

pamoja na wa mpangilio wa maneno katika

sentesi, vyote vinathibistisha kwamba lugha ya

Kiswahili ni ya kibantu kama zilivyo nyingi

nyinginezo.

No comments:

Post a Comment