FASIHI ANDISHI
__________________________________________________________________
I.
USHAIRI
Kuna mitazamo ya
aina mbili katika kuelezea dhana ya ushairi.kuna wanamapokeo na mamboleo. Hata
hivyo kabla ya kuendelea zaidi kuwachambua tuangalie wataalam mbalimbali
wanavyofasili dhana hii . Dhana ya ushairi imejadiliwa na wataalamu mbalimbali
huku kila mmoja akitoa fasili yake. Baadhi ya wataalam hao ni kama ifuatavyo:
MAPOKEO
Mssamba, (2003)
akimnukuu Shaban Robert,anasema; “ushairi ni sanaa ya vina inayopambanuliwa
kama nyimbo, mashairi na tenzi zaidi ya kuwa na sanaa ya vina ushairi
unaufasaha wa maneno machache au muhtasari.”
Mnyampala (1970)anasema kuwa
“ushairi ni msingi wa maneno ya hekima tangu kale ndicho kitu kilichobora sana
maongozo ya Dunia kwa kutumia maneno ya mkato na lugha nzito yenye kunata
iliyopangwa kwa urari wa mizani na vina maalum.”
Amri Abeid (1954:1) anasema kuwa “ushairi au utenzi ni
wimbo, hivyo kama shairi haliimbiki halina maana.”
Abdulatifu anasema kwamba
ushairi ni ule ulio na sifa ya ulinganifu wa vina na mizani, lugha laini (lugha
tamu) na lugha hii iweze kugusa moja kama ilivyokusudiwa.
Encyclopedia American (EA) inaeleza kuwa
ushairi ni kauli zenye hisia na ubunifu, mpangilio fulani wenye urari,
uwasilishaji wa tajiriba au mawazo ya mtunzi kwa maana ambayo huibua tajiriba
kama hiyo katika nyayo za wasomaji au wasikilizaji na kutumia lugha ya picha
yenye wizani wa sauti.
MAMBOLEO
Kezilahabi ( )anasema
kuwa “ushairi ni tukio hai au wazo ambalo limeonywa kwetu kutokana na upangaji
uzuri wa maneno fasaha yenye mizani Fulani ili kuonyesha ukweli”
Topan (1996) anasema kuwa
“shairi ni unaoeleza hisia za ndani za binadamu kwa mpangilio Fulani wa maneno”
hivyo kwa mujibu wa Topan ushairi lazima uguse hisia za ndani ya moyo wa
binadamu.
Njogu na Chimerah (1999) wanasema “
ushairi ni sanaa ya lugha inayoeleza jambo kwa njia ya mkato na kwa namna
inavyoteka hisia za msomaji au msikilizaji”
Mulokozi na Kahigi (1982:25) wanasema
ushairi ni “sanaa inayopambanuliwa kwa mpangilio maalum na fasaha na wenye
muwala, kwa lugha ya picha, sitiari au ishara katika usemi, maandishi au
mahadhi ya wimbo ili kuleta wazo au mawazo, kufunza au kueleza tukio au hisia
fulani kuhusu maisha au mazingira ya binadamu kwa njia inayogusa moyo.”
Hivyo basi tunaweza kusema kuwa ushairi ni
kazi ya sanaa yenye kuandikwa au kuimbwa kwa kufuata kanuni za ushairi au
kutofuata kanuni za ushairi ikiwa na maana kuwa ushairi waweza kuwa wa
kimapokeo au wa kisasa ilimradi ushairi huo uwe na ujumbe.
Katika
ushairi FANI na MAUDHUI ni muhimu sana, mawazo fikra au sihi za ndani ni vitu
muhimu sana katika ushairi
CHANZO/CHIMBUKO LA USHAIRI
Dhana ya chimbuko inafasiliwa naTUKI (2004) kuwa ni mwazo au asili ya
kitu.
Baadhi ya wataalamu wameweza kuelezea
chimbuko la ushairi wa Kiswahili kwa kuzingatia mitazamo au nadharia mbili
ambazo ni kama ifuatavyo:
1.
Nadharia
ya kwanza inadai kuwa; Chimbuko la ushairi wa Kiswahili ulitokana na ujio wa
Waarabu.
2.
Na
nadharia ya pili inasema kuwa; Chimbuko la ushairi wa Kiswahili ni zao la jamii
ya waswahili wenyewe.
Hapa tunaenda
kuzielezea nadharia hizi kila moja na kujaribu kuona ubora wake na udhaifu wake
katika kuelezea chimbuko la ushairi
1.
CHIMBUKO
LA USHAIRI INATOKANA NA UJIO WA WAARABU
Kwa kuanza naLyndon (1962) “Swahili Poetry” anatoa
hoja tatu ambazo ni:
·
ushairi
wa Kiswahili umetokana na Uislamu,
·
ushairi
ulianzia kwenye upwa wa kaskazini mwa Kenya hususani Lamu.
·
Na
maudhui ya ushairi wa Kiswahili yalitokana na ushairi wa Kiarabu. Utungo wa
kwanza wa ushairi andishi wa Kiswahili ni Tambuka,
Mwengo bin Athmani (1728)
Ubora
wa Nadharia hii
·
Ubora
wa nadharia hii au mtazamo wa Harries kuhusu chimbuko la ushairi wa Kiswahili
ni kwamba umesaidia wengine kuendelea kuchunguza zaidi kuhusu chimbuko la
ushairi wa Kiswahili.
Udhaifu
wa nadharia hii
® Udhaifu wa
nadharia hii ni kuwa si kweli kwamba ushairi wa Kiswahili uliletwa na Uislamu
bali ulikuwepo hata kabla ya ujio wa Uislamu, kwani ushairi hautenganishwi na
jamii husika. Hivyo jamii za waswahili walitumia Nyanja mbalimbali za ushairi
katika shughuli zao mbalimbali au shughuli zao za kila siku, kama vile;
shughuli za kilimo na ufugaji.
® Pia ushairi wa
Kiswahili ulianza karne ya 10BK na ushairi wa Kiswahili ulikuwa ukitungwa na
kughanwa kwa ghibu bila kuandikwa. Wataalam wengi wanakubaliana kuwa asili ya
ushairi wa Kiswahili ni tungo simulizi hasa ngoma na nyimbo.
®Udhaifu mwingine
katika mtazamo wake wa kusema kuwa ushairi ulianzia pwani ya kaskazini ya Kenya
si kweli kwa kuwa waswahili walikuwepo hata sehemu nyingine kama vile Kilwa na
Bagamoyo ambapo ushairi wa Kiswahili ulitumika.
® Hoja ya kusema
ushairi wa Kiswahili ulitokana na Kiarabu haina mashiko kwa kuwa waswahili
walikuwepo hata kabla ya waarabu na walikuwa na ushairi wao isipokuwa ujio wao
ulileta athari kubwa kwa kuwa ulichanganya na mambo ya dini ya kiislamu na
hati.
®Knappert
(1979)
“Four centuries of Swahili verse” anasema;
“Ushairi wa Kiswahili ulichipuka kwenye upwa wa Kenya kutokana na nyimbo na
ngoma za waswahili na ulianza katika karne ya 17 na pia ni ushairi wa Kiislamu
wenye kuchanganya sifa za tungo za kiafrika na za kiajemi.
Ubora wa hoja hii ni kwamba, ni kweli
Knappert amekubali kuwa,ushairi wa Kiswahili ulitokana na waswahili wenyewe.
Hata hivyo hoja yake ina udhaifu kwa kuwa
ushairi wa Kiswahili ulianza kabla ya karne ya 10 BK na pia amejikita katika
maudhui ya mambo mengine kama vile siasa, uchumi na kijamii. Vilevile
amechanganya chimbuko la ushairi wa Kiswahili na Uarabu.
2. NADHARIA YA PILI INASEMA KUWA USHAIRI NI
ZAO LA WASWAHILI WENYEWE.
Nadharia hii
imejadiliwa na wataalam mbalimbali akiwemo Shaban Robert, Jumanne Mayoka (1993)
na Senkoro, Mulokozi na Sengo.
Jumanne, M. Mayoka (1993) anasema ushairi
umetokana na jamii ya wanadamu wenyewe na umesheheneza ukwasi mkubwa wa lugha
ambayo imekuwa ikitumika katika hatua zote za kisiasa, kiuchumi na kiutamaduni
katika historia ambayo mwanadamu amepitia, Kwa mfano kuwa msamiati uliotumika
tangu enzi za kuishi mapangoni, enzi za uwindaji, ujima, utumwa, vita vya
makabila, uvamizi wa wageni, ukoloni na harakati za kupambana na ukoloni hadi
kupata uhuru na maendeleo yake.
Ubora wa hoja
Ubora wa hoja hii ni kwamba ina mashiko
ndani yake kwa sababu, kila jamii ina sanaa yake na ushairi ni moja kati ya
sanaa hizo ingawa inaweza ikaathiriwa na sanaa ya jamii nyingine. Pia ushairi
umekuwa ukikua na kuendelea kadri jamii inavyokuwa na kuendelea.
Udhaifu wa hoja.
Udhaifu wa hoja hii ni kwamba si kweli kuwa
katika kipindi hicho ushairi ulikuwa tayari umesheheni ukwasi mkubwa wa lugha,
na kama ulikuwa kweli umesheheni huu ukwasi wa lugha alipaswa kutuonesha huo
utajiri wa lugha anaouzungumzia katika ushairi.
Senkoro (1988) anasema kuwa ushairi uliibuka
pale lugha ilipoanza katika kipindi cha uhayawani (kipindi ambacho mwanadamu
alipoanza kupambana na mazingira yake) kwenda katika kipindi cha urazini
(maana) ili kumwezesha binadamu na mazingira yake kwa mfano, zana za kazi
zilizotumika ziliwafanya waimbe kwa kufuata mdundo wa zana hizo.
Masamba anasema kwamba kimsingi chimbuko la
ushairi wa Kiswahili ni waswahili wenyewe katika nyimbo, ngoma nk ambazo
ziliimbwa katika masuala ya kilimo, jando na unyago n.k. Massamba anaendelea
kusema kwamba nyimbo hizi zilikuwa zikiimbwa bila kufuata vina na mizani lakini
kwa kadri muda ulivyoenda walizidi kuziendeleza na kuziboresha. Hivyo suala la
vina na mizani lililetwa na wageni sio kiini cha ushairi wa kiswahili
Mulokozi fasili ya fasihi haiwezi kutenganishwa
na utamaduni wa maisha ya watu. Anaelezea kuwa ushairi wa Kiswahili hutumia
lugha ya Kiswahili, hivyo ili kujua chimbuko la ushairi wa Kiswahili ni lazima
ujue juu ya waswahili wenyewe
Pamoja na kuwa nadharia hii imeonesha
kukubalika na wataalamu mbalimbali kama vile Senkoro, Mayoka na Shekhe Amri
Abeid, lakini bado ina mapungufu. Hii ni kwa sababu imeshindwa kuonesha muda
maalumu ambapo ushairi wa Kiswahili ulianza na ni wapi ulianza kutumika. Hili
ni suala ambalo linaumiza vichwa vya wataalamu mbalimbali hadi hivi sasa, kwani
hakuna mtaalamu yoyote aliyefanikiwa kuonesha ni wapi na ni lini ushairi wa
Kiswahili ulianza.
Hivyo basi, kutokana na nadharia hizo mbili tunaungana na nadharia
inayosema kuwa, chimbuko la ushairi wa Kiswahili ni zao la waswahili wenyewe,
kwa sababu waswahili wana utamaduni wao ambao ulikuwepo kabla ya ujio wa
Waarabu. Na waliutumia ushairi huo katika shughuli mbalimbali za kijamii, kwa
mfano katika harusi, jando na unyago.
AINA ZA USHAIRI/BAHARI ZA USHAIRI
Kwa ujumla
ushairi upo katika makundi mbalimbali. Uainishaji wa ushairi unategemea
wataalam. Mlokozi (1996) anadai kuna
bahari 13 za ushairi ambazo kwa mujibu wa tapo la wataalamu wa Mombassa
1.
Wimbo/Tathilitha
·
Shairi
la aina ya wimbo lina mishororo 3 inayoweza kuwa na mikondo tofauti, unaweza
kuwa na kina kimoja mwishoni
·
Mara
nyingi wimbo huwa na vipande viwili
2.
Shairi/Tarbia
·
Utungo
ambao una mishororo 4 katika kila beti na kila mshororo una vipande 2
·
Shairi
huweza kuwa na maudhui ya namna yoyote ile
3.
Utenzi/utendi
·
Ni
ushairi wenye mizani michache kuliko 12
·
Una
vina vinavyobadilikabadilika isipokuwa cha mwisho
·
Kwa
kawaida husimulia visa virefu vya kihistoria.mfn vita nk
4.
Zivindo
·
Ni
shairi linalofafanua maana ya maneno
·
Lengo
kuu ni kufunza lugha. Mfn shairi la Kihindi.
5. Tumbuizo
·
Hauna
idadi kamili ya mizani na mishororo
·
Nia
yake ni kutoa hisia ambazo zimembana mtu. Mfn Mbolezi-nyimbo za misibani,
nyimbo za kubembelezea watoto
6. Hamziyya
·
Una
mishororo miwili miwili na vina vyake viko mwisho tu wa beti
·
Ulitungwa
na Sharif Aidarus bin Uthman
·
Ulikuwa
ni wa kumsifu mtume Mohamadi S.W.A
7. Dura Mandhuma au Inkishafi
·
Unatokana
na utenzi wa mtu aliyeitwa Inkishafi
·
Una
mambo ya kuonya, kufuata mambo ya kidini na kuelekeza
8.
Ukawafi
·
Una
mstari mmoja wenye vipande vitatu
®Ukwapi-silabi
6
®Utao-silabi
4
®Mwandamizi
5
·
Zinahusu
maudhui ya kidini
9.
Wajiwaji
·
Ni
utungo ambao una mishororo 5 kila ubeti wenye mizani 5
·
Zinahusiana
na mambo ya kidini, kumsifu mtu shujaa na bingwa
10. Wawe au Vave
·
Asili
yake ni kaskazini ya mwambao wa Pwani hasa sehemu za Amu na Pate
·
Unahusu
kilimo, ziliimbwa wakati wa kufyeka mistu, kuchoma pori nk
11. Kimai
·
Ni
utungo unaohusu mambo ya baharini au wakati wavuvi wanapomtafuta mwenzao ambaye
amepotea
·
Ni
utungo unaohusu ubaharia
·
Idadi
ya mizani hubadilika badilika na vina si vya lazima
12. Ngonjera
·
ni
mazungumzo au mabishano ya kishairi kuhusu mada Fulani
·
huundwa
kwa kulumbana pande mbili
·
suluhisho
la kile kinachojadiliwa hupatikana mwishoni
13. Kikwamba
·
Ni
utungo ambao neno moja hutumiwa kila mwanzo wa ubeti na neno hilo hufululizwa
na mabadiliko mbalimbali.
MABADILIKO NA
MAENDELEO YA USHAIRI WA KISWAHILI
MAENDELEO YA
KIHISTORIA:
ü Wataalamu ambao
wanajaribu kutupa taarifa kuhusu maendeleo ya ushairi wa Kiswahili ni pamoja na
M.M. Mulokozi (1996) ambaye anatuambia kwamba ulianza karne ya 10BK
ü Katika kipindi
hiki hakukuwa na ushairi ambao ulikuwa umeandikwa kwa utamaduni wa Waswahili
bali kulikuwa na ushairi simulizi uliganwa kwa ghibu
ü Kuanzia miaka ya
1000BK wakati wa ukoloni kulitokea athari kubwa katika ushairi wa Kiswahili k.v
hati ya maandishi na dini ya kiislamu
ü Ushari
uliwaunganisha Waswahili na duni pana ya umma na taaluma ya uandishi kwa hati
ya Kiarabu uliwapa wenyeji ujuzi wa kusoma na tabia ya kuandika
1000-1500BK
ü Katika kipindi
hiki kulikuwa na ustawi na ustaarabu wa kimji wa waswahili katika miji yote ya
Pwani na biashara ilistawi kati ya
wageni na wenyeji
ü Katika kipindi
hiki fasihi pia ilistawi
ü Mashujaa
wanaosimuliwa katika tendi k.v Fumo Lyongo waliishi kipindi hiki
ü Ushairi
uliendelea kuwa simulizi
ü Ushairi wa
mwanzo uliitwa SWIFA
1500-1750BK
ü Hiki ni kipindi
cha tatu na kilikuwa kipindi cha misukosuko ya wenyeji na Wareno
ü Kulikuwa na
tungo zilizohidhiwa zilizowahusu Wareno, Migeni, Poatugei afila
ü Tungo nyingine
zilikuwa ni utendi wa Hamziyya, Siri Lasinari, Utendi wa Tambuka 1723 nyingi
zilikuwa zikiwapa moyo Waswahili
ü Waswahili walifanikiwa
kuwaondoa wareno.
1750-1900
ü Hiki kilikuwa ni
kipindi cha nne, na kilikuwa ni kipindi cha utawala wa Waarabu
ü Kulikuwa na
migogoro mingi ya kivita katika utawala wa Waarabu
ü Tabia za
Mamwinyi, wafanya biashara, matajiri na wamisionari vilistawi
ü Kipindi hiki
kilitawaliwa na fasihi ya kidini ambayo ilitafakari theologia na falsafa ya
maisha
ü Kulikuwa na
tendi nyingi zilizoibuka kuko Arabuni wakati wa mtume Muhamed. Mfn Shutaki,
Angamia, Nakaa, Masahibu nk
ü Pia kulikuwa na
tungo za kitamaduni, mawaidha na tumbuizo. Mfn utendi wa Mwanakupona
ü Washairi
walijitokeza kuhusu mashairi ya kisiasa ambao ni Myaka bin Haji (1776-1840),
huyu aliishi Mombassa.
KARNE
YA ISHIRINI (20)
ü Katika kipindi
hiki uchapishaji wa magazeti na vitabu ulijitokeza. Kulikuwa na Asasi za kudai
uhuru. Waandishi waliandika sana kuhusu kudai uhuru. Mfn Saada Kandoro
ü Baada ya uhuru
ushairi wa kisiasa ulienea zaidi kama vile Ngonjera na makue.
MAJARIBIO NA
MABADILIKO KATIKA USHAIRI WA KISWAHILI
Senko ( ) anasema baada ya fahamu zake kufunguliwa
alianza kuangalia mabadiliko katika ushairi.alidai kuwa kuwa kuwa dunia
inabadilika hivyo na ushairi hauna budi kubadilika.
ü Wangai Mwai
(2008:73) fasihi hubadilika badilika katika kumbo na maudhui kwa hiyo ushairi
wa Kiswahili sharti uruhusu mabadiliko yanapotokea.
MGOGORO WA
USHAIRI WA KISWAHILI
ü Baadhi ya
washairi kama vile E.Kezilahabi, M.M Mulokozi, K.K Kahigi na wengineo walinza
kuandika kazi za ushairi zisizo na urari wa vina na mizani
ü Wengi
walichukulia na kurudi nyuma kwa ushairi lakini waandishi hao waliona ni hatua
ya maendeleo
ü Hivyo mashairi
yaliyotungwa kwa mfumo huo yalipata majina mbalimbali kama vile Makue,
Mtiririko, Mapingiti. Nk
ü Na hivyo
watungaji wa mashairi haya waliwaita wanamapinduzi na wengine wakawaita
wachochezi
ü Ibrahim Noor Shariff (1988:183) amedai kuwa
mzozo uliibuka pale wanamabadiliko
walipodai mambo matatu:
1)
Mbinu
za kutunga mashairi zilikuwa chache mno
2)
Sharia
za kutunga mashairi ziliwanyima uhuru wa kutunga
3)
Muundo
wa tungo za kishairi uliokuwa wa Kiswahili hapo awali haukuwa na vina wala
mizani, hivyo sharia si za lazima.
ü Kauli hizi za
wanamabadiliko zilipingwa sana na wanamapokeo ambao waliamini kwamba urari wa
vina na mizani ndiyo roho ya ushairi, ruwaza ya vina na mizani ndizo
zinazoufanya ushairi wa Kiswahili ujitambulishe.
Njogu na
Chimerah (1999:113) wanadai kwamba mgogoro huu ulikuwa baina ya vijana na wazee
waliokuwa wamekulia katika mazingira ya tungo za vina na mizani
MAWAZO YA
WANAMABADILIKO KUHUSU USHAIRI
Mawazo yao kwa
ujumla yalipingana kwa kiasi kikubwa na mawazo ya wanamapokeo japo kuna
mazingira Fulani walifanana. Wanamabadiliko waliamini kuwa
v Hakuna sheria za
kutunga mashairi (Kezilahabi 1977:60), kila shairi lina njia yake ya kutunga na
njia yake ya kutoa mawazo.
v Dhamira/maudhui,
mawazo, maadili na falsafa zitawale fani ya ushairi
v Walidai kuwa
mabadiliko ya umbo la ushairi yamefungamana na maendeleo ya historia ya jamii
zetu, ni sehemu ya jamii yetu,hivyo kubadilika kwa ushairi wa Kiswahili si kitu
cha kigeni
v Vina na mizani
ni kunga za utungaji zilizozuia ushairi wa Kiswahili kukua na kusambaa kwa
mapana yake na marefu yake.
Soma Njogu na
Chimerah (1999) ufundishaji wa fasihi.
II.
RIWAYA
Riwaya sio
utanzu wa muda mrefu sana bali ni utanzu ambao umeanza kushika mashiko hivi
karibuni kuanzia karne ya 19 huko Ulaya
Encloypedia hudai kuwa
riwaya ni ubunilizi ya kinathari[1]
inayotosha kuwa kitabu (kitabu kwa mujibu wa UNESCO ni chapisho lolote lenye
kuanzia kurasa 48 na kuendelea.) bunilizi ya kifasihi ni ambapo matukio
mengi yamebuniwa
Enclopedia
Bratanica
wanasema “riwaya ni masimulizi marefu ya kubuni ya kinathari yaliyochangamana
kiasi na yenye kuzungumzia tajiriba[2] ya
binadamu. Wanaendelea kusema kwamba kwa kawaida riwaya huwa na mfululizo wa
matukio yanahusiana na yenye kulihusu kundi Fulani la watu kaka manthari
mahususi
Mphahlele (1976) anasema kwamba
riwaya fupi huwa na kati ya maneno thelathini na tano elfu (35,000) na hamsini
elfu (50,000) na riwaya ndefu zaidi inaweza kuwa na maneno zaidi ya sabini na tano
elfu (75,000)
Mhando na
Balsidyawanadai
kwamba katika riwaya lazima kuwe na mchanganyiko wa matukio na ujenzi wa
wahusika naye Foaster (1949) anachangia kwa kusema kwamba
riwaya lazima iwe na wakati.
SIFA ZA RIWAYA
v
Ni
masimulizi ya kubuni
v
Ni
hadithi ya nathari katika masimulizi
v
Ni
ya mpangilio au hakuna mpangilio
v
Inafungamana
na wakati (yaani yale yanayotendeka katika jamii hiyo)
v
Ina
sifa ya urefu kama tulivyoona hapo juu
v
Ina
mawanda mapana (yaani inaweza kuzungumzia mambo kwa upana sana)
v
Lazima
kuwe na mchangamano wa visa mfano; katika riwaya ya Janga Sugu la Wazawa ina
visa kama, ushirikina, vifo, mapenzi ya kweli na ya uongo,ndoa, mila nk
v
Ina
wahusika wengi
CHIMBUKO LA RIWAYA
Riwaya imejazwa
na mambo makubwa mawili:
1)
Fani
za kijadi za fasihi
2)
Mazingira
ya kijamii
1.
FANI ZA KIJADI ZA KIFASIHI
a)
Ngano-hadithi
za kubuni zinazohusu wanyama, watunzi wengi wameathiriwa na ngano kw wasababu
wanachota visa, mbinu za kifani , dhamira katika ngano (zinaonekana kwamba ni
za kingano zaidi)
b)
Visasili-masimulizi
ya kubuni ambayo yanaeleza juu ya maisha, asili, ya vitu na hatima yake. Kwa
kawaida visasili huaminiwa kuwa ni hadithi za kweli
c)
Visakale-ni
hadithi za kale zinazohusu kabila la kale, udini nk. M.M.Mulokozi anasema kuwa
kila kabila lina visakale vyake. Katika riwaya visakale vinajitokeza katika
riwaya ya Kisima cha Giningi
d)
Hekaya-ni
hadithi za kusisimua kuhusu masaibu na matukio ya ajabu yasiyo ya kawaida, mara
nyingi masaibu yanasababishwa na mapenzi, huwa ni ndefu kuliko hadithi nyingine
lakini si ndefu kuliko riwaya. Katika taaluma ya Kiswahili ni riwaya ya Adili
na Nduguze-Shaaban Robert, Riwaya ya Ubeberu Umeshindwa ya KIIMBILA( 1971)
e)
Tendi-ni
hadithi ya kishairi kuhusu mashujaa wa kihistoria na wakubuni wa jamii au taifa.mfano Utendi wa Fumo Lyongo, kuna
baadhi ya riwaya zimeiga mbinu za kiutendi. Mfano huko Ulaya Illiad Odyssey,
Don Tuliv 1928, Toistoi (1828-1910). Mfano katika Afrika ni riwaya ya Ngugi wa
Thiong’o ya Matigali.
f)
Masimulizi
ya wasafiri-ilihusu masaibu waliyopata wasafiri mbalimbali. Mfano Riwaya ya
kiingereza ya kwanza ni Robinson Kruso ilihusu habari ya mhusika mkuu ambaye
alikuwamo katika merikebu iliyozama na akaokoka na kuamua kuiishi katika kisiwa
peke yake. Katika Kiswahili kuna riwaya kama vile “utumwa” “Kwa Heri Iselamagazi” hizi zote ziko
katika muundo huu.
2.
MAZINGIRA YA KIJAMII
Katika karne ya
16 fani nyingi ziliendelea. Na mojawapo ya sababu ya kuendelea kwa riwaya
ilikuwa ni:
1)
Ukuaji
mkubwa wa shughuli za kiuchumi huko Ulaya baada mapinduzi ya kiviwanda
2)
Mageuzi
ya kijamii na kisiasa yaliyofungamana na mabadiliko ya kiuchumi
3)
Ugunduzi
wa teknolojia ya upigaji chapa
AINA ZA RIWAYA
Mpaka
sasa hakuna vigezo maalumu vya uainishaji wa riwaya, kila mtaalamu huangalia
kwa jinsi anavyoona yeye. Wengine wanaangalia muundo, mtindo, umbo,
lengo/shabaha/historia.Madumula (2009:61
anasema “riwaya inaweza kuainishwa kifani, kidhamira, kihistoria na kiitikadi
Naye
Mulokozi M.M (1996) anaonyesha michepuo miwili ya riwaya:
1)
Riwaya
ya dhati(zinahusu masuala ya kijamii)
2)
Riwaya
pendwa
Katika mhadhara
huu tutaangalia riwaya kama alivyoainisha Madumula
1)
RIWAYA YA KITAWASIFU
v Inahusu maisha
ya mtu binafsi, yaani mwandishi mwenyewe, tatizo hapa ni uaminifu wa mwandishi,
si rahisi kuandika kweli yote.
v Mfano katika
Kiswahili ni Riwaya “Maisha yangu baada ya miaka 50” ya
Shaaban Robert
2)
RIWAYA YA KIWASIFU
v Inahusu mtu
mwingine na siyo mwandishi mwenyewe
v Pia inahusu
maisha ya mtu binafsi lakini ni maisha ya mtu mwingine na siyo ya mwandishi
mwenyewe
v Ni matukio ya
kusisimua ambayo hayajawatokea watu wengine
v Lengo kuu ni
kueleza ugumu wa maisha ya maisha ya mhusika mkuu jinsi anavyopambana na
maisha. Mfano Wasifu wa Siti Binti Saadi ya Shaaban Robert
3)
RIWAYA YA KIMAADILI
v Ina lengo la
kufundisha maadili mema ambayo ndiyo msingi katika maisha
v Inahusu: mateso
na uvumilivu, majuto baada ya kutambua kosa. Mfano katia Kiswahili ni Adili
na Nduguze, Kusadikika, Kufikirika-zote za Shaaban Robert
4)
RIWAYA YA KIHISTORIA
v Huchanganya
historia halisi na sanaa ili kuleta maudhui Fulani
v Hazielezi
matukio yote ya kihistoria bali yale ya muhimu tu, yaliyoathiri mwelekeo na
mwenendo wa jamii Fulani
v Maudhui yake ni
kumbukumbu ya mambo yaliyopita na dhamira zake huwagusa watu wengi. Mfano
katika Kiswahili ni Riwaya ya Uhuru wa Watumwa ya J. Botela, Kwa Heri
Iselamagazi ya J Mapalala, Zawadi ya Ushindi ya Beni Mtobwa, na Njozi
iliyopotea ya Mung’ong’o
5)
RIWAYA YA KISOSHOLOJIA
v Inahusu maisha
ya watu na msisitizo wake ni katika mila, desturi na mabadiliko ya kijamii
v Dhamira huanzia
ngazi ya familia hadi kitaifa na hata kiulimwengu
v Husawiri
matatizo yaliyo katika jamii kwa kuonyesha chanzo chake. Mfano katika Kiswahili
ni Dunia
Uwanja wa Fujo ya Kezilahabi, Siku ya Watenzi Wote ya Shaaban Robert na Harusi ya J.Safari
6)
RIWAYA YA KISAIKOLOJIA
v Aina hii inaweka
mkazo juu ya mikinzano ya ndani ya binadamu, kiakili, kinafsi na kijinsia
v Huonyesha uwezo
na udhaifu wa binadamu katika kuzikabili hali ngumu za maisha
v Mhusika mkuu
husukumwa katika ukingo wa aidha kufa ili ayaepuke matatizo au aishi na hayo
matatizo. Mfano katika Kiswahili ni riwaya yaKIU ya Muhamedi
S.Abdalah, Nyota ya Rehema ya
huyu huyu Muhamed, Rosa Misitika ya Kezilahabi na Kichwa Maji ya Kezilahabi
7)
RIWAYA YA KIMAPINDUZI
v Ni riwaya ambayo
inajadili matatizo ya kisiasa
v Inalenga kuleta
mabadiliko ya kisiasa na kijamii
v Mara nyingi
riwaya za kimapinduzi zina mwelekeo wa kisosholisti ambapo mlengwa mkuu ni umma
kushika hatamu
v Mkazo upo katika
ITIKADI kama msingi na dira ya kuongoza jamii
v Wahusika wake
wanatoka katika matabaka mbalimbali
v Mfano katika
Kiswahili ni riwaya ya KULI ya Adamu Shafi, Utengano ya Saidi A
Mohamed, Dunia Mti Mkavu ya S.A.Muhamedina KASRI MWINYIFUAD ya Shafi A Shafi
8)
RIWAYA YA FALSAFA
v Inajadili
migogoro na maisha ya binadamu kwa kutafakari kwa mantiki na kwa kina kuhusu
mambo yanayohusu maisha
v Inajadili
maswali kama vile: maana ya maisha nini? Hatima ya binadamu nini? Uhusiano wa
binadamu na malaika ukoje?
v Mifano ya riwaya
ya kifalsafa ni: Mzingire, dunia uwanja wa fujo, Nagona, babu alivyokumbuka ya
S.A Muhamedi, Riwaya ya Binadamu-ya K.w Wamitila. Riwaya hizi ni ngumu sana
kuelewa zinaelezea, hata wahusika wake ni wa kufikirika zaidi, mfn wanyama nk
9. RIWAYA
PENDWA
v Ni riwaya ambazo
hujishughulisha na masuala ya upelelezi, mapenzi na ujasusi, mara nyingine
zinahusisha mapigano ya kimwili na ya kiakili kati ya mtu mmoja na watu wengi.
Na mara nyingi huyu mtu mmoja huwashinda watu wengi
v Riwaya hii
inakuwa na mhusika mkuu mkweli (ambaye anapewa sifa ambazo zinazidi uwezo wa
mwanadamu wa kawaida-yaani huwezi kumshinda kuanzia mwanzo hadi mwisho). Riwaya
za namna hii zina chumvi nyingi. Mfano Riwaya ya “Kifo ni haki yangu” mhusika
wake mkuu Camila anayekata nyeti za wanaume. Mfano mwingine ni Simu ya kifa ya Faraji Katambula, Kikosi cha
Kisasi ya E.Musiba. Mzimu wa watu wa kale, Kosa la Bwana Msa-vya Muhamedi
S.Abdula-mhusika wake mkuu ni Msa
HISTORIA YA
RIWAYA YA KISWAHILI
v Utanzu wa riwaya
umekuja baada ya utanzu wa ushairi na tamthiliya lakini ukuaji wake umekuwa kwa
kasi kubwa. Inasemekana kwamba riwaya ya Kiswahili ilianza kujitokeza katika
mwisho mwa karne ya kumi na tisa. Kwa nini ilichelewa sana hapa Afrika? Sababu
yake ni kwamba
1. Hadhira kubwa ya watu haikujua kusoma na
kuandika
2. Hadhira kubwa ya watu haikuweza kununua
vitabu
3. Jamii ya waswahili haikuwa na mitambo ya
kupigia chapa na pia haikuwa na mfumo mzuri wa usambazaji vitabu(hapakuwa na
printers nk)
Hivyo
tunaona kwamba wakati wa ujio wa wakoloni ulisababisha kuanzishwa kwa baadhi ya
vituo vya kupigia chapa, kwa mujibu wa Mulokozi ( ) anasema ukoloni uliweka
mazingira ambayo yameweza kuilea riwaya. Mfano: hati ya maandishi ya Kirumi,
mfumo wa usambaji wa vitabu
Mwanzo
riwaya ya Kiswahili ilianza kujitokeza kwanza kama tafsiri ya kazi za nje,
hivyo tafsiri nayo ilisaidia sana kuchipuka kwa riwaya. Kwa kadri tafsiri
zilivyokuwa zikifanywa, waswahili walianza kuiga vitabu hivyo.
1930
KULIANZISHWA KAMATI YA LUGHA YA AFRIKA MASHARIKI
Kamati
hii ilihimiza uandishi katika lugha ya Kiswahili kwa njia ya kushindana. Hivyo
ilianzisha mashindano ya uandishi wa Kiswahili. Riwaya ya kwanza ya Kiswahili
ilikuwa Uhuru wa Watumwa ya MBOTELA Ilichapwa mwaka 1934, riwaya nyingine ni
riwaya ya “Mzimu wa watu wa kale”na “Simu ya Kifo”
MWAKA 1940 hadi
1960
Kulijitokeza
riwaya ambazo zilikuwa zikifuata mkondo wa kingano.Njogu na Chimerah (2008)
wanaeleza kuwa”kimaudhui riwaya nyingi zilikuwa na mambo ya kimila na tabia
kama njia ya kutunza maadili. Miongoni mwa riwaya hizo ni Utu bora mkulima,
Kufikirika, Kusaidikika, Adili na Nduguze na Siku za watenzi wote zote za
Shaaban Roberti.
Kulikuwa
na mambo yafuatayo:
Ukombozi
wa bara la Afrika na ujenzi wa jamii mpya, hivyo maudhui yake yalikuwa ni
ujenzi wa jamii mpya na:
• Kusuta ubinafsi na ukandamizaji
• Zilikuwa zikihakiki unyama wa maisha ya
kimiji
• Zilikuwa zikiielekeza jamii katika mkondo
wa kibinadamu katika usawa na ustawi. Mfano riwaya hizo ni LILA NA FILA, KABURI BILA MSALABA-iliandikwa na KAREITHI
Katika
kipindi hiki pia kulijitokeza kundi la Riwaya Pendwa zilizohusu upelelezi na
uharifu mfano Mzimu wa watu wa kale, Kisima cha Giningi, Simu ya Kifo
Zile
za uharifu niMTAKA YOTE HUKOSA YOTE ya
Leo Odera Omera, Tatizo Kisauni ya CHADHORO
MIAKA YA 1970
HADI 2000
v Ni kipindi cha
kupevuka na kushamiri kwa riwaya ya Kiswahili, katika kipindi hiki riwaya
nyingi zilianza kujishughulisha na uongozi na usaliti wa kisiasa.
v Njogu na
Chimerah (2008) wanadai wasanii walianza kutafakari jinsi ukoloni ulivyoanza
kufungua milango kwa watu wachache na kutumia mali kwa manufaa yao wenyewe
v Katika kipindi
hiki kuliibuka riwaya za kihistoria kwa mfano KWA HERI ISELAMAGAZI iliyoandikwa
na Mapalala. Miradi Babu ya wazalendo.
v Katika kipindi
hiki kulizuka riwaya ya kifalsafa na ya majaribio. Mfano Nagona 1987,
Mzingile(1991)-Kezilahabi. Riwaya ya Zilahiri na Zirani ya William
v Katika kipindi
hiki kulikuwa na ongezeko la riwaya ya vijana na watoto. Mfano wa riwaya hizo
ni Mashujaa wa Kaza kamba-ya Shija (1980) wimbo wa Sokomoko (1990), Ngome ya
Mianzi (1990), Ngoma ya Mianzi(1991) Moto wa Mianzi (1995) zote hizi ni za
Mulokozi.
MAJARIBIO NA
MABADILIKO KATIKA RIWAYA YA KISWAHILI
®Fasihi
huithamini jamii kihistoria, kiitikadi, kisiasa, kiuchumi na kiutamaduni na
kijamii, na kwa kuwa jamii imekuwa ikibadilika badilika kimtazamo, fasihi nayo
imekuwa ikibadilika kwa sababu jamii inabadilia. Na hivyo fasihi nayo inahitaji
kupokea mabadiliko hayo ili kwendana na jamii husika.
®Mabadiliko
katika riwaya (fasihi) yanatokea kwa sababu ya wasanii kutumia vionjo vipya
katika kuziumba kazi zao. Kama anavyosema Khamisi (2007) anasema,mara moja
tunaona neno kionjo linajisemea lenyewe kimya kimya juu ya mabadiliko ya utanzu
wa fasihi. Lengo la mabadiliko hayo ni kwamba “chenye mwanzo hakikosi kuwa na
mwisho”
®Utanzu wa riwaya
ya Kiswahili haukuepuka mabadiliko. Sababu zilizobadilisha mabadiliko haya ni
makali ya wembe wa kisiasa, mfano nchini Kenya makali ya kisiasa yalikuwa dhidi
ya Masosholisti. Mfano wa riwaya ni Gamba la Nyoka,
®Majaribio na
mabadiliko ya riwaya ya Kiswahili yalianza pale ambapo waandishi wengi wa Kenya
na Tanzania walipoanza kukataa kukubali kila kitu walichokisikia. Walipoanzaa
kukataa kanuni za jamii za ughunaji, hivyo wakaanza kuandika riwaya tofauti na
za mwanzo.
®Madumula
anawanukuu SCHOLES na APLLOE riwaya huweza kubadiliko kutokana na utanzu
wenyewe kuwa hauna mashiko legelege na tepetepe, hubadilika badilika
®Hivyo kutokana
na majaribio na mabadiliko katika riwaya ya Kiswahili tunaona upywa katika kazi
za riwaya katika fani na maudhui yake. Kisanaa riwaya hizi zinachanganya
uhalisia na falsafia. Mfano wa riwaya ya Kufikirika. Mfano mwingine ni
UKIUSHI-Mtiririko haueleweki, na riwaya hizi zinakuwa na mwingiliano matini
yaani kuchanganya kazi nyingi katika kazi moja.kisanaa pia zina wahusika wa
kidhani
®Pia riwaya hizi
zina mazingaombwe sana, kwa mfano katika Nagona lugha yake ni ya mafumbo,
visasili, pia ni lugha inayoelekeza, haifafanui sana.kimaudhui riwaya hizi za
majaribio inatazama matatizo kwa mtazamo wa ndani. Inashughulikia masuala ya
ulimwengu wote, riwaya hizi pia kimaudhui zinaitetea dunia dhidi ya maangamizi
ya uovu mkubwa.
3.
TAMTHILIYA NA
DRAMA
Kumekuwa na
mkanganyiko kati ya dhana hizi mbili, watu wamekuwa wakizichanganya sana.
·
Tamthiliya ni drama na kinyume chake
·
Tamthiliya
ni drama lakini si drama zote ni tamthiliya
A.
TAMTHILIYA
·
Mulokozi
(1999:88) tamthiliya ni kazi iliyokusudiwa kutendwa jukwaani kwa ajili ya
hadhira fulani
·
Tamthiliya
huitwa mchezo wa kuigiza. Istilahi hii tamthiliya imetokana na neno methali
lenye maana ya mfano/ishara ya kitu
·
Wamitila
(2003)tamthiliya ni kazi ya kidrama na ya kimaongezi ambayo huigizwa mbele ya
hadhira/kazi iliyoandikwa ili kusomwa
·
Kimuundo
tamthiliya hudhihilika katika:
®matendo na maonyesho, mazungumzo
huchukua sehemu kubwa katika uwasilishwaji wake wa maudhui (huwa katika
diolojia)
®haiweki msisitizo mkubwa katika
uwasilishwaji wake jukwaani wakati drama inaweka msisitizo mkubwa katika
uwasilishwaji wake
®Penina Mhando anadai kuwa “Tamthiliya ni ule utungo unaoweza kuwa
umeandikwa au haukuandikwa ambao ambao unaliweka wazo linalotaka kuwasilishwa
katika umbo la tukio la kiliwezesha kutendeka mbele ya hadhira”
·
Kutokana
na sifa hii ya kutendeka jukwaani tamthiliya inawekwa kwenye kundi la sanaa za
maonyesho(Mulokozi)
SANAA ZA
MAONYESHO
Mohamedi na
Balysidya wanasema kuwa sanaa za maonyesho ni kitendo chochote chenye sifa 4
a)
Mchezo
b)
Mchezaji
c)
Uwanja
wa kutendea
d)
Watazamaji
©tamthiliya ni
andiko la kiuigizaji linalotoa simulio kwa kuonyesha maneno na matendo
B.
DRAMA
Wamitila (2003)
anasema “ ni aina ya utanzu wa fasihi ambao kimsingi hudhamiriwa kuigizwa mbele
ya hadhira” inaweza kuwa imeandikwa au haikuandikwa lakini msisitizo wake ni kuigizwa
·
Msingi
mkuu wa drama ni utendaji na utanzu huu umebuniwa kwa ajili ya thieta
·
Wahusika
hupewa majina ya kuigiza mbele ya hadhira
Iwochukuu (2000)
anasema “drama ni mabadiliko, ubunifu na usawiri wa uhalisi jukwaani. Msingi
mkuu wa drama ni matendo. Hoja hii imeungwa mkono naAristotle anayeifafanua drama
kama uigaji wa matendo
·
Bretcht
anasisitiza kuwa drama si uigaji wa matendo pekee pia ni chombo cha ufafanuzi
wa hali za kijamii, chombo cha mabadiliko ya kisiasa na kiuchumi
·
Kitendo
huitwa drama endapo kitendo hicho ni mwigo wa kitendo cha
kilichokwishatangulia.
DRAMA ZA KIJADI
Jamii ya
waafrika ikiwemo ambayo utamaduni wake ulikuwa haujaingiliwa na wakoloni
ilikuwa na sanaa ya maonyesho zilizogawanyika katika makundi mbalimbali.
Balisdya na Mhando walianisha aina mbalimbali za drama hizo
1.
SHEREHE
·
Zilihusishwa
na kundi moja kwenda kundi jingine mfano. Jando na unyago, jina kwa mtoto,
kuota meno nk
·
Ziliambatana
na madaraka kwa mwanajamaii ya mwanajamii aliyeingia katika kundi jipya.
sherehe ziliwekwa katika katika umbo la vitendo na vikapewa uzuri wa kisanaa
2.
NGOMA
·
Mhando
na Balisdya wanasema ni chombo, sherehe au uchezeshaji wa viungo vya mwili.
Malengo yake ni kuburudisha
3.
MASIMULIZI YA
HADITHI
·
Katika
usimuliaji wa hadithi kuna vipengele vya kidrama vinavyojitokeza. Yaani:
v
Usimuliaji
v
Uigizaji
v
Uimbaji
v
Muziki
4.
KUSALIA
MIUNGU
·
Jamii
fulani inapopata mafanikio au matatizo fulani ndipo huenda kutambikia miungu
yao kwa kushukuru au kuomba kutatuliwa matatizo yao
5.
MAJIGAMBO
·
Masimulizi
ya kujigamba ya mtu kuhusu mambo ya kishujaa aliyopata kuyatenda maishani mwake
·
Kwa
kawaida hutumia lugha ya kishairi na masimulizi huambatana na vitendo vya
majigambo yenyewe.
·
Pia
yaliambatana na matumizi ya maleba
AINA ZA
TAMTHILIYA
1.
TANZIA
·
Ni
tamthiliya yenye huzuni inayogusa hisia za wasomaji kiasi cha kuogopesha na
kumuonea huruma mhusika mkuu ambaye hupatwa na masahibu/matatizo/majanga hayo
·
Msingi
mkuu inalenga msomaji kupata hisia
·
Mhusika
mkuu huwa ni maarufu
·
Aristotle
anasema kuwa “ mhusika mkuu lazima atoke katika familia yenye nasaba
bora/tabaka la juu”
·
Si
tanzia zote mhusika anatoka tabaka la juu. Mfano KIFO KISIMANI-mhusika mkuu
hapa anatokea katika tabaka la chini kabisa
Misingi ya
utokeaji wa tanzia
·
Iamushe
hisia za woga na huruma miongoni mwa hadhira
·
Shujaa
lazima awe mtu mwema, sura nzuri,umbo zuri, ili yanayomtokea yasitarajiwe
·
Mhusika
huonyesha kuumia kadri mtu anavyoonekana kuwa ni mwema na ana umbo zuri.
·
Anguko
la shujaa huja kutokana na uamuzi wake ama kosa lake mwenyewe
·
Katika
tanzia ya kirasimi shujaa hutoka katika nasaba bora
2.
RAMSA/KOMEDI
·
Ni
tamthiliya ambayo inachangamsha na huishia kwa kufurahisha/ni tamthiliya ya
vichekesho, hii haina maana kwamba haina maudhui mazito ndani yake.
·
Inashughulikia
mambo yale yale yanayoweza kushughulikiwa na tanzia. Mfano masuala ya
unafiki,uzembe, wivu nk, hata hivyo inayashughulikia kwa namna tofauti na
tanzia
·
Kwa
kawaida wahusika wa Ramsa huumbwa vibaya kuliko walivyo
·
Udhati
wa ramsa si kwamba usanii humalizika katika kicheko/furaha zaidi ni kuishia
mhusika mkuu kufanikiwa
shujaa wa kiramsa
·
Si
lazima awe mtu maalum/mbabe au shujaa, anaweza kuwa mtu wa kawaida
·
Kwa
mujibu wa Aristotle anasema mhusika wa ramsa lazima awe mtu wa wastani chini ya
wastani, awe ni mtu ambaye hatarajiwi kujitokeza na mtu wa nasaba duni na
matendo yake yawe ya ucheshi
·
Ni
lazima awe mtu ambaye akifanikiwa wasomaji au watazamaji watafurahi
uhusika wa wahusika wa ramsa
·
Ramsa
inawahusu watu wa kawaida kuliko ilivyo tanzia
·
Inawahusu
watu wa kipato cha kati na cha chini
·
Na
dhamira zote huelekezwa kwa watu wa kipato cha chini na duni. Mfano walalahoi
AINA ZA RAMSA
a)
UTANI
·
Ni
aina ya ramsa ambayo mambo inayozungumzia yanaokana kuwa ya kipuuzi
·
Mambo
hugeuzwa kuwa kinyume kabisa na jinsi yalivyo
·
Kwa
kawaida sura za wahusika hubadilishwa kuwa kama vinyago
·
Lengo
kuu ni kuchekesha-ambalo ndilo haswaa, lengo la tamthiliya ya ramsa
b)
RAMSA
ZA MAPENZI/MAHABA
·
Hizi
zinahusu mapenzi ambapo wapendanao huwekewa vikwazo kama vile fedha, elimu,
din, kabila nk
·
Wahusika
hawa hushinda vikwazo hivyo
c)
TASHTITI/DHIHAKA
·
Zinalenga
kwa viongozi wa kisiasa au dini
·
Zinawahusu
matapeli, wanafiki, wala rushwa, ni
·
Mhusika
mkuu anakuwa na sifa za utapeli nk
·
Lengo
kuu ni kumdhihaki huyu kiongozi ili aachane na tabia hizo
·
ni
njia ya walalahoi kupeleka malalamiko yao kwa viongozi
SIFA ZA RAMSA
·
Shartiivutie
akili na siyo hisia
·
Ni
lazima kuwa na matendo bila kufikiria hii itapelekea msomaji au mtazamaji kujua
kwamba wahusika hawa hawana akili
·
lazima
iwe na hali ya utu (ikitukumbusha
ubinadamu wetu)
·
sharti iwe na mila na desturi ambazo hadhira
inazifahamu toka katika jamii yake
·
Hadhira
isiogope au kupata uchungu kwa sababu hii sio lengo lengo la ramsa
·
Wahusika
wa ramsa hujaribu kuepuka vikwazo ambavyo vimewekwa
·
Inaonyeshahaja
ya kuikomboa
nafsi
Mfano wa ramsa ni kama vile
MFALME JUHA
d)
TANZIA-RAMSA
·
Hii
ni tamthiliya ambayo inaonyesha mabaliko ya aina fulani yanayogeuza matukio ya
tanzia kuwa ya ramsa
·
Ni
tamthiliya inayochanganya vipengele vya tanzia na ramsa
·
Hutumiwa
sawa na tamthiliya ya kibwege-hii ni tamthiliya ambayo
inaonyesha kwamba kicheko au furaha ndiyo jibu pekee la maisha kwa watu ambao
hawana imani na maisha ambao kwao misingi dhabiti ya maisha imeondoleo. Mfano tamthiliya ya AMEZIDI ya S.A
Mohamedi
e)
MELO-DRAMA
CHIMBUKO ,
MABADILIKO NA MAENDELEO YA TAMTHILIYA YA KISWAHILI
CHIMBUKO LA
TAMTHILIYA
Tamthiliya chimbuko lake duniani kote
linashahibiana/zinapatikana duniani kote na kuonekana katika maumbo tofauti
tofauti. Tamthiliya inahusishwa sana na visakale na matendo ya kidini. Katika
bara la Ulaya tamthiliya inahusishwa na miviga ya kidini katika jamii ya
Wayunani/Wagiriki wa zamani/ancient Greek. Miviga hii katika jamii ya wayunani
iliambatana na dua ya kuzaliwa..mpaka kufa na kuoza na kuwa binadamu tena
1.
Huko India
tamthiliya
zilitokana na tenzi zilizoitwa Mahabharata
na ………pia zilitokana na miviga zilizoendana na utendi wa tendi hizo kutika
mahekalu ya kidini
2.
Kule Japani na China-drama inatokana
na dansi na miviga ya kidini baadaye miviga hii ilijitenga na dini na kuanza
kujishughulisha na sanaa
3.
Katika Afrika-maigizo ya
tamthiliya yalikuwa yanapatikana huko Misiri na maigizo haya yalikuwa yanahusu
kufa na kufufuka kwa mungu wa wamisiri aliyeitwa osiais. Miviga hii ilikuwa inaigizwa kila mwaka kwa miaka kama elfu
mbili. Pia katika Afrika kulikuwa na maigizo ambayo hayakuwa yameandikwa lakini
yalikuwa ni sehemu ya matendo ya kijamii yaani miviga na ngoma. Kulikuwa na
tamthiliya bubu, maigizo ya watoto na maigizo ya watani. Drama hizi zilikuwa
zikifungamanishwa na fasihi simulizi
Hivyo
tamthiliya inatokana na mambo makuu matatu
a.
Miviga
na viviga vya kijamii, na dini pamoja na tendi
b.
Usawilishaji
wa maisha ya kawaida kwa ajili ya burudani, elimu nk
c.
Sanaa
za maonyesho za kijadi; ngoma na dansi
MAENDELEO YA TAMTHILIYA YA KISWAHILI 9/1
Maendeleo ya
tamthiliya yamegawanywa katika vipindi vitatu
1.
KABLA
YA UKOLONI:
Ø
Kulikuwa
na tamthiliya ambazo hazikuandikwa lakini zilikuwa zikionyeshwa katika matukio
mbalimbali kama vile jando na unyago, arusi nk
Ø
Hazikuwa
na muundo wa Kiaristotle: mwanzo, kati na kilele
2.
KIPINDI
CHA UKOLONI
Ø
Kilianza
mwaka 1860-1960
Ø
Kipindi
hiki kilikuwa na aina mbili mpya ya tamthiliya
a.
Kizungu
—zililetwa mwanzoni mwa utawala wa wazungu. Zilikuwa na malengo mawili: 1.
Kuwaburudisha wazungu 2. Kufunza imani
ya kikristo.
®
Huko
Kenya ilianza kuonyeshwa/kuigizwa Nairobi na mombassa kabla ya vita ya kwanza
®
Tanzania
zilianza kuigizwa mashuleni mwaka 1920
®
Katika
kipindi hiki kulianzishwa vikundi mbalimbali za kuigiza tamthiliya ya kizungu.
Mfano hapaTanzania kundi lilianzishwa ni Dar es salaam player 1947. Na kundi
lingine ni Arusha Little Theater
®
Na
huko Kenya kulikuwa na kundi la National Theater 1952
Makundi haya
yalitawaliwa na michezo ya wageni
b.
Vichekesho:
--zilikuwa ni tamthiliya gezwa.
®
Zilianza
mwaka 1920 kwa ajili ya kuwaburudisha wenyeji
®
Miongoni
mwa vichekesho maarufu ni kile cha KIOO
c.
Mwisho
ilijitokeza aina ya tatu: TAMTHILIYA ANDISHI ZA KISWAHILI
®
Zilianza
kujitokeza mwaka 1950
®
Zilianza
kutungwa mwaka 1952
®
Shughuli
za tamthiliya zilikuwa zikisimamiwa na Gramah Gyslop-huyu alikuwa ni mkoloni
huko Kenya aliyepewa kusimamia tamthiliya..mwaka 1954 yeye mwenyewe alianza kuandika.
Mfano ni tamthiliya ya kuigizwa ya AFADHALI MCHAWI
®
Henry
Huria aliandika tamthiliya iliyoitwa: NAKUPENDA LAKINI nayo iliigizwa mwaka
1954 na kuchapwa 1957
®
Baada
ya Henry motisha ya kutunga tamthiliya iliongezeka. Kulijitokesha watu wengi wa
kutunga. Mfano GERSHOM NGUGI, tamthiliya ya NIMELOGWA NISIWE NA MPENZI
®
NYOIKE
aliandika tamthiliya ya MAISHA NINI iliigizwa mwaka 1955
3.
KIPINDI
CHA UHURU
Vile
vile kuna aina tatu
1.
Tamthiliya
za kizungu-ziliendelea kuigizwa hata baada ya uhuru lakini umaarufu wake ulipungua
sana kwa upande wa tamthimini
®
Katika
kipindi hiki tamthiliya za kizungu zilianza kutafsiriwa mfano, JULIUS KAIZA
na ‘MABEPARI WA VENIS- Ilifasiriwa na
mwl Nyerere.
®
Nyingine
ni MAKBETH iliyotafsiriwa na S.S.MUSHI
®
MKAGUZI
MKUU WA SERIKALI iliyotafsiriwa na
C.MWAKASAKA
***Tammthiliya
zilizowahusu waafrika ni Tamthiliya ya Ngugi wa Thiong ya THE BLACK
HERMIT-MTAWA MWEUSI
***MASAHIBU YA
NDUGU JERRO
***I WILL MARRY
WHEN I WANT-na Ngugi
2.
Vichekesho
®
Vilikuwa
vikizungumzia matatizo ya watu wa kawaida. Mf. Ukosefu wa kazi, uhalifu
®
Vilikuwepo
pia vichekesho vya kisiasa.mf siasa ya ujamaa
®
Vilikuwepo
baadhi zilianzishwa na wanasiasa
3.
Tamthiliya
andishi ya Kiswahili
®
Baada
ya uhuru kulitokea mashindano yaliyosimamiwa na Youth Dramma ambayo yalikuwa
mashindano ya uandishi wa drama.
®
Ibrahimu
Husein katika kazi yake ya WAKATI UKUTA ni matokeo ya mashindano hayo.
®
1970-1994
Kulichapishwa kazi nyingi za tamthiliya ya Kiswahili. Mfano wa kazi hizo ni
KINJEKITILE, MASHETANI 1971, JOGOO KIJIJINI NA….1989, ARUSI 1980, KWENYE UKINGO
WA THIM 1989
®
Zingine
za Penina Mhando: HATIA, 1972. TAMBUENI HAKI ZENU 1984 NGUZO MAMA 1982
®
Mwingine.
E.mbogo: GIZA LIMEINGIA 1980, TONE LA MWISHO 1981, NGOMA YA NG’WANAMALUNDI
1988, MORANI 1983, SUNDIATA 1985
HUKO KENYA:
THOMAS
M,---BAHATI NASIBU 1971
C.N CHACHA---MKE
MWENZA 1981
JAY
KITHO------MALIMWENGU ULIMWENGUNI 1983
BIBI ARUSI 1985
MAJARIBIO
KATIKA TAMTHILIYA YA KISWAHILI
Tunapozungumzia
majaribio katika tamthiliya ya Kiswahili tunazungumzia upya wa kazi ya
tamthiliya. Waandishi waliokuwa wakiandika kipindi kile walikuwa wakiongozwa na
mwongozo wa Kiaristotle. Ni vigumu sana kuona tofauti yoyote unapozingalia kazi
hizi labda kwa upande wa maudhui.
Kuanzia mwaka
1970 watunzi wa tamthiliya ya Kiswahili hawakuridhika kabisa na utunzi wa mbinu
ya kiaristotle, hivyo walianza kuchota mbinu kutoka katika sanaa za kijadi.
Ukiangalia tamthiliya kama vile za Penina Mhando, mfano Nguzo Mama, ina muundo
tofauti kabisa-ni mtindo wa ngano, hivyo hii nayo ni tamthiliya ya majaribio
Pia kuna mbinu
ya majigambo, mfano ya Penina Mhando ya HARAKATI ZA UKOMBOZI, lakini pia
SUNDIATA imetumia majigambo. Pia tamthiliya ya KIVULI
KINAISHI imetumia majigombo
Kuna
matumizi ya TENZI SIMULIZI katika baadhi ya tamthiliya za majaribio. Mfano ni
MKWAVA WA UHEHE
Kuna matumizi ya
uganga. Mfano NGOMA YA NG’WANAMALUNDI