Sunday

Wazazi na Walezi chanzo cha wasichana kukatisha masomo Tarime

0 comments
Picha ya mtandao

Imebainika  kuwa chanzo cha wasichana kufanya vibaya katika Masomo yao  ni tabia ya baadhi ya  Wazazi na walezi wilayani hapa kuwageuza  watoto wao kuwa kitega uchumi Mara baada ya kukeketwa.

Japo serikali inapinga vitendo vya ukeketaji kwa watoto wakike lakini kwa  baadhi ya wazazi wilayani hapa wamekuwa wakifanya jambo hilo ni furaha kwao kwani mtoto akisha kekektwa kwao  tayari ni fursa ya kujipatia kipato.

Diwani wakata ya Binagi wilayani hapa Marwa Chacha  amesema matokeo katika ya sekondari Nyamwigura si ya kuridhisha kutokana na wazazi kutoa kipaumbele kuwaozesha mabinti wao hasa waliokeketwa.

Shule ya sekondari ya Nyamwigura  ni mmoja ya shule zilizojengwa kwa nguvu za  wananchi lakini  kumekuwepo na changamoto ya wanafunzi wakike kutohitimu masomo yao jambo ambalo wazazi wanaliona ni kero kubwa kwao.

Magabe Tai na Helena Mnanka ambalo ni wakazi wa Kijiji cha Nyamwigura walisema wao kama wazazi wamekuwa kikwazo kikubwa cha wasichana wao kushindwa kufikia malengo yao ya masomo na kuishia kuolewa.

"Baadhi yetu tunapenda sana Mali kuliko mafanikio ya watoto wetu, watoto wanafaulu vizuri kwenda sekondari lakini si nyingi anaolewa na baba yake anachukua Mali kutokana na kupenda Mali kuliko Elimu," alisema Tai.

Helena Mnanka anatumia fursa hiyo kuimbo serikali kufuatilia wanafunzi wanaoacha masomo ili kubaini sababu za wako kufanya hivyo.

"Serikali ingekuwa inafanya sensa kwa wanafunzi wanaoacha shule  kabla ya kuingia kidato cha tatu  wangebaini huku kwetu kuwa wanafunzi wengi wanasimamishiwa masomo na kuolewa, jambo ambalo hukatisha ndoto zao," alisema Mnanka.

Naye Anthony  Charles  ambaye ni mkuu wa shule ya sekondari Nyamwigura alisema changamoto kubwa inayozikabili shule za seokndari nchini ni shule hizo kukosa hamasa ya kitaluma inayosababishwa  na wazazi.

"Wazazi wamekuwa kikwazo kikubwa kwa mafanikio ya wananfunzi wetu, wao wamekuwa wakiwatumia wanafunzi has a nyakati za shule na wakati mwingi kushindwa kufuatilia maendeleo yao pale wanapobaki nyumbani hawawaulizi sababu ya kufanya hivyo," alisema Charles.

Katika kuhakikisha wanaboresha utendaji na ufundishaji katika shule ya sekondari Nyamwigura wazazi walifanya harambee ya kununua vifaa kitaaluma katika shule hiyo kwa kuchangia zaidi ya sh, 3 milioni.

Maoni ya mhariri

Wazazi badilikeni wateteeni wanenu( E.mashele)