1.1 Utangulizi
Ukitaka kuelewa lugha ni nini uwe unawasikiliza watu wanapozungumza lugha ambayo huielewi
huku jambo lililozungumzwa linakuhusu moja kwa moja .Katika hali kama hiyo wewe mwenyewe
mazungumzo hayo yataonekana ni mwingiliano wa sauti tu ambazo zinakuletea kelele tu.Lakini
wahusika yamkini utawaona wakicheka,wakikutazama ,wakihuzunika ,wakioneshana ishara na
kuonesha hisia zao.Wewe yamkini utaambulia kuona ishara na kupata hisia kutokana na uzoefu wa
jamii utokayo.kimsingi wao huelewana kwa lugha waitumiayo hali hii ndio hujumuiswa na kutoa jibu
la kwamba lugha ni chombo cha mawasiliano.
Swali la kujiuliza :ni kwa namna gani kelele zinazosikika zikitamkwa mara kadhaa na kwa namna
fulani tofauti tofauti ,zinawezesha kuelewana ,kupeana maelekezo ,kuwasilisha ujumbe na kupeana
habari kwa kila muhusika wa kelele hizo.Yamkini wazo unaloweza kupata kwa haraka linaweza kuwa
lazima kelele zitolewazo na wahusika zina maana fulani ijulikanayo kwa wasemaji /watamkaji wa
kelele hizo.
Kwa hakika kelele za namna hiyo zikifikia kiwango cha kuweza kufikisha mawasiliano
juu ya masuala yanayojitokeza katika jamii fulani ndipo kelele hizo huitwa lugha ya jamii husika.
Madhumuni ya Muhadhara
Baada ya kusoma muhadhara huu utaweza:
Kueleza asili ya lugha
Kueleza maana /dhana ya lugha
Kujadili aina za lugha
Kujadili mitazamo mbalimbali ya fasili ya dhana ya lugha
Kujadili tabia za lugha.
Kufafanua sifa za lugha.
7
1.2 Asili ya Lugha
Ni dhahiri kuwa kila jamii ina hadithi zake kuhusu jinsi lugha yake ilivyozaliwa/kuanza.
Lakini katika
historia kuna hadithi nyingi zinazohusu asili/chimbiko la lugha zote za binadamu.Mojawapo ya
hadithi hizo ile inayosimuliwa katika kitabu maarufu kama Biblia inayohusu chanzo cha watu kunena
lugha mbalimbali wakati wa ujenzi wa mnara wa Babeli.Ambapo inasemekana kwamba kulitokea
kutoelewana kwa kila mmoja kuzungumza lugha yake na huo ukawa mwanzo wa lugha mbalimbali
Duniani.Hadithi hii yaelekea kuwa na ukweli kiimani zaidi kwani watu wa imani hii huamini kuwa ni
kweli lakini kitaalumu hakuna kigenzo chochote ambacho kinaweza kidhibitisha ukweli huo.
1.2.1 Mtazamo wa kiisimu
Kiisimu asili ya lugha huweza kutazamwa kwa namna mbili .namna ya kwanza ni ile inayoangalia hali
za mabadiliko ya binadamu toka kale hadi kupata lugha asili ambazo zote ni kamili kwa kiwango cha
kukidhi mahitaji ya jamii fulani. Katika mtazamo huu inaelezwa kwamba lugha huweza kuzuka kukua
na kufa.Namna ya pili ya mtazamo juu ya asili ya lugha ni ule unaozingatia namna motto anavyoipata
lugha.Kimsingi ni dhahiri kwamba hakuna motto anayezaliwa akiwa na lugha au uwezo wa
kuzungumza lugha fulani . Badala yake kila motto huzaliwa katika hali ya kawaida bila lugha lakini
huwa na uwezo wa kupata lugha yeyote ya jamii inayomlea au jamii inayomzunguka.ukiangalia
namna hii utagundua kuwa ili mtoto aweze kupata lugha ni lazima awe miongoni mwa jamii ya
watu.mpaka sasa wataalamu hawajasema lolote iwapo mtoto ataachwa mahali bila kuwa na
mwingiliano na watu /jamii yeyote atakuwa na lugha au atakuwa na athari gani kilugha kutokana na
upweke huo.
Katika ujumla wake umejifunza kwamba chimbuko la lugha linafungamana sana na maumbile
pamoja na mazingira ya mtu binafsi na jamii yake kwa mda mrefu.katika kipengele cha muda
haijajulikana vema muda kamili ni upi na hivyo kupelekea kuwepo na simulizi kuhusu chimbuko la
binadamu na lugha yake.
1.3 Maana ya Lugha
Fasili ya lugha kwa mujibu wa wa crystal (1992) anasema :”lugha ni mfumo wa sauti nasibu, ishara au
maandishi kwa ajili ya mawasiliano na kujieleza katika jamii ya watu”
8
Katika fasili yake ametaja mambo makuu matano ambayo ni mfumo,sauti za nasibu, sautialama na
ishara,jamii ya wanadamu, mawasiliano na kujieleza/kujitambulisha.
Ili kupata dhana nzima ya fasili hii ni muhimu tuangalia kila kipengele katika fasili yake:
1.3.1 Mfumo
Kila lugha ina muundo wake ambao huwa ni fofauti na lugha nyingine.kwa maana hii kila lugha ni
kijisehemu cha miundo iliyopo katika kundi zima la miundo ya lugha duniani.miundo hiyo yaweza
kuwa jinsi maneno yalivyoundwa jinsi maneno yalivyofuatana.hivyo kila lugha ina ruwaza maalumu.
1.3.2 Sauti Nasibu
Hapa ina maana kuwa hakuna uhusiano wa moja kwa moja kati ya neno na kile kinachowakilishwa
katika lugha.Hivyo maana inayowakilishwa huwa ni ya kinasibu tu au inatokana na makubaliano ya
wanajamii/watumiaji wa lugha fulani katika mazungumzo yao ambayo huwa yanatofautiana kutoka
rika moja hadi jingine.
Mfano: Neno MEZA halina maana ya moja kwa moja na umbo linalowakilishwa.
1.3.3 Sauti, Alama na Ishara
Kimsingi kila lugha huteua sauti ,alama au ishara zianazowakilisha wazo au ujumbe.lugha nyingi
hutumia sauti katika mazungumzo wakati baadhi ya lugha hutumia ishara za maandishi katika
mawasiliano na lugha nyingine hutumia alama katika kukamilisha mawasiliano.
1.3.4 Jamii ya Wanadamu
Kimsingi ni wanadamu pekee ndio watumiao lugha na ni jamii zao pekee zinazoteua maneno na
kuyapa maana waitakayo katika jamii hiyo sambamba na jinsi gani miundo ya lugha zao wanataka
ziwe.Viumbe wengine wana njia za mawasiliano ambazo zinatofautiana kabisa na njia za
mawasiliano ya wanadamu.Hivyo lugha huwa ni kwa wanadamu tuu.
1.3.5 Mawasiliano
Katika kueleza dhana nzima ya lugha inafaa kugusa dhima ya lugha hiyo kwa wale waitumiayo.Lugha
hutumika kama njia kuu ya mawasiliano.Kwa kupitia lugha watu huweza kutoa na kupokea ujumbe
9
pamoja na kutolea hisia zao.Kwa kutumia lugha tunasema tukitakacho ili kukidhi mahitaji
yetu.Mawasiliano katika lugha kunaajumuisha kuzungumza ,kuandika,kusoma na hata kutumia
mifumo mingine ya ishara.njia zote hizi ni njia za mawasiliano kwa kutumia lugha.
Katika ufafanuzi wa dhana ya lugha ni muhimu kuzingatia vipengele vilivyojadiliwa hapo juu ilio
kutoa dhana ya lugha kwa upana wake.
1.4 Aina za Lugha
Kwa kutumia msingi wa kutazama hali halisi na mifumo ya sauti na ishara anayoitumia binadamu
kwa ajili ya kukidhi mahitaji yake ya lugha katika jamii,wataalamu wa lugha wameafikiana kutenga
lugha katika aina kuu mbili ambazo ni lugha asili na lugha unde.
1.4.1 Lugha za Asili
Lugha asili ni ile lugha inayohusisha mfumo wa sauti zinazotolewa kwa kutumia ala katika chemba ya
mdomo wa binadamu Lugha asili ina sifa za kuwa na viwango tofauti katika muundo wake,na huwa
na uwezo wa kuzalisha tungo zisizo na ukomo/kikomo.kwa mujibu wa mwanaisimu John
Lyons,lugha asili ina viwango viwili muhimu vya muundo ambavyo ni :
(i) Kiwango cha msingi kinachohusisha vipashio kamili vyenye maana kama vile maneno
(ii) Kiwango kisicho msingi kinachihusisha vipashio ambavyo vyenyewe havina maana lakini
hutumika katika kuunda vipashio vipashio vya msingi.vipashio hivi huwa ni sauti katika lugha
(Lyons 1970:11-13)
Sifa hii ya uwezo wa kuzalisha tungo zisizo na ukomo kimsingi inahusu hasa uwezo wa binadamu wa
kuunda na kuelewa idadi isiyo kikomo ya maumbo ya maneno na sentensi katika lugha yake.hii
hufanyika kiasili bila mhusika kukusudia kutumia kanuni fulani za kisarufi katika lugha yake.Katika
uzalishaji huu mtumiaji wa lugha hutumia sauti fulani ili kupata maneno ya aina fulani.Kwa mfano
kwa kutumia sauti i,m,l na a katika mipangilio mbalimbali ,katika Kiswahili tunaweza kupata maneno
kama imla, lima, lami.
10
Pia kwa kutumia muundo wa aina moja kuweza kuzalisha sentensi nyingi mbalimbali.kwa mfano kwa
kutumia muundo wa wenye KIIMA, KITENZI NA YAMBWA ianwezekana kupata sentensi kama:
Tembo amemla mtu
Mtu amemla tembo
Mwalimu anasoma gazeti
Mama anapika ugali
Mkulima analima karanga.n.k.
1.4.2 Lugha Unde
Lugha unde ni ile inayohusu mfumo wa ishara ambazo binadamu amezibuni na huzitoa kwa kutumia
viungo vyake vya mwili kama mikono,vidole kope za macho n,k maandishi pia huingia kwenye kundi
la hili kwani ni nyenzo mojawapo anazoziunda mwanadamu ili kikidhi mahitaji yake ya
mawasiliano.katika hali ya kawaida lugha hii huwa na maana tofautitofauti kutokana na rika la watu
uhusiano wao,mahali, tukio napengine mahitaji yake.
Hadi leo haijajulikana kama wanyama wana aina gani ya lugha kati ya hizi.chakujiuliza ni je wanyama
wana lugha ?na kama wanayo ipo katika kundi gani?aidha sifa zilizobainishwa zinaelezea kitu
kinachoitwa lugha na kudokeza kwamba si kila njia ya mawasiliano ni lugha katika maana ileile ya
lugha.
1.5 Mitazamo Mbalimbali Juu ya Fasili ya Dhana ya Lugha
Wataalamu wengi wameileza dhana ya lugha tangu miaka ya 1920 na 1930 hususan wanaisimu wa
skuli ya isimu-miundo ambao ni Leonard Bloomfield na Edward Sapir.mawazo yao kuhusu ni lugha
ni kwamba (i)lugha ni ishara (ii)ishara hizo huzihusisha moja kwa moja na ala za sauti zilizomo katika
bomba la sauti,(iii)sauti hizo zimo katika mfumo maalumu,(iv)mfumo huo wa sauti ni
wanasibu(V)kwa kutumia mfumo huo wa nasibu, jamii inayoitumia lugha husika huwasiliana.zipo
fafanuzi nyingine za lugha ambazo zimejikita katika misingi ya Nyanja totauti ya kitaaluma kama
ifuatavyo:
Kwa wanafalsafa wanaona lugha ni chombo cha fikra. Wao huona kwamba mtu hawuzi kufkiri bila
kuwa na lugha hivyo lugha ni chombo cha fikra.
11
Kwa wanazuoni /wanaelimu jamii wanaona kwamba lugha ni namna fulani ya tabia.wao huhusiana
namna mtu anavyotumia /anavyoongea na tabia yake kama mtu anaongea maneno yote kwa ukali
hiyo ndio tabia yake na tofauti yake ni sahihi.
Kwa wanasaikolojia wanaona lugha ni mlango wa kutambua akili za binadamu wao wanaamini
kwamba bila lugha huwezi kutambua akili za watu.
Ama kwa hakika wapo wataalamu wengine ambao huenda wamefafanua zaidi juu ya dhana nzima ya
neno lugha ni jukumu,lako kutafua zaidi juu ya dhana hii.
1.6 Tabia za Lugha
Ama kwa hakika zipo tabia ambazo zinajitokeza kwa kila lugha ,tabia hizo zinaihalalisha lugha fulani
kuwa lugha kwa maana halisi ya lugha.
1.6.1 Tabia ya kukua
Lugha ina tabia ya kukua,lugha inavyozidi kutumika katika jamii huongeza maneno kulingana na
mahitaji, kitendo hicho hupelekea lugha kuwa na tabia ya kukua.Katika mchakato huu maneno ya
zamani hubadilika na maneno mapya hujitokeza,mabadiliko haya hujitokeza kutokana na maendeleo
ya kijamii,maendeleo ya sayansi na teknolojia.mabadiliko haya huwa yanajikita katika nyanja zote za
kimaisha yaani kisiasa kiuchumi na kiutamaduni,kwa mfano kipindi cha maendeleo ya vyama vingi
ndipo tulipopata misamiati ya ngangari ngunguri n.k pia kuna misamiati kama kasheshe,kilimo
kwanza,kompyuta n.k.
1.6.2 Tabia ya kuathiri na kuathiriwa
Lugha ina tabia ya kuathiri lugha na kuathiriwa na lugha nyingine.kwa kawaida lugha inavyochua
maneno fulani kutoka lugha nyingine huwa inaathiri lugha inakochukua maneno wakati lugha
inayopokea maneno yale huwa inakuwa inaathiriwa na lugha ile.ni dhahiri kwamba Kiswahili
kimeathiriwa na lugha ya kiarabu,kibantu,na kiingereza,wakati huohuo Kiswahili kimeathiri lugha
hizo.
12
1.6.3 Tabia ya ubora
Lugha ina tabia ya ubora .Tabia hii ina maana kwamba kila lugha ni bora kwa wale wanaoitumia
.Hakuna lugha iliyobora kuliko nyingine kwani kwa wale wanaoitumia inawafaa.Ijapokuwa upo
uwezekano wa kuwa na bora lugha, bora lugha hujitokeza sana kwenye rejesta ambazo huzingatia
mawasiliano ya kundi fulani na hivyo kuwa na bora lugha badala ya lugha bora.
1.6.4 Tabia ya kujitosheleza
Lugha ina tabia ya kujitosheleza kulingana na mahitaji ya jamii ambayo inaitumia.Tabia hii
hujipambanua wazi kutokana na kujitosheleza kimsamiati kulingana na mahitaji ya jamii husika.
1.7 Sifa za Lugha
Lugha huhalalishwa kuwa lugha kutokana na sifa zifuatazo:
(i) Lugha ni lazima imuhusu Mwanadamu
Ama kwa hakika hakuna kiumbe kisichokuwa mwanadamu (mtu)kinachoweza kuzungumza lugha
kwa maana halisi ya lugha.Lugha ni chombo maalumu wanachotumia wanadamu kwa lengo kuu la
mawasliano.Kwa mantiki hiyo basi sifa kuu ya chombo hiki ni lazima kiwe kinamhusu mwanadamu
na si vinginevyo.
(ii) Sauti
lugha ambayo inamhusu mwanadamu,huambatana na sauti za binadamu zinazotoka kinywani
mwake.Katika jambo hili ni lazima mwanadamu atamke jambo kinyani mwakekwa sauti.Ijapokuwa
mwanadamu anaweza kutumia njia nyingine ya maandisha na akawa amefikia lengo lake la
mawasiliano.
(iii) Lugha ni lazima iwe na utaratibu maalumu
Kama ilivoelezwa kwenye fasili ya lugha kuwa lugha ni sauti zenye utaratibu maalumu.ambao
hupangwa kwa kufuata utaratibu fulani unaokubalika kwa jamii hiyo ya watu.Kwa maana hiyo basi si
kila sauti itokayo kinywani mwa mwanadamu ni lugha,itakuwa lugha iwapo itakuwa imefuata taratibu
zinazokubalika katika jamii husika.mfano mtoto anapolia anatoa sauti lakini hatuwezi kusema kulia ni
13
lugha kwa sababu ni sauti inayotoka kinywani la hasha.Utaratibu wa sauti hizo kwa neon moja hitwa
Sarufi.
Mfano:
(a) Hatusemi.
(i) Juma wimbo anaimba.
(ii) Kitabu changu mimi nimekipoteza.
(b) Jamii imepatana kusema kwa utaratibu ufuatao:
(i) Juma anaimba Wimbo.
(ii) Mimi nimekipoteza kitabu changu.
(iv) Lugha huwa na misingi ya Fonimu.
Lugha hufuata misingi ya fonimu ,ambapo lugha ina vitakwa au vipashio ambayo huitwa
fonimu.wanaisimu wanakubaliana kwa ujumla kwamba fonomu ni sauti yenye uwezo wa kuleta
tofauti katika maana ikipachikwa katika neno la lugha husika.Baadhi ya fonomu za lugha ya
Kiswahili:
1./a/,/e/,/i/,/o/,/u/.
Katika neno {tata} tunaweza kupachika fonimu nyingine na tukapata maana tofauti tofauti kama
ifuatavyo:
{tata}={teta}={tita}={tota}={tuta}
Pia katika neno {taa} tunaweza kuzalisha maneno yafuatayo:
{taa}={tea}={tia}=[toa}={tua}
2./p/,/b/,/t/,/d/,/f/,/k/,/g/,/s/,/z/n.k
Tunaweza kupata maneno kama pawa,bawa,tawa,dawa,chawa,jawa,gawa sawa zawa na maneno
mengi mengineyo.
(v) Lugha hufuata mpangilio wa vipashio unaoleta maana
Lugha ni lazima iwe na mpangilio wa vipashio mpangilio huo huwa unafahamika na
watumiaji wa lugha husika. Katika mpangilio huo ndipo unapotokea muundo wa sentensi
kwa maana kwamba ili sentensi iwe na maana ni lazima vijenzi vya sentensi hiyo view
kwenye mpangilio unaokubalika.katika lugha ya kiwsahili mpangilio huo huanza na
fonomu,neno,kirai,kshazi na hatimaye sentensi.
14
(vi) Lugha Husharabu
Lugha husharabu /hushabihiana hii ina maana kwamba lugha huchukua baadhi ya maneno
kutoka
Lugha nyingine ili kujiongezea msamiati wake. Tabia hii inazisaidia sana lugha
zinazokua.Katika tabia hii lugha ikishachukua neno kutoka lugha nyingine hulifanya neno
lile liendae na maneno mengine ya lugha husika.Kimsingi vitu viwili vinaweza kutokea
katika tabia hii,kwanza lugha inaweza kuchua neno kutoka lugha fulani na kulitumia kama
lilivyo,pili lugha inaweza kuchukua neno kutoka lugha nyingine na kulirekebisha ili liendane
na mfumo mzima wa lugha husika.Vitu vyote hivi kwa neno moja huitwa kusharabu.
(vii) Lugha Inajizalisha
Lugha ina sifa ya kutumia vipashio vyake kujiongezea misamiati/maneno
mapya.Kujizalisha kwa lugha huweza kutokea kwa njia ya kunyambulishaji na mara
nyingine lugha hujipatia misamiati kutokana na urudufishaji.
Unyambulishaji hufanyika pale vipashio vinapopachikwa kwenye mzizi wa neno ili
kuzalisha maneno mengine.
UNYAMBULISHAJI
UAMBISHAJI UNYAMBUAJI
MZIZI
KIELELEZO
Unyambulishaji unahusu kitendo cha kuongeza vipashio mbele na nyuma ya mzizi.
Uambishaji katika Kiswahili hutokea kabla ya mzizi wakati unyambuaji hutokea baada ya
mzizi.
Katika mzizi{-lim-} inawezekana kufanya unyambulishaji na kupata maneno kama:
(a) Yeye Analima
(b) Wewe Unalima
(c) Mimi Ninalima
(d) Wao wanalima
15
Kutokana na mfano wa hapo juu utaona kwamba uambishaji unaopofanyika unaendana sambamba
na upatanishi wa kisarufi kama inavyoonekana katika mfano hapo juu a-d
Hata hivyo katika unyambuaji Kiswahili hujiongezea msamiati kwa kuzalisha maneno mapya,angalia
mifano ifuatayo:
(a) pig=>ku-pig-a=>ku-m-pig-a=>tu-li-m-pig-a
(b) pig-i-a=>pig-ish-a=>pig-ish-an-a=>pig-ik-a
(c) pig-ik-a
1.8 Hitimisho
Lugha ni lazima iwe sauti za kusemwa na binadamu. Sauti hizo za binadamu lazima ziwe na
utaratibu maalumu wa kuwasiliana, na kama hakuna utaratibu maalumu hiyo siyo lugha. Sauti na
milio iko mingi duniani, milio ile inayoweza kuwafanya binadamu wawasiliane ndiyo tunayoiita
lugha.
Lugha lazima iwe na sifa zinazoambatana na tabia za binadamu katika utamaduni wake. Vinginevyo
lugha husika itakuwa si asilia
Zoezi
1. Lugha ni nini ?
2. Jadili sifa za lugha ukitoa mifano muafaka
3. Jadili tabia ya lugha
4. Fafanua dhana zinazokusudiwa na Wana-Isimu wanaodai kwamba :
(a) Lugha husharabu
(b) Lugha ni mfumo wa sauti nasibu
(c) Lugha ni sauti, alama, ishara
(d) Lugha ni mawasiliano
(e) Lugha hutambulisha msemaji
5. Jadili jinsi lugha na watumiaji wake wanavyoshirikiana kitabia katika jamii
husika
16
Marejeo
1. Grimes, B. (2000), Ethnologue, 14th ed. Dallas: SIL.
2. Nkwera, Fr. F. V. (2003), Sarufi, Fasihi na Uandishi wa Vitabu, Sekondari na
Vyuo. Creative Prints Ltd: Dar es Salaam.
3. Habwe, J na Karanja, P. (2004), Misingi ya sarufi ya Kiswahili.
4. Bussman, H. (1996) Routedge Dictionary of language and linguistics.
17
MUHADHARA 2
Nadharia ya Ukuaji wa Lugha
2.1 Utangulizi
Kuna mambo mbalimbali yanayofanya lugha yoyote ikue. Mambo hayo ni kama vile matumizi ya
lugha katika shughuli mbalimbali kama vile:
Shughuli za utawala na kampeni za kisiasa.
Shughuli za kibiashara ndani na nje ya nchi.
Maswala ya Elimu.
Mikutano ya nchi (kitaifa) na kimataifa.
Shughuli mbalimbali za kiutamaduni, muziki, sherehe, nk.
Matumizi ya lugha katika vyombo vya habari kama vile magazeti, redio, televisheni, nk.
Urahisi wa lugha yenyewe katika kueleweka na kuweza kuchukua maneno ya kigeni au
maneno ya utamaduni wa mataifa mengine bila mgogoro.
Urahisi huo wa lugha waweza kuwa katika:
(i) Matamshi yake
(ii) Msamiati
(iii) Miundo
(iv) Maana-:mfano neno moja kuwa na maana zaidi ya moja, nk.
(v) Mwingiliano wa tamaduni mbalimbali na uhamiaji wa kigeni.
(vi) Vita. Husababisha kuchangamana kwa watu wengi pamoja na hivyo huweza
kusababisha lugha ya utamaduni fulani kuenea na kukua haraka ukilinganisha na lugha
za tamaduni nyingine.
18
(vii) Usanifishaji. Husababisha lugha fulani iteuliwe kutumika katika nyanja fulani kama
elimu, utawala, biashara, nk. Na hivyo lugha hiyo hukua. Kutokana na usanifishaji
ndipo tunapata lugha rasmi na lugha ya taifa.
Hivyo kukua kwa lugha ni hali ya kuongezeka kwa msamiati. Msamiati ni jumla ya
maneno yanayotumiwa katika lugha fulani. Ili lugha yoyote ikue lazima msamiati wake
ukuzwe.
Sababu za uundaji wa msamiati/maneno ni kama zifuatazo:
(a) Kwa ajili ya matumizi ya kawaida ambayo huchukua
sura mpya kila siku.
(b) Kwa ajili ya kuweza kutafsiri mengi kutoka lugha yako kwenda lugha ya kigeni au kutoka
lugha ya kigeni kuingia katika lugha yako.
(c) Ili kupata msamiati unaokubalika na shughuli mahsusi kama vile benki, forodhani, Jeshini,
nk.
(d) Kwa ajili ya matumizi ya utamaduni wa watu wa taifa hili
au hata taifa jingine. Jambo la muhimu ni kuona msamiati wa Kiswahili unaendelezwa ili
kukidhi haja ya watumiaji wa Kiswahili katika kupokea maingiliano ya fani mpya za
utamaduni wa kigeni.
(e) Ili kukidhi msamiati wa masomo yote katika lugha yako, ambayo hapa ni Kiswahili.
Madhumuni ya Muhadhara
Baada ya kusoma muhadhara huu utaweza:
Kuielewa dhana ya uundaji wa msamiati
Kujua njia mbalimbali za uundaji wa msamiati
19
2.2 Njia za Uundaji wa Msamiati
Njia zinazojitokeza katika uundaji wa msamiati ni kama ifuatavyo:
Njia ya kutumia mpangilio tofauti wa fonimu au vitamkwa:
Kila lugha ina fonimu au sauti za msingi ambazo hutumika kujenga silabi ambazo nazo hujenga
maneno yote ya lugha husika. Maneno mengi katika lugha huweza kupatikana kwa kubadili
mpangilio wa vitamkwa/sauti-fonimu za lugha husika.
Kwa mfano:
Sauti-fonimu /a/, /o/, /n/ zikibadilishiwa mpangilio kwa namna mbalimbali zinaweza kuzalisha
maneno kama vile:
(i) o-n-a => ona (ii) => noa (iii) => oana.
(ii) Sauti- fonimu /i/m/l/a/tunaweza kupata (i)=> lima (ii)=>imla (iii)=> lami
Njia ya miambatano yaani kuunganisha maneno:
Hapa maneno mawili yanaunganishwa na kuwa neno moja. Kuna aina mbalimbali za miambatano:
(i) Miambatano kati ya jina huru na jina huru.
mwana + hewa mwanahewa
mwana + nchi mwananchi
Afisa + misitu Afisamisitu
(ii) Miambatano kati ya Nomino na Kivumishi.
Mla + mbivu Mlambivu
Mwana + kwetu Mwanakwetu.
(iii) Miambatano kati ya jina tegemezi na jina huru. Jina tegemezi linatokana na kitenzi.
Mpiga + maji Mpigamaji.
Mpiga + mbizi Mpigambizi
(iv) Miambatano kati ya kitenzi na jina.
20
Piga + mbizi pigambizi
Pima + maji pimamaji
Kutohoa maneno:
Kila lugha ina uwezo wa kuchukua maneno kutoka kwenye lugha nyingine ili kukidhi haja ya
mawasiliano kulingana na maendeleo ya jamii. Kiswahili nacho kimechukua maneno kutoka lugha
mbalimbali za kigeni na lugha za Kibantu na kuyatohoa ili kusadifu misingi ya sarufi yake.
Mfano:
(a) Kiingereza:
(i) tractror => trekta => trekita => terekita
(ii) plaugh => plau => pulau
(iii) shirt => sheti => shati
(iv) geography => jiografia => jografia
(v) machine => mashine
(b) Kiarabu:
(i) laki => pokea
(ii) ahadi => milele
(iii) dhaifu => nyonge
(iv) ila => isipokuwa
(c) Kireno:
(i) bibo => bibo
(ii) roda => roda
(ii) mesa => meza
(iii) copa => kopa
(d) Kiajemi:
(i) bandar => bandari
(ii) dirisha => dirisha
(iii) kod => kodi
(iv) pilao => pilau.
21
(e) Kihindi:
(i) achari => achari
(ii) biyme => bima
(iii) ghati => gati
(iv) lakh => laki
(f) Kijerumani:
(i) schule => shule
(ii) hella => hela
(g) Kutoka Lugha za Kibantu
(i) faculty => kitivo kivung ikulu bunge ugiligili kimbele mbele
(ii) pole => pole pole
(iii) kinyume => kinyume nyume
(iv) kimya => kimya kimya
(v) kizungu => kizungu zungu
Kwa njia ya kufupisha maneno:
Njia ya kufupisha maneno inachukua ama herufu ama silabi ya kwanza ya kila neno lililojitokeza
katika jina zima la mahali au kitu funi.
Mfano:
(i) Taasisi ya Uchunguzi wa Kiswahili => TUKI
(ii) Baraza la Kiswahili Tanzania => BAKITA
22
(iii) Chama Cha Mapinduzi => C.C.M
(iv) Baraza la Mitihani la Taifa => BAMITA
Njia ya kutumia mnyambuliko na uambishaji:
Neno jipya huundwa kwa kuunganisha viambishi kwenye mzizi au shina la neno. Njia hii hukuza
lugha bila taabu kwani maneno ya lugha nyingi yanaweza kunyumbuliwa na kuambishwa, kama
ifuatavyo:
(a) Mnyambuliko wa Majina:
(i) taifa => taifisha => taifishwa => taifishiwa. nk.
(ii) soma => somea => somesha => someshea => someshwa => someshewa =>
somesheka => , nk.
(b) Mnyambuliko wa Vitenzi:
(i) piga => pigana => pigisha => pigishwa => pigishia => pigia => pigiana, pigika,
nk.
(ii) cheza => chezana => chezesha => chezeshwa => chezeshea => chezeana =>
chezwa => chezeka, nk.
(c) Mnyambuliko wa Vivumishi:
(i) fupi => fupisha => fupishia => fupishwa => fupishiwa => => fupishana =>
fupishika, nk.
(ii) safi => safisha => safishana => safishia => safishiana => safishika, nk.
(d) Mnyambuliko wa Vielezi:
(i) haraka => harakisha => harakishana => harakishika => harakishia =>
harakishiana, nk.
Njia ya Kutumia Uambishaji
(i) taifa => utaifa, mataifa, utaifishaji, nk.
(ii) piga => kupigana, anapiga, nk.
(iii) safi => msafi, wasafi, nk.
(iv) haraka => kuharakisha, nk.
23
Njia ya kufananisha sauti/umbo:
Baadhi ya maneno ya Kiswahili yametokana na mwigo wa sauti au dhana ya kitu fulani.
Mfano:
(i) Piki-piki- piki-piki => pikipiki,
Neno ambalo limetokana na mwigo wa sauti (mlio) wa chombo husika.
(ii) tu-tu-tu => mtutu (wa bunduki)
neno ambalo limetokana na mwigo wa sauti ya risasi inapotoka kwenye bunduki
baada ya kufyatuliwa.
(iii) kifaru
Hii ni zana ya kivita ambayo imepewa jina hilo kutokana na umbo lake lililofanana
na mnyama aitwaye kifaru.
Njia ya vijenzi/viundaji:
Mara nyingi vijenzi huunda neno ambalo huwa nomino. Vijenzi hupachikwa mwishoni mwa kitenzi ili
kiwe nomino. Maneno yanayojitokeza huwa na maana na ngeli tafauti tafauti.
Vijenzi vitumikavyo ni kama ifuatavyo:
Kijenzi Kitenzi Nomino
{i} jenga mjenzi
linda mlinzi
soma
x
x