MICHEZO NA NGOMA ZA WASUKUMA (Wigusha na liheba na mbina ja Basukuma)
Hapa duniani kila kabila lina MICHEZO yake ya asili.wasukuma walikuwa na MICHEZO mingi ya asili.Baadhi ya michezo iliyokuwa inachezwa na kabila la wasukuma ni
1-NHEEGA ni mchezo mkubwa sana uliochezwa kati ya kijiji na kijiji
2-MBINA ni mchezo ulishidanisha makundi mawili kati ya BHAGALU NA BHAGIKA.
3-ISOLO ni mchezo uliochezwa na watu wazima pamoja na wazee hadi sasa nitaendelea
4-KWIFUKA ni mchezo wa mieleka
5-KWISHIGA ni mchezo wa riadha
6-KUJIHA ni mchezo wa kuongelea
7-KWICHOLA ni mchezo wa kutafutana
Hizo ni baadhi ya Michezo ya kisukuma.hivyo MBINA KIUAHALISIA sio Tamasha bali ni ushidani wa magroup mawili kati ya BHAGALU NA BHAGIKA
MAJINA YA NGOMA YA WASUKUMA (mina ga mbina ja basukuma)
1-Kadigi ni ngoma ya zamani sana katika history ya wasukuma
2-Lilinda ni ngoma ya watemi iliitishwa na watemi tena mara moja kwa mwaka ilikuwa inachezwa MALYA
3-Bucheye ni ngoma iliazishwa na wachungaji wa ng'ombe.walipokuwa wanatoka kuchunga na wakiwa wameua mnyama
4-wigashe
5-Banungule
6-Bayeye
7-Pajanga
8-Manyule
9-Ndono
10-Kadete
11-Bagobogobo
12-Bulubuka
13-Pondekeja
14-Bubilingi
15-Bakomyalume
16-Sogota
17-N'handala na
18-Ben
NGOMA INAYOCHEZWA SIMIYU (Iding'ha)
Kama kunakitu wachopenda wasukuma wa ukanda wa NTUZU basi ni ngoma mfano
5-6-05 kila mwaka ktk kijiji cha kindwabiye
25-26-05 inachezwa tena Nkololo
30-05 Bariadi
Nimeeleza hapo juu kwa ufupi kuhusu Ngoma za wasukuma hasa hii Mbina.
Hoja yangu hapa nikuwaelewesha wale wote wanataka kupotosha kuhusu mbina ni waombe wote wale ambao mnaita majina ya ajabu.
Nimesikitishwa sana kuitwa kongamano la mbina la wanawake mara TAMASHA MARA WALSHA. HII NI KUPOTOSHA NA KULETA MAANA NYINGINE KABISA.HIVYO NIWAOMBE WABUNGE WA VITI MAALUM MLIOTUMIA MANENO HAYO MYAONDOE KWENYE CRIP ZENU HIZO KAMA HUJUI MAANA YA MBINA KAA KIMYA.
HABARI YA MC KWENYE MBINA HAKUNA MC ILA KUNA MAMAJU KAMA NAYEYE ANATAKA HUO MPUNGA WA MH MBUNGE AANZE KAZI YA UMAJU
PILI WATU WASITUMIE MGOGO WA MBUGE KUJINUFAISHA KAMA HUYO MC ANAYETUTAGAZIA AMEANDAA MBINA KUMBE NI MBUNGE. KAMA NAYEYE ANATAKA UBUNGE WA VITI MAALUM APIGE KAZI NAMSHUKRU KATIBU WA MBUNGE KWA KULIWEKA SAWA. PILI ASIINGILIE MILA ZA WATU
NIKIPATA MUDA NITAENDELEA KUWAPATIA ASILI NA CHIMBUKO LA MBINA
Na MTEMI MOGA