Tuesday

VIPENGELE VYA KIFALSAFA KATIKA RIWAYA YA BW. MYOMBEKERE NA BI BUGONOKA

0 comments
CHUO KIKUU CHA DAR ES SALAAM
UDSM-LOGO





IDARA YA LUGHA YA KISWAHILI NA ISIMU
TAASISI YA TAALUMA ZA KISWAHILI
 JINA LA KOZI: : FALSAFA YA KIAFRIKA NA NADHARIA YA FASIHI
MSIMBO WA KOZI: KF 204
MSIMAMIZI WA KOZI: MWL. FESTO.N. JOSTER
SIKU YA KUWASILISHA: ALHAMISI
NA.
JINA
NA. USAJILI
KOZI
SAINI
1.
Gaspery Emanuele K
2016-04-2479
BAK
EGM

SWALI LA MUHULA:
Kwa mifano bayana taja na kujadili vipengele vya falsafa ya kiafrika vinavyojitokeza katika riwaya ya Bwana Myombekere na Bi Bugonoka, juzuu ya kwanza. Vipengele hivyo vinahalisika vipi katika jamii yako ya leo.



Katika kujibu swali hili nimeligawa kaitka sehemu tatu ambazo ni utangulizi, kiini na hitimisho. Katika utangulizi nimeeleza dhana muhimu katika swali, katika kiini nimeeleza vipengele vya kifalsafa  ya Kiafrka vinavyojitokeza katika riwaya ya Bwana Myombekere na Bi Bugonoka katika juzuu ya kwanza na uhalisia wa vipengele hivyo katika jamii.
Odera (1990), anasema Falsafa ni taaluma ambayo kanuni za msingi kuhusu asili, binadamu na jamii huchunguzwa na kujadiliwa.
vilevile Sodipo (1993), anasema falsafa ni udadisi unaohusu dhana na kanuni zinazotuongoz kuhusu uzoefu au mazoea kuhusiana na maadili, dini, sheria, sheria, saikolojia, historia, sayansi ya jamii na siasa.
Hivyo, Falsafa ni mawazo ambayo watu katika jamii wanaamini kuwa ni kweli na yanafanya mawazo hayo kuendelea kutawala misingi ya maisha toka kizazi kimoja hadi kingine.
 Kuhusu falsafa ya Kiafrika wataalamu kama vile Placide Temples (1959), Oruka (1990) na Mbiti (1990). Wameifafanua dhana hii ya falsafa ya Kiafrika kuwa ni fikra au mitazamo wanayoishughulikia Waafrika wenyewe na watu wengine ambao si Waafrika lakini wanakubaliana na mila  na desturi za Kiafrika na fasihi simulizi za Kiafrika. Hivyo falsafa ya Kiafrika ni ile ambayo imejikita katika mifumo ya kijamii, mila, desturi na fasihi simulizi za Waafrika.
 Kwa ujumla falsafa ya Kiafrika ni mawazo ya Waafrika wenyewe juu ya mambo mbalimbali wanayoyafanya kama vile imani juu ya maisha, mila, desturi na jinsi ya kushirikiana katika jamii na kutafuta masuluhisho juu ya changamoto mbalimbali zinazowakabili katika maisha yao ya kila siku.
Katika kujibu swali hili riwaya ya ‘‘Bwana Myombekere na Bi Bugonoka’’ hasa juzuu ya kwanza ndiyo iliyotumika. Riwaya hii imeandikwa na Aniceti Kitereza na kufasiliwa na Gabriel Rugumbika mwaka (1980). Kwa ujumla riwaya hii inazungumzia maisha ya Bwana Myombekere na Bi Bugonoka ambayo yamegubikwa na changamoto za kifamilia kama vile suala la ugumba ambalo Bugonoka alikumbana nalo huku wakifanya juhudi za kadha wa kadha katika kuondoa tatizo la ugumba hasa kupitia kwa waganga hadi walipofanikiwa kupata mtoto aliyeitwa Ntulanalwo.
Katika riwaya hii vipengele mbalimbali vya falsafa ya Kiafrika vimejitokeza, pia ni vipengele vinavyohalisika katika jamii vipengele hivyo ni kama ifuatavyo;
Falsafa ya uchawi, mwanafalsafa Placide Temples anasema Waafrika wanategemea sana nguvu za kichawi. Suala la uchawi limejitokeza katika riwaya ya Bwana Myombekere na Bi Bugonoka hudhihirika hayo pale mwandishi anaposema,
‘‘........kisa kilichonifanya nikafarakana na mume wangu
ni kwa sababu wake wenzangu ndio walinisingizia ya ka
                                    ma mimi niliwashika ulozi kuwa wao ndio walioua watoto
 wangu baba na ndugu zangu wakapata uchungu sana waka
nena ondoka twende pamoja, huwezi tena kukaa hapa saba
bu wachawi hawa wameanza tangu siku nyingi, tazama jinsi
wameharibu utumbo (kizazi) wako, tumeshuhudia wazi pengi
ne wasikuue na wewe pia, nasi tukaambulia bure! Wahenga wetu
walisema, ekilya isoke, kilya n’obwongo ( kilacho nywele kitau
miza na ubongo. Basi ndivyo hivyo wamenitoa.............................
Myombekere akajibu ‘‘Aa! Sivyo, afadhali ingekuwa kama hao wake
wenzako wangesemwa na watu wengine tuu kwamba wao ndio wachawi
wa kupindukia hasa, hawalali nyumbani.
                                                                        (uk- 20)
Yote haya yanadhihirisha kuwepo kwa falsafa ya kichawi. Pia katika jamii suala la uchawi ni halisi hasa katika jamii ya Wasukuma ambapo wachawi hutumia nguvu za kichawi kuua, kuangamiza na kuharibu maendeleo ya watu wengine.
Falsafa ya nguvu uhai, kipengele hiki kinaelezwa na mwanafalsafa Placide Temples ambapo anasema Waafrika wanaamini katika nguvu uhai na wanaona kuwa chanzo kikuu cha nguvu uhai ni Mungu mwenyewe. Nguvu hii upita kwa Wahenga na Mizimu ambapo hupeleka kwa binadamu na binadamu hupeleka kwa wanyama na mimea. Temples anaendelea kusema kuwa Waafrika wanaamini nguvu ya waganga na hivyo mganga anauwezo kubwa wa kupunguza na kuongeza uhai kwa binadamu. Vilevile Temples anajiuliza maswali mbalimbali kuhusiana na suala la waganga mfano, dawa zinawezaje kuponya?  Dawa inawezaje kuua mtu aliye mbali? Ni vipi mtu aliyekufa anaweza kuzaliwa upya, na anasema kitendo cha kupungukiwa nguvu huitwa ‘‘kufwa’’  na kadhalika katika ‘‘The Bantu Philosophy’’ (uk-22) Temples anasema kuwa majibu ya maswali yote matatu, ili uweze kuyajibu lazima uwe mshirika wa mambo yote hayo. Katika riwaya hii suala la nguvu uhai linajitokeza mara nyingi kwani mwandishi amewaonesha wahusika Bwana Myombekere na Bi Bugonoka wakimtegemea Mungu, vilevile wakiamini Mungu ndiye mwanye uwezo mkubwa. Pia wakiwatumia waganga katika kutatua shida zao mfano mwandishi anasema;
                                                ‘‘wewe hutazaa mtoto maishani mwako mpaka kufa! Ijapo nikioa             
                                                Wanawake wengi, nisipojaliwa na Mungu yote hayo ni majivuno    
                                                ya bure’’
                                                                                    (uk-16)
Vilevile suala hili limejitokeza pale msanii anaposema;
                                                ‘‘Myombekere naye akanena, ‘‘hata mimi, tangu wazee wako          
                                                wakuchukue , huwa natembea kwa watu kuwauliza kama hayo
                                                lakini nilipofika kwa mwingine, akaniambia hivi, sasa wewe bila
                                                mke wako nitawezaje kuwaganga? Utarudi siku nyingine na mke
                                                wako ndipo niwajaribie, kwa sababu aaguae ni maulana.’’
                                                                                    (uk-18)
Maelezo hayo yanadhihirisha kuwa Waafrika wanaamini kuwa Mungu ndiye mwenye nguvu uhai kubwa kuliko viumbe wengine. Pia mwandishi ameonesha kuwa Waafrika hawatumii waganga katika kutatua matatizo  yao kwani uamini kuwa mganga ana nguvu uhai kubwa kudhihirisha hayo mwandishi anasema;
                                ‘‘Bugonoka hajahesabiwa kuwa mgumba na mimi hapo niliwaambia
                                                 nyinyi mnajua waganga si vizuri zaidi mngekwenda pamoja nae
                                                ,wapate kumponya? (uk-17)
Vilevile pale mwandishi anaposema;
                                                ‘‘......Kibuguma akaingia ndani, akamtafutia dawa la kabila jingine
                                                Iliyokuwa haifanani na ile ya kwanza, akaitia katika kisonzochake
                                                alafu akamueleza hivi, ‘‘ dawa hii ni sawa na ile niliyoanza kukupa
                                                lakini hii kazi yake ni kutibu ihuzi (ugonjwa wa mchango) ambao                            
                                                ndio unaouwa watoto wako wakiwa bado tumboni mwako.........’’
                                                                        (uk-159)
Haya yanadhihirisha uwepo wa nguvu uhai katika riwaya hii ambapo pia suala hili linadhihirika katika jamii kwani yapo matangazo mengi kuhusu waganga na huduma wanazotoa kama vile kusafisha nyota, mvuto, kurudisha mpenzi na kutafuta au kurudisha mali iliyopotea.
Falsafa ya uduara, Temples anasema kuwa Waafrika hupenda vitu vya umbo la duara kama vile ngoma, nyumba, sufuria, vyungu na sahani kwani uamini kuwa ni vitu vizuri. Kipengele cha uduara kimejitokeza katika riwaya hii kwani mwandishi ameonesha wahusika wakitumia vitu vya duara kama vile ungo, vyungu na mitungi. Mfano mwandishi anasema;
                                                ‘‘ akachukua pembe la mizimu na ungo wake akatoka navyo nje’’
                                                                        (uk-8)
Vilevile mwandishi anaposema;
                                         ‘‘Basi walipo kwisha kazi hiyo, ndipo Nkwanzi,akamtuma             Barongo, leta kile kibuyu cha kuweka mafuta na  oleabya  (chungu cha kuwekea mafuta)   tumtilie mafuta (siagi) ili akifika  aungie nyama hii waliyo mpa. (Uk 97)


                                   
Vilevile katika kudhihirisha suala la uduara katika riwaya hii mwandishi anaonesha majina ya watu, vitu pamoja na miezi inayoanza na herufi ‘o’  ambayo ni ya duara mfano anaposema;
                                                ‘‘mwezi wa omwilaguzu (February)  ulikuwa ni wa saba tangu
                                                Bugonoka atunge mimba’’
                                                                        (uk-273)
Pia mwandishi anaonesha pale anaposema;
                                                ‘‘mwezi wa saba (omwerogwechanda) au ikiralya bubezi (julai)’’
                                                                        (uk-252)
Pia mwandishi anaonesha tena suala ilo anasema;
                                                ‘‘mwenzi wa tisa 9. Omutagato (Septemba) mambo yaonekanayo
                                                Katika mwezi huo ni haya’’
                                                                        (uk-253)
Mambo hayo yanadhihirisha falsafa ya uduara katika riwaya hii ambayo pia yanahalisika katika jamii ya Wasukuma ambao hupenda kujenga nyumba zao katika umbo la duara.
Falsafa ya hofu ya uhai na kifo, Temples anaamini kuwa Waafrika wanahofu juu ya uhai na kifo kwa kudhihirisha hili unaweza kuangalia salamu zao na pia mtu anapopata na ugonjwa huhofu kuwa hawezi kupona na kifo kinamsogelea.katika riwaya hii kipengele hiki kimejitokeza pale mwandishi anaposema;
                                                ‘‘baada ya siku kidogo Yule malkia wa wanawake kule kwake,
                                                alipoona nyama iliyowindwa na Mbwa wake kabla hawajawatuma
                                                kwa mfalme wa wanaume ipo karibu kupungua, bila kuona Mbwa
                                                wake, hapo akatoa tangazo la kuwaalika watu wake wote na
                                                walipo kutanika Bukimbo akawaambia hivi, sikilizeni wanawake
                                                kumbe ukarimo uko wa kujiua. Mimi niliona huruma sana nikatoa
                                                mbwa wangu, wakaenda kwa omukama mwenzangu, kwa sababu
                                                mimi nilidhani labda hao watarudishwa upesi, kumbe sivyo!
                                                Tazameni mpaka leo hii hawaonekani na hakuna hata mmoja
                                                Atokaye kule kuja kutuhakikishia kuwa mbwa walifika ama
                                                Hapana. Basi nilichowaita ninyi wake wenzangu ni hiki, ninaona
                                                Kuwa huyo adui njaa tumemjenga kweli msingi wake  na tena
                                                Itakuwa kweli kutuangamiza sote bila shaka tutakufa tuishe..’’
                                                                                    (uk-198)
Pia kipengele hiki kinajitokeza pale mwandishi anaposema;
                                                ‘‘.............Baada ya Gwaleba kuondoka, ndipo Bugonoka akaamwa
                                                Mbia mume wake hivi, mimi nilikuwa nimekwisha kuogopa niki
                                                Dhani leo tumepata hatia mbaya ya kifo cha mtu mjini mwetu
                                                Mtoto  wa watu huyu tumbaku ya chirangi umuuwie hapa na                                               Watu waje waseme sisi tumemloga!Myombekere akajibu ndiyo 
hata mimi nimejisemea peke yangu moyoni, toba ya Rabii  tumetumwa na nini kumpa kirangi cha tumbako kali hivi kama akifia mjini mwangu humu itakuwa hatia yangu ya kulipizwa kisasi.’’          (uk.175)
hoja hiyo inadhihirisha uwepo wa hofu ya uhai na kifo. Kipengele hiki kinahalisika katika jamii kwani tunaona kuwa yapo mabango mengi yenye kauli mbiu ya ukimwi unaua jihadhari nao, vilevile katika jamii watu uamini kifo kinasababishwa na uchawi.
Falsafa ya maisha ya ndoa,  katika falsafa hii Temples anasema Waafrika wanaamini katika ndoa zao  na ndoa hizo hudumishwa ili kupata watoto. Uhai wa bindamu unaanzia kwenye mimba ambayo ni matokeo ya ndoa. Katika riwaya hii mwandishi anamwonesha mhusika Bi Bugonoka akiangaika kutafuta mtoto ili kudumisha ndoa yake na Bwana Myombekere. Vilevile mwandishi anaonesha maisha ya upweke yaliyo na shida kwa kumtumia mhusika Myombekere wakati ambapo Bugonoka alichukuliwa na wazazi wake, kudhihirisha hayo mwandishi anasema;
‘‘hapo jamaa wa Myombekere wakaanza kuwaka kwa hasira na kupayuka wakamwambia amkatae mke wake, wakisema wewe ni ndugu yetu, sasa unakubali kukaa na mke wako huyu akiwa mgumba hivi uzuri wako wote huu huishie chini! Hivi wewe unadhani kufufuka hapa duniani ni nini? Sii kuzaa na kuacha mbegu yako hapa duniani ikiwa hai ndiyo maendeleo ya ukoo wetu.’’ (uk.1)
                                                  
Falsafa ya ubuntu; ‘Obuntu ni falsafa ya Kiafrika inayo sisitiza mahususiano na ushirikiano wa jamii kama misingi ya maisha bora  na amani katika jamii. Neno Ubuntu  linatoka kwenye neno la Kizulu na Kixhosa  na jamii nyingi za kiafika. Neno la kihaya Obuntu au kwakiswahili utu linabeba kwa kiasi fulani maana yaneno utu. Falsafa ya Obuntu  inatokana na mila na utamaduni wa Kiafrika  ambao umejengwa juu ya maslahi yajamii  zaidi ya maslahi ya mtu binafsi. Msingi wa falsafa hii ni ‘mtu sii mtu bila watu’ kwa Kizulu ‘‘ Umuntu ngumutu ngabantu’’  kwa Kihaya  ‘ ‘Omuntu ti muntu ka ataliho bantu’’. Katika riwaya hii swala la utu limejitokeza sehemu kadha wakadha mfano pale ambapo Myombekere anapo amua kwenda kwa wakwe zake kuomba radhi mwandishi anasema ;
‘‘ Basi Myombekere  alipo maliza mjini mwake  siku kadha wakadha  moyo wake ukazidi kumdunda sana na kumshauri arudi kwa wakwe zake kuomba radhi.(Uk 40)
Kitendo cha Myombekere kwenda kuomba radhi ni miongoni mwa matendo ya utu kwa waafrika. Vilevile kipengele hiki kinajitokeza pale ambapo Myombekere anasaidiwa na watu ku beba mitungi ya pombe kupeleka kwa wakwe zake. Mwandishi anasema
‘ ‘Baada ya kuitoa ile mitungi ya pombe, wakajitwika vichwani. Kila mwanaume alijitwika mtungi mmoja. Wale wanawake wawili walikwenda wakipokezana kibuyu  cha pombe kinachoitwa engunda  yobukanza bwa ninazara (kibuyu cha machicha cha mama mkwe).
 Suala la kushirikiana ni miongoni mwa matendo ya utu katika falsafa za Kiafrika. Kipengele hiki cha kifalsafa kinajitokeza katika jamii za leo hasa jamii ya wasukuma ambayo hishirikiana katika mambo mbalimbali ya kijamii na katika shughuli mbalimbali za kiuchumi kama vile shughuli za kilimo. Vilevile ni wakarimu na hushirikiana na kutiana moyo matatizo yanapotokea

Kuwepo kwa vipengele hivi vya kifalsafa katika riwaya hii ambayo inaakisi jamii yaa waakerebe inadhibitisha kuwa waAfrika wana falsafa yao. Na kupinga madai ya wana magharibi ambao wanadai kuwa Afrika haina falsafa




















MAREJELEO
Kitereza, J. (1980). ‘‘Bwana Myombekere na Bi Bugonoka’’. Dar es salaam: Tanzania Publishing House.
Mbiti, J. (1990). African Religion and Philosophy. New York: praeger Publisher.
Odera, H.O. (1990). Trend in Contemporary African Philosophy. Nairobi: Shirikon Publishers.
Sodipo, J.O. (1993). Foundation of African Philosophy. Ibadan: Ibadan University Press.
Temples, P. (1959). ‘‘ The Bantu Philosophy’’