Wednesday

AINA ZA SINONIMIA

0 comments

i)                   Sinonimia za kimantiki /logica / synomimes.
Ni sinonimia zinazotokea pale ambapo leksimu mbili au zaidi huweza kubadilishana nafasi katika sentensi afifu zhote pasipo kuathiri masharti ya ukweli ya sentinsi hizo.
Mfano -Lengo, Kusudi, Nia, Dhumuni, Mama anatembea pole pole / Taratibu.  Haraka haraka, Upesi upesi.
ii)                 Sinonimia Kuntu (Absolute Synomimes)
Ni Sinonimia ambazo hutokea pale ambapo Leksimu mbili au zaidi huweza kubadilisha nafasi katika miktadha yote bila athari yeyote ya maana.  Watafiti wanakubaliana kuwa hakuna lugha yeyote duniani yenye sinonimia kuntu.
Hivyo ni vigumu kupata maneno yenye maana sawa kwa asilimia moja.
“Eneo moja wapo linaloaza kuwa na Sinonimia kuntu ni eneo la Silabi”
Mfano             Ving’ong’o au Nazali wakati wote vinaweza kubadilishana
                        Sintaksia        -           Saruji miundo
                        Fonolgia        -          
                        Mofolgia
Elimu viumbe          -           Baiologia
            VYANZO VYA SINONIMIA / SABABU
            Habwe ba jaranja
i)                   Ukopaji wa misamiati
Maneno yakiwa na asili tofauti huleta hali ya Usinonimia.  
Mfano             Neno Shule limetoholewa toka lugha ya kijerumani “Schule “ lakini kuna neno “Skuli “ hili limtokana na School la kiingereza.
Maneno haya yanatumika katika lugha ya Kiswahili wengine wanatumia Skuli na wengine Shule/
ii)                 Jinsia
Hutokana na maneno yanayolejelea ama mwanmke au mwanaume.
Mfano             Hali ya kutokuwa na uwezo wa kuzaa kwa m-ke ni Utasa na Ugumba kwa mwanaume.  Msichana mrembo lakini Mvulana mtanashati Mwanamke aliyefiwa na mume  -  Mjane
Mwanaume aliyefiwa na mke      -  Mgaje
Mwitiko Abee na Naam
iii)              Tofauti za kijiogorafia au Maeneo  Wazungumzaji wa  lugha moja ambao wanaisi katika maeneo tofauti ya kijiografia wanaweza kuwa na maneno tofauti yanayorejelea dhana au kitu kile kile.
Mfano             Zanzibar                    -           Markiti
                        Tanzania bara           -           Soko
                        Tanzania bara           -           Umeme
                        Kenya                         -           Stima
                        Tanzania                    -           Bomba
                        Zanzibar                    -           Mfereji
                        Tanzania                    -           Dala dala
                        Kenya                         -           Matatu
iv)               Taaluma au Uwanja
Taaluma mbili mbili huwa na maneno mbali mbali yanayotumiwa kurejelea kitu au dhana ile ile.
Mfano             katika riwaya kuna Aya lakini ushairi kuna Ubeti, maneno hayo yote hutejelea kitengo au mfululizo wa maandishi.
v)                 Wakati
Baadhi ya Sinonimia huzuka kutokana na wakati.
Mfano             Habwe na Karanja
Kuna neno kama soko kuna mahali liliitwa Utuku
Mfano             Zamani wanyonyaji  - Mabepari  kwa sasa Mafisadi
vi)               Urasimi
Tunarejelea neno lipi ni sanifu kuliko lingine
Mfano             Hela, fedha, pesa – neno rasmi ni fedha 
                        Mpumbavu, mjinga – yanaonekana rasimi kuliko fara, bwege n.k.
vii)            Ujumla na Umahususi  yapo maneno ambayo hutumika kwa jumla na wakati mwingine hutumika kwa umahususi
Mfano             Hamu  neno la jumla  kiu – kinywa, njaa.
viii)          Rika au Umri
Tofauti za umri na rika, yapo maneno ambayo yanaonekana ni ya kitoto zaidi mengine ni ya kiutu uzima.
Mfano             Piga  - mtu mzima / kutandika  chapa – mtoto
ix)               Elimu au Hadhi
Watu wenye elimu tofauti tofauti hutumia maneno tofauti, wakati mwingine huwa ni kutofautisha.
Mfano             neno  Afya – kawaida  na Siha – kitaaluma njema
x)                  Dini
Dini tofauti huwa na maneno tofauti kwa ajili ya kuelezea dhana zinazolingana hasa Waislamu na Wakristo
Mfano             Dhana ya kujinyima chakula kwa minajili ya kupata fadhila za kidini Waislam  -  Saumu na Wakristo   -  Kwaresma  
Mahali pa kuabudia Wakristo  -  Kanisa
Waislamu  –  Msikitini,  Sala  -  Swala
NAMNA YA KUBAINI KAMA NI SINONIMIA KUNTU AU SIO KUNTU
Kuna mbinu kuu 2:-
i)                   Kuangalia miktadha mbalimbali ya matumizi husika ya Sinonimia
ii)                 Katika mazungumzo au katika maandishi
1.         KUANGALIA MIKTADHA MBALIMBALI YA MATUMIZI YA SINONIMIA HUSIKA KATIKA MAZUNGUMZO AU MAANDISHI
            Mfano             Fahamu, Jua, Elewa,  je maneno haya yanatumika kote
·         Nilielewa atakuja, Nilifahamu atakuja
-     Muasherati, kahaba, mzinzi  -  utofauti kidogo kimaana
2.         *  Kutunga sentensi kahaa tofauti kwa kutumia kila Sinonimia kwa sentensi moja kishi kubadilisha nafasi ya kila Sinonimia katika sentensi hizo na kuweka Sinonimia nyingine
            Mfano -Shimo, Tobo, na Tundu
i)                   Hamis alichimba shimo.
ii)                 Suruali ya Festo ina tobo
iii)              Chandarua change kima matundu mengi
iv)               Ni rahisi ngamia kupenya kattika tundu la sindano kuliko tajiri kuingia katika ufalme wa Mungu.
Hizo ni Sinonimia lakini sio Sinonimia Kuntu.
Shimo  -  kubwa, Vifaa  jembe n.k.
Tundu  -  Dogo zaidi
UANTONIMIA / UNYUME
Ni uhusiano wa kimaana baina ya maneno mawili ambayo maana zake ni vinyume yaani maana ya neno moja ni kinyume cha maana ya neno jingine
Mfano             Neno  - Nenda - Rudi          Cheka - Lia                Kubwa  - Dogo
Kuna aina kadhaa
AINA ZA UNYUME AU UANTONIMIA
i)                   Unyume kamilishani / complimentary or simple antonyms.  Ni Unyume ambao unampaka usiopitika ambapo ukanushi wa upande mmoja ni unenetezi wa upande wa pili
Mfano             Mwanamke   -           Mwanaume
                        Hai                  -           Mfu
                        Pata                -           Kosa
                        Kweli                         -           Si kweli
ii)                 Unyume  kadilifu (Gradable)
Ni unyume ambao hamna mpaka usiopitika hivyo huweza kuelezwa kwa makadirio yaliyopo baina ya pande mbili husika.  Ukamohi wa upande mmoja si lazima uwe ni unenko wa upande mwingine (wa pili) kubwa  -  ndogo si lazima kinyume cha kubwa iwe ndogo kwani inaweza kuwa ndogo wastani n.k.
Zito  -  nyepesi inaweza kuwa nzito wastani n.k..
iii)              Unyume elekeana (Relational Antonyms)
Ni unyume unaokuwepo pale ambapo uhusiano baina ya leksimu mbili katika jozi huwa ni wa kiuelekeano yaani Leksimu nyingine kutegema na Uelekeo yaa upande ambako tendo linaelekewa.
Mfano             Nenda            -           Rudi   -    Uelekeo Fulani yaani tenda linaelekewa wapi
                        Panda             -           Shuka
                        Sukuma         -           Vuta
                        Kushoto         -           Kulia
                        Mbele             -           Nyuma
                        Juu                  -           Chini
                        Chomeka       -           Chomoa
iv)               Unyume Rejezi au Tenduzi
Ni unyume ambao huhusisha Leksim ambayo kwazo tendo la Keksim mojawapo kuweza kubadilishwa ili kurejelea kinyube chake.
Mfano             Chomoa         -           Chomeka
                        Ezeka             -           Ezua
                        Ziba                -           Zibua
UHOMONIMIA
Ni hali au uhusiano ambao umbo moja la kiisimu huwa na maana nyingi zisizohusiana.
Mfano             Panda
·         Kusia mbegu
·         Kwea mlima au mti
·         Tawi la mti
Kaku
·         Ugonjwa wa vidole
·         Ganda la yai
·         Ndugu mkubwa wa kiume
UPOLISEMIA
Ni Sifa ya neno moja kuwa na maana nyingi zinazohusiana, au ni hali ya neno kuwa na maana nyingi zinazo husiana yaani maana inakuwa moja lakini inahusiana na vitu vingi
Mfano             Mdomo
                        (N) wingi wake midogo
                        i)  Ni sehemu ya nje ya kinywa inayomwezesha kiumbe kupitisha
     kitu chakula.
ii) Uwazi wa kitu kama chupa ya birika n.k.
iii) Kinywa
Kichwa
i)  Ni sehemu ya mwili wa kiumbe hai
ii)  Ni injini ya gari moshi inayokokota mabehewa
iii) Ni kiongozi wa familia
iv)  Mtu hodari sana katika masomo
              
             UHIPONIMIA
Ni uhusiano wa kiwima baina ya  Maneno ambapo fahiwa ya neno moja hujumuishwa katika fahiwa ya neno jingine.Ina maana kwamba maana za neno Fulani ni sehemu ya maana y neno jingine.  Kuna  neon  moja  jumuishi na madogo madogo na ili uelewe maana ya neno kubwa lazima uhusishe maneno madogo madogo.
Neno lenye maana pana huitwa neno jumuishi nayale yenye maana finyu huita Haponimia
MATUNDA
                                                  Ndizi    Chungwa   Embe  Parachichi
Fahiwa ya neno Ndizi ni sehemu ya fahiwa ya matunda hivyo ukitaka kuifasili ndizi utasema ni aina ya matunda, ili uweze kuelewa maana ya ndizi, chungwa, embe, parachichi ni sehemu ya fahiwa ya neno jumuishi ambayo ni Matunda
UMERONIMIA
Ni uhusiano ulipo baina ya Leksimu inayotaja sehemu na ile inayotaja kitu kizima.
Mfano             Mwili
-          Shingo
-          Kichwa
-          Mabega
-          Miguu
-          Tumbo
Meronimia inahusu kitu na sehemu zake, nikitaka kujua kichwa ni nini nitarejelea sehemu mbali mbali za kichwa
MAANA KATIKA NGAZI YA TUNGO AU SENTENSI
Kuna vipengele 5
i)                   Usawe
ii)                 UtataUkinzani
iii)              Ukinzani
iv)               Upotoo
v)                 Uziadu – dufu
USAWE
Ni uhusiano baina ya sentensi mbili au zaidi zenye kudhihirisha maana moja ya msingi.
Mfano             Sikujua kwamba usingeongea naye abadani
                        Sikufahamu kuwa usingezungumza naye katu
Katika sentensi hizimaneno yanaetofautiana lakini maana ile ile
-          Maelezo yako yalikuwa magumu kueleweka
-          Ilikuwa vigumu kuelewa maelezo yake
Katikasentensi hizi kinachotofautisha ni mpangilio.
AINA ZA USAWE
i)                   Usawe wa kilekisika
ii)                 Usawe wa kimuundo
1.         USAWE  WA KILEKSIKA
Ni Usawe unaotokana na sentensi mbili au zaidi kuwa na maneno yenye maana ile ile ya msingi katika nafasi ile ile.
Mfano            Sikujua kwamba usingeongea naye abadani
                        Sikufahamu kuwa usingezungumza naye katu
Maneno yaliyotumika katika nafasi ile ile yanabeba maana ya msingi
2.         USAWE WA KIMUUNDO
Hutokana na maana ya msingi ya sentensi mbili au zaidi hubaki ile ile japo sentensi zina mpangilio tofauti.  Hapa kinachozingatiwa saidi na muundo wa ile sentensi.
Mfano             Maelezo yake yalikuwa magumu kueleweka
·         Ilikuwa vigumu  kuelewa maelezo yake.
Kilichotofautisha hapa ni mpangilio tu.
Mfano             Hakuna aliyelewa maneno yake ya ajabu
·         Maneno yake ya ajabu hakuna aliyeelewa.
UTATA
Ni hali ambayo sentensi moja huwa na maana au tafasiri zaidi ya moja au huwezi kuelewaeka kwa namna zaidi ya moja.
AINA ZA UTATA
i)                   Utata wa Kileksia / Kileksika
ii)                 Utata wa Kimuundo
UTATA WA KILEKSIA
Ni Utata unaosababishwa na matumizi ya Homonimia na Polisemia
Mfano             Baada ya shida nyingi alifannikiwa kumleta Papa nyumbani
                        Papa               -           Mnyama
                                                -           Mkuu wa kanisa.
Siku hizi bei ya kanga na sh 10,000
-           Ndege
-           Nguo.
            UTATA WA KIMUUNDO
Hutokana na jinsi sentensi ilivyo pangiliwa au umbo la neno au kirai kuwa katika nafasi malumu katika sentensi.
Mfano             -           Wanawake na wanaume waangalifu walikaa  kando.
1.            -           Wanawake walikaa kando
-           Wanaume waangalifu nao walikuwa kando
2.            -           Wanaume waangalifu na Wanaume waangalifu walikaa
Kando
                                    *  Mtoto alilalia maziwa
                                                -           Alikunywa maziwa akalala
                                                -           Alilala juu ya maziwa.
                                    * Ananipenda zaidi kuliko wewe
                                                -           Nyinyi nyote wawili mnanipenda
                                                -           Wewe unanipenda lakini mwenzio ananipenda zaidi yako
            UKINZANI
Ni hali itokeayo pendi kiyambo cha lugha kinapokuwa na sifa Fulani na wakati huo huo hakina sifa hiyo.
Kiambo cha namna hii hunena kwamba mtu au kitu Fulani kina sifa Fulani na wakati huo huo hakina sifa hiyo.
Mfano             Mwanamke Yule ni mwanamke kweli kweli
                        + Me
                                    - Ke
Bibi yangu nikijana kabisa.
                        + Uzee
 - Uzee
            Yule kijana ni mwizi mtakatiu
                        + Mtakatifu
 - Mtakatifu
            Huyu mtoto ni mtu mzima
                        + Uzima
 - Uto Uzima au
                        + Utoto
 - Utoto
Nilikwenda mbele nikarudi nyuma
                        + mbele
 - mbele
            UPOTOO
Ni Ukiushi wa kisemantiki utokeao pindi vijenzi semantiki viwili singanifu vinapounganishwa kueleziea jambo au kitu.
Mfano             Alichora barua kwa guu wa kushoto
·         Viatu vyake vinacheka
·         Kaptura yake inwasha taa
·         Kuchora – haliendani na neno “barua” kifaa kinachotumika kuchora hakiendani na mguu (wa kushoto)
·         Barua – haichorwi
Viatu vyake vinacheka
            *Matumizi holela ya maneno katika lugha na husababisha upotoshaji
  UZIADA – DUFU
Ni urudiaji wa maneno usio wa lazima au usiohitajika ambao hauifany sentensi kueleweka zaidi au haufafanui zaidi maana.
Mfano             -     Mke wangu ni mke wangu
·         Mwizi ni mwizi tu
·         Mwanafunzi ni mwanafunzi tu
·         Mwalimu ni mwalimu

No comments:

Post a Comment