Friday

Diamond Platnumz kuanza tour yake leo nchini Marekani

0 comments




Supastaa 'Naseeb'Diamond Platnumz anatupa karata yake ya kwanza leo mjini Atlanta kwenye tour yake ya kimuziki nchini Marekani.

Kwa mujibu wa ratiba yake Diamond anatarajia kufanya show 11 nchini humo katika miji mbalimbali. Tour hiyo inayoanza leo Ijumaa Oktoba 8, itafikia tamati Oktoba 31, 2021.

Aidha, Diamond Platnumz amerejea Marekani ikiwa ni miezi kadhaa tangu akanyange ardhi hiyo, alipohudhuruia hafla ya utoaji wa tuzo za BET 2021 ambapo alikuwa anawania tuzo ya Best International Act.

No comments:

Post a Comment